Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA NASSIR ALI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itarekebisha mitaala ya elimu ili elimu ya ujasiriamali na stadi za maisha ziweze kufundishwa kwa wanafunzi wanaohitimu darasa la saba na kidato cha nne ambao hawatabahatika kuendelea na masomo na hatimaye waweze kuwa na uelewa wa kujiajiri na kujitegemea?

Supplementary Question 1

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.
Kwa kuwa Serikali yetu ya awamu ya tano imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa Taifa la viwanda je, Serikali haioni muda muafaka sasa wa kuandaa mitaala ya stadi za kazi na ufundi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kwa kuwa mahitaji ya dunia sasa yamebadilika, je, Serikali haioni umuhimu wa kufanya marekebisho makubwa ya sera yetu ya elimu ya juu na elimu ya kati ili wahitimu waweze kushindana kimataifa?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, sera zetu mpaka sasa zimekuwa zikizingatia masuala ya kuwezesha stadi za kazi. Suala linalojitokeza katika ugawaji wa rasilimali na kuboresha ili ziendane na uhalisia hiyo ndio inakuwa ni changamoto. Kwa mfano suala la kujifunza kwa vitendo ni jambo muhimu sana, lakini wakati mwingine unakuta kwamba bajeti inapokuwa finyu ule muda wa vitendo unapunguzwa.
Kwa hiyo, Serikali itaendelea kuongeza jitihada katika maeneo hayo ikiwemo kuboresha vyuo vya ufundi kama vile vyuo vya wananchi ambavyo tumeshavichukua kwenye Wizara yetu pamoja na VETA, lakini pia kufungua vituo mbalimbali vya kujifunzia ukiacha katika mfumo rasmi hata mfumo usio rasmi ili baadaye hata wale wanaokuwa wanajifunza kupitia mifumo isiyo rasmi waweze kupata hizo stadi za kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa upande wa elimu ya
juu hivyo hivyo, wanafunzi wamekuwa wakifundishwa, lakini pia tumekuwa tukiangalia nchi mbalimbali zinaenda vipi kupitia workshops ambazo tunabadilishana mawazo, vilevile hata kupitia mitaala yetu. Kwa mfano siku nyuma elimu ya ujasiriamali ilikuwa haipo vyuoni, ilikuwa haifundishwi lakini sasa hivi tunazo degree, masters mpaka Ph.D za ujasiriamali. Kwa hiyo, tumekuwa tukifanya hivi na naamini tutaendelea kuzingatia kadiri tunavyopata mawazo mbalimbali ikiwemo ya kwenu Waheshimiwa Wabunge.

Name

Kiteto Zawadi Koshuma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA NASSIR ALI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itarekebisha mitaala ya elimu ili elimu ya ujasiriamali na stadi za maisha ziweze kufundishwa kwa wanafunzi wanaohitimu darasa la saba na kidato cha nne ambao hawatabahatika kuendelea na masomo na hatimaye waweze kuwa na uelewa wa kujiajiri na kujitegemea?

Supplementary Question 2

MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.
Kwa kuwa mitaala ya elimu Tanzania inazingatia misingi na mahitaji ya kijamii hususan masuala ya utandawazi. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweka somo la computer katika shule za sekondari na msingi?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kimsingi tayari Serikali ilishaanza kuweka masomo ya computer au TEHAMA kwa ujumla katika shule zetu, isipokuwasiyo shule zote ambazo tayari zimeshapata hizo fursa kutokana na miundombinu halisi. Lakini kupitia hii miradi ya REA ambayo sasa karibu kila kijiji kinakuwa na umeme, vilevile karibu taasisi zote za umma ikiwemo shule zitakuwa na umeme. Kwa hiyo, tunaamini kwamba eneo la TEHAMA litaweza kupata nguvu zaidi na tayari wizara inafanyia kazi kuhakikisha kwamba wanafunzi wengi wanapata fursa ya kupata mafunzo hayo.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA NASSIR ALI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itarekebisha mitaala ya elimu ili elimu ya ujasiriamali na stadi za maisha ziweze kufundishwa kwa wanafunzi wanaohitimu darasa la saba na kidato cha nne ambao hawatabahatika kuendelea na masomo na hatimaye waweze kuwa na uelewa wa kujiajiri na kujitegemea?

Supplementary Question 3

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa takribani miaka miwili iliyopita kumekuwa kuna uhitaji mkubwa sana wa mafunzo ya ujasiriamali, lakini kumekuwa kuna walimu wanaofundisha chini ya kiwango. Serikali inasema nini kuwadhibiti walimu hao kwa kupunguza bei lakini pia kufundisha katika viwango ambavyo vinaweza kusaidia walaji ambao wengi ni wanawake?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, somo la ujasiriamali ni somo ambalo linaweza likafundishwa katika ngazi mbalimbali kama ambavyo wengi tunafahamu, ujasiriamali upo katika sura mbalimbali. Kuna ule ambao unakuwa informal ndio wajasiriamali hawa wadogo wadogo wanaanza, lakini kuna ule ambao unakuwa katika ngazi kubwa zaidi. Kwa hiyo kunaile kupata mafunzo ya awali na kupata mafunzo makubwa zaidi. Jambo kubwa ambalo ningependa leo Waheshimiwa Wabunge mlifahamu ni kwamba katika suala zima la ujasiriamali wengi tunafikiria ni ile kufanya biashara, kuuzauza labda vitu au maduka na vitu kama hivyo. Lakini ujasiriamali tunachotamani hasa watu wakifahamu, ni ile namna gani mtu anafanya shughuli zake kwa njia tofauti ili kuongeza thamani, kiasi kwamba hata Waheshimiwa Wabunge kufanya Ubunge pia ni ujasiriamali wa aina yake. Kwa hiyo, naomba tulizingatie katika sura hiyo.

Name

Riziki Shahari Mngwali

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KHADIJA NASSIR ALI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itarekebisha mitaala ya elimu ili elimu ya ujasiriamali na stadi za maisha ziweze kufundishwa kwa wanafunzi wanaohitimu darasa la saba na kidato cha nne ambao hawatabahatika kuendelea na masomo na hatimaye waweze kuwa na uelewa wa kujiajiri na kujitegemea?

Supplementary Question 4

MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na nishukuru kwamba Mheshimiwa Naibu Waziri ameweka vizuri swali ambalo nilitaka kuuliza, ni hiyo hiyo kwamba kuja na misamiati ambayo mwisho wake tunaona kama tunakwama na pale mwanzo akazungumzia mpaka suala la bajeti. Lakini ni vipi Serikali sasa itarudisha katika shule za msingi na sekondari yale mafunzo au taratibu za elimu ya kujitegemea ambapo watoto walikuwa wanajifundisha kupika maandazi, kufuga kuku, kutengeneza mifuko na kazi kama hizo, hizo hazihitaji bajeti wala hazihitaji misamiati lakini watoto wakitoka pale wana ujuzi. Ni lini Serikali itafanya hivyo? Ahsante.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwamba kupitia stadi za kazi wanafunzi wamekuwa wakipata muda wa kujifunza masomo kama hayo. Lakini kuna wakati sera zetu huwa zinakuwa kama zina mgongano kidogo. Kwa mfano kuna wakati tulisema kwamba wanafunzi wasipewe kazi, watoto wasipewe kazi, watu wakachukulia hiyo ni kufuta mpaka hizo stadi za kazi. Lakini kwa kuacha kufanya hivyo, tumejikuta tumerudi nyuma. Kwa mfano, katika shule tunazosema kwamba wazazi wachangie chakula, kwa kweli kupitia mashamba hasa kwa shule zile ambazo zina maeneo huko vijijini wangeweza kulima mashamba yao na wakapata chakula, watoto huku wakiwa wanajifunza na wakati huo wanapata chakula.
Kwa hiyo, mimi nitoe rai yangu kwa shule zote kuona kwamba stadi za kazi hasa kulingana na mazingira yetu ni ya muhimu sana nawapongeza sana shule kama sekondari ya Rugambwa, wao wanafanya vizuri sana.(Makofi)

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. KHADIJA NASSIR ALI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itarekebisha mitaala ya elimu ili elimu ya ujasiriamali na stadi za maisha ziweze kufundishwa kwa wanafunzi wanaohitimu darasa la saba na kidato cha nne ambao hawatabahatika kuendelea na masomo na hatimaye waweze kuwa na uelewa wa kujiajiri na kujitegemea?

Supplementary Question 5

MHE. ALMAS A. MAIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Ni lini Serikali itarudisha mitaala ya shule za upili ili iweze kuzalisha mafundi mchundo na mafundi sadifu kama ilivyokuwa zamani watu hawa walizewa kujitegemea? Ahsante.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi binafsi nikiwa ni mnufaika katika eneo hilo niliweza kutembelea katika shule nyingi ambazo zinatoa mafunzo ya ufundi, ikiwemo Ifunda, Mtwara, Bwiru na kadhalika. Lakini kitu nilichojifunza ni kwamba zile shule baada ya kuzichanganya na wanafunzi ambao wanasoma kidato cha tano na cha sita imejikutwa kwamba kwa upande wa ufundi ni kama vile ufundi haupo. Vilevile baada ya kuwa VETA ina uwezo wa kuingiza wanafunzi moja kwa moja katika masomo ya ufundi sanifu.
Kwa hiyo, ilionekana lile eneo kama linakuwa reduntant, sasa baada ya hapo tuliita timu kutafakari namna gani tunaweza tukaendelea na shule hizo. Jambo tuliloliona ni kwamba kwa hali ya sasa ambayo elimu imeongezeka na shule nyingi zinatoa wanafunzi wanaofaulu vizuri mpaka kidato cha nne, tunafikiria kwamba hizo shule zirejeshwe katika kutoa mafunzo ya ufundi sanifu, lakini baada ya kujenga shule ambazo zitawachukuwa wale waliokuwa wanasoma kidato cha tano na sita ili kusiwe na upungufu katika eneo hilo, kwa hiyo hali halisi ndio hiyo.