Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Primary Question

MHE. KAPT. GEORGE H. MKUCHIKA aliuliza:- Sheria ya Jeshi la Kujenga Taifa ya Mwaka 1964 (The National Service Act. 1964) imeweka ulazima wa Vijana Watanzania wanaomaliza kidato cha sita kujiunga na mafunzo ya Jeshi la kujenga Taifa kwa mujibu wa Sheria. (a) Je, katika miaka mitatu iliyopita ni vijana wangapi waliomaliza kidato cha sita kila mwaka na kati yao wangapi walijiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa? (b) Je, waliojiunga ni asilimia ngapi wa waliotakiwa kujiunga?

Supplementary Question 1

MHE. KAPT. GEORGE H. MKUCHIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikuwa nasubiri ruhusa yako.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza napenda nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake ambayo si mazuri sana kwa mustakabali wa maendeleo ya nchi yetu. Hata hivyo, kabla sijauliza maswali yangu mawili ya nyongeza, nataka niwapongeze Waheshimiwa Wabunge vijana wa Bunge la 10 ambao kwa hiari yao walijiunga na mafunzo ya Jeshi la kujenga Taifa, walionesha kwamba kuongoza ni kuonesha njia. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, maswali yangu ya nyongeza ni kama ifuatavyo:-
Kwa kuwa Baba wa Taifa alituandalia akafanya JKT kama ndiyo jando, mahali pa kuwafunda, kuwaandaa vizuri vijana wa Tanzania kimaadili, kiuzalendo na kiulinzi; na kwa kuwa sasa inaonekana vijana wengi hawaendi tumeporomoka kutoka asilimia 75 mpaka mwaka huu 23. Je, kwa kutokuwapeleka hawa vijana JKT, Serikali haioni kwamba inachangia kuwaunda vijana ambao hawana maadili, legelege, ambao hawana uzalendo katika nchi yao? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa changamoto zilizoelezwa na Wizara nimezipitia zote ziko ndani ya uwezo wa Serikali. Je, Serikali inaweza kuliahidi Bunge hili kwamba itaunda kikosi maalum cha kupitia changamoto hizi, kuziondoa na kuhakikisha kwamba vijana wote wanakwenda Jeshi la Kujenga Taifa kwa mujibu wa Sheria na kwamba hata kama ikibidi kuomba pesa walete maombi hapa Bungeni; kwa sababu Watanzania tuna uzoefu wa kushughulikia matatizo mbalimbali kaa UPE; na kama mwaka wa jana tulivyopeleka watoto wote kutoka darasa la kwanza mpaka form four wamekwenda bila malipo? Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba vijana ambao hawapati fursa ya kujiunga na Jeshi la Kujenga Taifa, kwa kweli hawawezi kuwa sawa kimaadili na kiuzalendo kama wale ambao wamepitia Jeshi la Kujenga Taifa. Hata hivyo, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi ni kwamba Serikali ina nia na dhamira kubwa ya kuhakikisha kwamba vijana wote wanaomaliza kidato cha sita wanajiunga na Jeshi la Kujenga Taifa, lakini tunakabiliwa na changamoto kama nilivyoziorodhesha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli nakubaliana na Mheshimiwa Mkuchika, kwamba wakati umefika wa kuunda kikosi kazi cha kupitia changamoto zote hizi au tuseme kufanya mikutano na wadau wote kwa sababu moja ya tatizo kubwa ni mihula ya masomo. Wale wanaoanza Chuo Kikuu wanaanza mwezi Septemba jambo ambalo linasababisha tusiweze kuwachukua vijana hawa wote wengine wanakuwa wameshaanza masomo. Kwa maana hiyo ni kukaa pamoja kuangalia ni jinsi gani tunaweza tukafanya marekebisho ya mihula hii, aidha vyuo vikuu au muda ule wa kumaliza form six ili vijana wote waweze kupitia JKT angalau kwa miezi mitatua ambayo inatolewa sasa hivi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto nyingine kubwa ni changamoto ya rasilimali fedha. Jambo hili limekuwa ni kikwazo kikubwa, tutaendelea kuomba bajeti mwaka hadi mwaka ili kuziondoa na wakati huo huo tunajipanga ili JKT liweze kujitegemea. Nadhani hiyo ndiyo njia nzuri zaidi ya kuhakikisha vijana wote wanapita huko.

Name

Wilfred Muganyizi Lwakatare

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Bukoba Mjini

Primary Question

MHE. KAPT. GEORGE H. MKUCHIKA aliuliza:- Sheria ya Jeshi la Kujenga Taifa ya Mwaka 1964 (The National Service Act. 1964) imeweka ulazima wa Vijana Watanzania wanaomaliza kidato cha sita kujiunga na mafunzo ya Jeshi la kujenga Taifa kwa mujibu wa Sheria. (a) Je, katika miaka mitatu iliyopita ni vijana wangapi waliomaliza kidato cha sita kila mwaka na kati yao wangapi walijiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa? (b) Je, waliojiunga ni asilimia ngapi wa waliotakiwa kujiunga?

Supplementary Question 2

MHE. WILFRED M. LWAKATARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Pamoja na majibu aliyoyatoa Mheshimiwa Waziri, takwimu zinaonesha ukweli kwamba changamoto alizozizungumza zinasababisha kupeleka vijana wachache ukilinganisha na idadi ya vijana wanaomaliza kidato cha sita. Nataka kujua, kutokana na ufinyu huo, ni vigezo gani hivi sasa wanavyovitumia katika kuteua vijana wa kwenda kwenye mafunzo haya na wale wasiokwenda watawafanyaje sasa?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa hakuna vigezo maalum vinavyotumika isipokuwa tunachofanya ni random selection. Kwa maana hiyo katika kila shule wanachaguliwa vijana wachache kwa utaratibu wa random. Kwa hiyo, wale wote ambao wanachaguliwa ni wale waliopatikana kwa utaratibu huo; hakuna vigezo maalum kwa sababu wote wanastahili kuchukuliwa, lakini ni kwa sababu ya muda na rasilimali fedha ambazo nimezizungumza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili ni kwamba kwa wale ambao hawajapata fursa ya kwenda huko, kwa sasa hivi hakuna utaratibu wowote uliopangwa, ni matumaini yetu kwamba uwezo ukiongezeka wa kuweza kuwachukua hata wale ambao wamemaliza vyuo vikuu, basi tutafanya hivyo wakati ukifika.

Name

Halima Abdallah Bulembo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KAPT. GEORGE H. MKUCHIKA aliuliza:- Sheria ya Jeshi la Kujenga Taifa ya Mwaka 1964 (The National Service Act. 1964) imeweka ulazima wa Vijana Watanzania wanaomaliza kidato cha sita kujiunga na mafunzo ya Jeshi la kujenga Taifa kwa mujibu wa Sheria. (a) Je, katika miaka mitatu iliyopita ni vijana wangapi waliomaliza kidato cha sita kila mwaka na kati yao wangapi walijiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa? (b) Je, waliojiunga ni asilimia ngapi wa waliotakiwa kujiunga?

Supplementary Question 3

MHE. HALIMA A. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Je, Serikali haioni umuhimu wa kugeuza Kambi za JKT kuwa vyuo vya VETA ili pamoja na mafunzo ya Kijeshi, vijana pia hasa wale wa kujitolea waweze kupata mafunzo ya ufundi? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa kwa sasa, hususani kwa wale vijana wanaoingia kwa kujitolea yana awamu mbili, kuna mafunzo ya Kijeshi ya miezi sita ya kwanza na baada ya hapo kuna mafunzo ya Stadi za Kazi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa Jeshi la Kujenga
Taifa linafanya utaratibu wa kupata usajili wa VETA ili waweze kutoa vyeti hivyo kwa wale wanaomaliza pale JKT. Kwa hiyo ni kwamba, Stadi za Kazi zinatolewa, zitaendelea kutolewa na usajili unatafutwa ili hatimaye vijana wanaomaliza pale siyo tu wawe wamemaliza JKT bali pia waweze kupata vyeti vya VETA. (Makofi)

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KAPT. GEORGE H. MKUCHIKA aliuliza:- Sheria ya Jeshi la Kujenga Taifa ya Mwaka 1964 (The National Service Act. 1964) imeweka ulazima wa Vijana Watanzania wanaomaliza kidato cha sita kujiunga na mafunzo ya Jeshi la kujenga Taifa kwa mujibu wa Sheria. (a) Je, katika miaka mitatu iliyopita ni vijana wangapi waliomaliza kidato cha sita kila mwaka na kati yao wangapi walijiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa? (b) Je, waliojiunga ni asilimia ngapi wa waliotakiwa kujiunga?

Supplementary Question 4

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa katika majibu yake Mheshimiwa Waziri amesema kwamba changamoto kubwa ni kutokana na ratiba za wanafunzi wanaomaliza form six kwenda Chuo Kikuu muda ni mdogo na wanafunzi wanaomaliza kidato cha nne mpaka kuja kuingia cha tano waliofaulu ni miezi nane. Je, anaonaje kuleta sheria hapa ili tuje tubadilishe wawe wanaenda JKT wakati wanasubiri kwenda form five?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema wakati nawasilisha bajeti yangu, kwamba wazo hili lilikuja ni wazo zuri, tulikubali kwamba tutalichukua tukalifanyie kazi kwa sababu kuna wadau wengi wakiwemo Wizara ya Elimu, tupitie nao kwa pamoja tuone uwezekano wa jambo hili. Kwa maana hiyo baada ya mazungumzo na wadau tutaweza kulitolea uamuzi.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. KAPT. GEORGE H. MKUCHIKA aliuliza:- Sheria ya Jeshi la Kujenga Taifa ya Mwaka 1964 (The National Service Act. 1964) imeweka ulazima wa Vijana Watanzania wanaomaliza kidato cha sita kujiunga na mafunzo ya Jeshi la kujenga Taifa kwa mujibu wa Sheria. (a) Je, katika miaka mitatu iliyopita ni vijana wangapi waliomaliza kidato cha sita kila mwaka na kati yao wangapi walijiunga na mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa? (b) Je, waliojiunga ni asilimia ngapi wa waliotakiwa kujiunga?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Mimi ni muumini wa msemo unaosema kwamba mbwa mzee hafundishwi Sheria. Baadhi ya vijana hatutaweza kuwafundisha uzalendo kwa kwenda tu JKT. Enzi za mwalimu kulikuwa na program za kwata mashuleni, tulikuwa tunafundishwa kwata kwa kutumia Bunduki za mbao. Pia kulikuwa na elimu ya kujitegemea ambapo vijana walikuwa wanafundishwa uzalishaji na stadi mbalimbali ambazo zinafundishwa sasa kwenye VETA. Je, Wizara iko tayari kushirikiana na Wizara ya Elimu, kwata ikarejeshwa mashuleni, vijana wakafundishwa ukakamavu kuanzia ngazi za chini na wakati huo huo elimu ya kujitegemea ikarejeshwa mashuleni kama zamani? (Makofi)

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli ni wazo zuri, wanafunzi kufundishwa mapema masuala ya kijeshi pamoja na elimu ya kujitegemea ni wazo zuri. Hata hivyo, kama nilivyosema tupo katika mchakato wa kuunda kikosi ambacho kitapitia changamoto zote; na kwa sababu kitajumuisha pia watu wa Wizara ya Elimu suala hili litazingatiwa ili tuone uwezekano wake.