Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deogratias Francis Ngalawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ludewa

Primary Question

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA (K.n.y. MHE. MARGARET S. SITTA) aliuliza:- Kwa mujibu wa takwimu za Serikali kumekuwa na ongezeko kubwa la Taasisi za Elimu zikiwemo shule za Serikali na zisizo za Serikali za msingi na sekondari, shule maalum, vyuo vya ualimu na vituo vya elimu ya watu wazima; na kwa kuwa suala la ubora wa elimu ni kipaumbele kwa Watanzania walio wengi. Je, kwa nini Serikali isiunde chombo kinachojitegemea cha ukaguzi wa elimu?

Supplementary Question 1

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa ruhusa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na changamoto nyingi za ukaguzi kwenye shule zetu za sekondari, msingi na vyuo vya ualimu, je, Serikali haioni sasa imeshafika wakati wa kuunda mamlaka au taasisi itakayosimamia ubora wa elimu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Idara zetu za Ukaguzi wa Elimu, shule za sekondari na msingi zimekuwa zikipata changamoto nyingi hasa za vyombo vya usafiri na watendaji. Je, Serikali ina mpango gani wa kuiwezesha Idara hiyo ya Ukaguzi ili iweze kufanya kazi yake katika ubora unaotakiwa?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimesema awali ni kweli Idara yetu ya Ukaguzi inakabiliwa na changamoto mbalimbali hususan katika ukuaji wa sekta ya elimu kama ilivyo sasa hivi.
Mheshimiwa Mwenyemiti, mwanzo idara hii ilikuwa inakaguliwa kupitia kwenye kanda zetu, lakini kwa sasa ni kanda pamoja na Wilaya, hata hivyo tunaona kwamba kuna mapungufu kidogo katika mfumo mzima, na ndio maana kupitia mabadiliko haya ya sheria tutaangalia namna bora zaidi ya kuendesha shughuli ya ukaguzi katika shule zetu za primary, sekondari na vyuo. Hali kadhalika kwa upande wa uwezo wa Idara za Ukaguzi, ni kweli kuna mapungufu hasa yanayotokana na vifaa kama vitendea kazi kama magari, ofisi na Wizara imeshaona hilo na tayari tumeshaanza kufanyia kazi, tayari kuna magari yamekuwa yakipelekwa kwenye Wilaya na mwaka huu tumeagiza magari mengine kwa ajili ya kupeleka kwenye Wilaya nyingine na wakati huo huo tunatarajia pia kwa mwaka huu kuanza kujenga angalau ofisi 100 kwa ajili ya wakaguzi katika Wilaya zetu.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA (K.n.y. MHE. MARGARET S. SITTA) aliuliza:- Kwa mujibu wa takwimu za Serikali kumekuwa na ongezeko kubwa la Taasisi za Elimu zikiwemo shule za Serikali na zisizo za Serikali za msingi na sekondari, shule maalum, vyuo vya ualimu na vituo vya elimu ya watu wazima; na kwa kuwa suala la ubora wa elimu ni kipaumbele kwa Watanzania walio wengi. Je, kwa nini Serikali isiunde chombo kinachojitegemea cha ukaguzi wa elimu?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa suala la udhibiti wa elimu huwezi kutofautisha na udhibiti wa vitabu vinavyoingia kwenye mfumo wa elimu na kwa kuwa imeonekana wazi kwamba taasisi ya elimu ambayo imepewa jukumu la kuthibiti ubora wa vitabu vinavyoingia kwenye mfumo wa elimu imeonekana kuna dosari kubwa. Je, Serikali ina mpango gani wa kurudisha chombo cha ithibati kama ilivyokuwa EMAC huko nyuma ili kudhibiti vitabu vinavyoingia katika mifumo yetu ya elimu na kuacha madudu yanayoendelea sasa hivi?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kurudisha mamlaka zilizokuwa zinafanya juu ya utungaji wa vitabu za wakati huo ni suala ambalo linabidi kuangaliwa zaidi. Kimsingi mapungufu yaliyojitokeza kwa mwaka huu Wizara ya Elimu imeanza kutunga vitabu kwa mara ya kwanza. Kwa hiyo, chombo kama hicho inabidi lazima kijengewe uwezo na ndio maana katika kufanya tathmini ya matatizo yaliyojitokeza, moja ya mambo yatakayoangaliwa ni uwezo wa chombo chenyewe, vilevile hata ushirikishwaji mpana wa wadau mbalimbali ikiwemo watu binafsi na wataalam kutoka katika maeneo mbalimbali.
Kwa hiyo, mimi nadhani kiujasiriamali tunasema kwamba kujifunza ni pamoja na kufanya makosa, lakini yasiwe ya kudhamiria yawe ni ya bahati mbaya. Kwa hiyo, tutaendela kuboresha na kushirikisha wadau wengi zaidi ili kuona kwamba tunapata vitabu vilivyo sahihi.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. DEOGRATIAS F. NGALAWA (K.n.y. MHE. MARGARET S. SITTA) aliuliza:- Kwa mujibu wa takwimu za Serikali kumekuwa na ongezeko kubwa la Taasisi za Elimu zikiwemo shule za Serikali na zisizo za Serikali za msingi na sekondari, shule maalum, vyuo vya ualimu na vituo vya elimu ya watu wazima; na kwa kuwa suala la ubora wa elimu ni kipaumbele kwa Watanzania walio wengi. Je, kwa nini Serikali isiunde chombo kinachojitegemea cha ukaguzi wa elimu?

Supplementary Question 3

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata hii nafasi. Kwa kuwa Mheshimiwa waziri amesema kwamba wana mpango wa kupeleka vitendea kazi na magari katika Ofisi za Ukaguzi wa Elimu, lakini kwa muda mrefu kumekuwa na matatizo makubwa ya ukosefu wa fedha za uendeshaji, unaweza ukapeleka magari kama hakuna fedha za uendeshaji bado hawataweza kufanya kazi; na kwa kwa muda mrefu wakaguzi wamekuwa wakifanya ukaguzi katika shule ambazo ziko jirani tu kwa sababu ya ukosefu wa fedha. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapelekea OC ofisi hizo zote za kanda ili ziweze kufanya kazi yao sawasawa? (Makofi)

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimesema awali ni kwamba kimsingi Wizara imedhamiria kuboresha eneo hili la ukaguzi. Suala la OC limekuwa likiimarishwa kila wakati na ndio maana tunataka kuangalia mfumo mzima, hata ikiwezekana mafungu yao ya upatikanaji wa OC yaende moja kwa moja bila kupitia katika ngazi nyingine.
Vilevile ukaguzi tunaotaka kuuzingatia si tu ule wa kuangalia masomo peke yake, mpaka miundombinu, shule iko wapi? Inafundisha vipi na imesajiliwa katika sura ipi? Kwa hiyo, tunataka kwenda kwenye ukaguzi kwa njia ambazo ni pana zaidi ili kuwezesha kuona kwamba mambo ambayo tunaagiza kupitia sera zetu na miongozo yanatekelezwa pia katika shule zetu za Serikali.