Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. RASHID A. SHANGAZI aliuliza:- Halmashauri ya Lushoto ina mzigo mkubwa wa kulipa mishahara ya watumishi ambapo inatumia zaidi ya shilingi 28,000,000 kila mwezi kulipa mishahara ya watumishi ambao kimsingi mishahara yao ilipaswa kulipwa na Hazina kupitia Utumishi. Je, ni lini Serikali itawatua wananchi wa Lushoto mzigo huu?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Spika, yapo pamoja na majibu ya Serikali ambayo kimsingi hayajatatua tatizo lengo lilikuwa ni Serikali itutue huu mzigo. Kama utakumbuka ni kwamba mapato ya ndani yanatakiwa yaende kwenye makundi maalum ikiwepo wanawake na vijana zile asilimia 10. Sasa Halmashauri inapotumia pesa zote hizi kwa ajili ya kulipa watumishi ambao ni jukumu la Serikali, je, Serikali haioni kwamba hili linaendana na kinyume na dhana nzima ya utawala bora?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa uhitaji huu
wa kutumia own source kulipa watumishi wa ndani bado unaonekana mahitaji yapo kwa sababu Serikali Kuu haiajiri na kwa sasa wakati wa zoezi zima hili la uhakiki wa vyeti Halmashauri ya Lushoto imepoteza zaidi ya watumishi 115. Serikali inatoa tamko gani la kufidia hili pengo ambalo wafanyakazi hawa wametoka?

Name

Angellah Jasmine Mbelwa Kairuki

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa, pamoja kwamba anasema kwa upande mmoja alikuwa hajaridhika, nimpongeze kwa namna ambavyo amekuwa akifuatilia suala zima la ajira hizi zinazofanyika kwa kutumia mapato ya ndani.
Mheshimiwa Spika, kwanza nipende kusema yafuatayo; kama Serikali hatu-entertain sana ajira hizi kwa kutumia mapato ya Halmashauri. Tunatambua kwamba mapato haya ya Halmashauri au own source yanatakiwa kwenda katika vipaumbele vingi na ndiyo maana tuaendelea kusisitiza ni vema Halmashauri zetu kupitia kwa waajiri ambalimbali na Maafisa Utumishi wahakikishe wanaweka mapendekezo yao na makisio yao ya Ikama ili kipindi ambapo tunaajiri basi waweze kupata mgao wa ajira kwa wakati sahihi bila kuathiri uwezo wao Halmashauri katika kulipa.
Mheshimiwa Spika, tumekuwa tukipata changamoto nyingine, wako ambao walikuwa wakiajiri kupitia hizi own source lakini unakuta hawafuati taratibu. Nipende kuweka angalizo kupitia Bunge lako, mchakato wa ajira hizi za own source unatakiwa usitofautiane na mchakato wa ajira zingine kama zinazofanyika katika Serikali Kuu na kulipiwa na Serikali Kuu, lakini vilevile hata katika sifa na miundo ya kiutumishi inatakiwa pia isiwe compromised, sifa zile zile kwa mujibu wa miundo ya maendeleo ya kiutumishi. Kwa hiyo, nimeona niseme hayo kwanza kabla sijajibu swali lake kwa undani.
Mheshimiwa Spika, nipende kumtoa hofu Mheshimiwa Shangazi, wao walipoleta haya mahitaji walionekana wanauweza kulipa, lakini nimuhakikishie tu katika mwaka huu ujao wa fedha 2017/2018 kwa Halmashauri ya Lushoto tumewatengea ajira nafasi 252 ambapo kati ya hizo kwa kada za afya tumewatengea nafasi 54, kwa upande wa elimu nafasi 132 kilimo nafasi 10, mifugo nafasi tano na nafasi nyinginezo 51.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa watumishi walioathirika katika zoezi la vyeti fake, kama nilivyosema katika siku nne zilizopita, tayari tumeshatenga nafasi 15,000 kwa ajili ya kuzibia zile nafasi 9,932 pamoja na nafasi zingine za ziada zaidi ya 5,000 katika maeneo mbali mbali yenye upungufu mkubwa na mahitaji.