Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. KABWE Z. R. ZITTO (K.n.y MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO) aliuliza:- Hivi sasa yapata miaka 11 utafiti wa mafuta na gesi katika mwambao wa Ziwa Tanganyika kwenye maeneo ya Kigoma, Rukwa na Katavi umefanyika au unaendelea kufanyika. (a) Je, ni nini hali ya utafiti huo? (b) Bonde la Mto Malagarasi nalo limefanyiwa utafiti wa mafuta na gesi; je, hali ya utafiti huo ikoje?

Supplementary Question 1

MHE. KABWE Z. R. ZITTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2011 Serikali iliingia mkataba au ilikubaliana na Kampuni ya Total ya Ufaransa kwa ajili ya utafutaji wa mafuta katika Lake Tanganyika North Block baadae mazungumzo yakafa, mwaka 2014 Kampuni nyingine ya Ras Al Khaimah nayo pia ikawa imepewa zabuni ya utafutaji wa mafuta wa kitalu cha Kaskazini cha Lake Tanganyika, lakini mpaka sasa na kwenye majibu ya Mheshimiwa Waziri hakuna maelezo yoyote kuhusiana na hilo, kuna maelezo ya block ya Kusini peke yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2015 TPDC ilifanya survey katika eneo lote la ziwa na katika majibu ya Waziri hakuna matokeo yoyote ya utafiti kama jinsi ambavyo Mheshimiwa Nsanzugwanko alikuwa anataka kupatiwa taarifa.
Swali la kwanza, Serikali inaeleza nini status ya sasa hivi ya utafutaji wa mafuta katika eneo la Kaskazini mwa Ziwa Tanganyika ambapo Waziri hujalitolea maelezo kabisa?
Swali la pili, nini status ya umeme wa maporomoko ya Mto Malagarasi ambao ni tegemeo kubwa sana la uzalishaji wa umeme katika Mkoa wa Kigoma? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Zitto, nakumbuka tangu wakati wa uwekezaji katika Mto Malagarasi, wakati wa uwekezaji na ufadhili wa MCC alikuwa mbele sana kufuatilia umeme wa Kigoma, kwa hiyo nakupongeza sana kwa niaba ya wananchi wa Kigoma.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nawapongeza sana wananchi pia na Wabunge wa Kigoma wote Mheshimiwa Serukamba Mheshimiwa Nsanzugwanko kwa mshikamano wenu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nijielekeze kwenye maswali mawili ya Mheshimiwa Zitto, status ya utafiti ikoje katika Ziwa Tanganyika. Kwanza kabisa pamoja na maswali ambayo yameulizwa na Mheshimiwa Zitto, kama alivyosema mwaka 2011 kampuni ya Total ilianza kufanya utafiti, lakini kulingana na gharama za uwekezaji ilishindwa na haikuendelea. Hata hivyo, taarifa zake zilitusaidia sana katika utafiti unaoendelea kwa sababu katika taarifa ambazo tulizipata, kampuni kwa kushirikiana na TPDC waliweza kuchora ramani za urefu wa kilometa 20,024 chini ya Ziwa Tanganyika ambazo zinatupa taarifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pili walitathmini taarifa za utafiti za Total za miaka 80 iliyofanyiwa utafiti na makampuni ya nyuma, kwa hiyo, Kampuni ya Total iliacha lakini ilituachia taarifa Mheshimiwa Zitto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo status ikoje, ni kwamba baada ya utafiti huo TPDC mwaka 2014/2015 ilifanya geo-survey katika maeneo ya Ziwa Tanganyika na kwa kweli pesa kubwa sana zilitumika shilingi bilioni 6.96 kwa ajili ya utafiti huo na matokeo yake kwa kweli matarajio ya kupata mafuta katika Ziwa Tanganyika yapo. Hiyo ndiyo status Mheshimiwa Zitto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na mradi wa Malagarasi ni kati ya miradi muhimu sana katika ukanda wa Ziwa Tanganyika, maeneo ya Kigoma na maeneo ya jirani kwa sababu kwa sasa Mheshimiwa Zitto tumekamilisha upembuzi yakinifu na tumeshaanza majadiliano na wawekezaji pamoja na wafadhili wetu, tumepata fedha kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika na mradi ule utagharimu dola milioni 149.5. Kwa hiyo, shughuli zitaanza mwezi wa saba mwakani na zitakamilika mwaka 2019/2020. (Makofi)