Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Uwanja wa mpira wa miguu Lindi ulijengwa tangu mwaka 1957 wakati wa ukoloni wa Gavana Sir Edward Twining na mpaka leo haujafanyiwa maboresho. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuukarabati na kuwa wa kisasa ukizingatiwa kwamba uwanja huo ulikuwa ukitumika kwa ajili ya michezo ya Afrika Mashariki?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nimshukuru Mheshimiwa Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri yenye matumaini. Ninashukuru Serikali inatambua kwamba uwanja ule unahitaji kukarabatiwa na kuwa uwanja wa kisasa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uwanja wa Lindi usifananishwe na viwanjwa vingine vilivyojengwa na Halmashauri. Uwanja wa Lindi ni miongoni mwa viwanja vitatu bora vilivyojengwa na wakoloni mana yake ni kwamba tumerithi kutoka mikononi mwa wakoloni ikiwemo kiwanja cha Mkwakwani - Tanga, kiwanja cha Dar es salaam na kiwanja cha Lindi Manispaa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uwanja ule umewahi kutumika kwa michezo ya Afrika Mashariki, kwa hiyo uwanja unahistoria ya kipekee kwamba timu za Afrika Mashariki zimechezwa katika uwanja wa Lindi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wana-Lindi sasa tunahitaji kuona uwanja ule unabadilika na kuwa uwanja wa kisasa, tunaiomba Serikali ituambie itatusaidiaje kukarabati uwanja ule? Ninajua kwamba Halmashauri haina uwezo wa fedha wa kukarabati uwanja ule na kuwa uwanja wa kisasa, kwa hiyo ninaiomba Serikali ituambie ni namna gani itaweza ikatusaidia kukarabati uwanja na kuwa uwanja wa kisasa?

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, HABARI UTAMADUNI SANAA NA
MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Hamida kwa jinsi alivyokuwa mstari wa mbele kufuatilia suala la ukarabati wa uwanja huu wa mpira wa miguu wa Ilula (Lindi), kwa kweli hii imekuwa ni chachu kubwa sana katika maendeleo ya ukuaji wa soka katika nchi yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niishauri Halmashauri ya Lindi kwamba iweke kipaumbele katika kutenga bajeti kwa ajili ya ukarabati wa uwanja huu. Pili, napenda kuchukua nafasi hii kumjulisha Mheshimiwa Hamida kwamba Serikali inalitambua hili na kutokana na hilo imekuwa ikitoa ushauri kwa TFF kuzisaidia Halmashauri kufanya ukarabati wa viwanja kwa kutumia wadau mbalimbali au wafadhili wa ndani na nje ya nchi, na kwa namna hiyo basi TFF imekuwa ikiweka katika orodha kila mwaka walau viwanja katika Halmashauri mbili hadi tatu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kumtaarifu kwamba uwanja wa Ilula upo miongoni mwa orodha ambayo imewekwa na TFF kwa ajili ya ukarabati. Niseme tu kwamba TFF watakapotaka kufanya ukarabati itabidi waweke mkataba na Halmashauri ya Lindi na mkataba huo unasharti kwamba ni lazima kipaumbele cha matumizi kiwe katika mchezo wa mpira, ahsante sana.

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Uwanja wa mpira wa miguu Lindi ulijengwa tangu mwaka 1957 wakati wa ukoloni wa Gavana Sir Edward Twining na mpaka leo haujafanyiwa maboresho. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuukarabati na kuwa wa kisasa ukizingatiwa kwamba uwanja huo ulikuwa ukitumika kwa ajili ya michezo ya Afrika Mashariki?

Supplementary Question 2

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa Chama cha Mapinduzi kirithi viwanja vilivyokuwa mali ya Watanzania kutoka kwa wakoloni wakati sasa nchi imekuwa ya mfumo wa vyama vingi; na kwa vile Chama cha Mapinduzi kimeshindwa kuitunza mali hii ya mayatima, ni lini Chama cha Mapinduzi kitarudisha viwanja hivi kwa Halmashauri au Serikali ili irudi mikononi kwa Watanzania wote badala ya kuendelea kudhulumu haki hii ya watanzania?[Neno kudhulumu siyo sehemu ya Taarifa Rasmi za Bunge]
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa heshima napenda kuondoa neno kudhulumu na badala yake liwe kuirejesha haki hii kwa Watanzania wote.

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, HABARI UTAMADUNI SANAA NA
MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa hakuna hati yoyote inayoonekana kwamba Chama cha Mapinduzi kimechukua viwanja kutoka kwa mmiliki yoyote, hati zote zinaonyesha ni miliki ya Chama cha Mapinduzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maana hiyo basi napenda kulithibitisha Bunge lako Tufu kwamba Chama cha Mapinduzi kinavifanyia ukarabati viwanja vyake kama zinavyofanya Halmashauri; kwa mfano uwanja wa Singida. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Singida Mheshimiwa Martha Mlata anasimamia zoezi hili, upo uwanja wa Mbeya na wenyewe unafanyiwa ukarabati na Chama cha Mapinduzi kwa kushirikiana na wadau. Ahsante.

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Uwanja wa mpira wa miguu Lindi ulijengwa tangu mwaka 1957 wakati wa ukoloni wa Gavana Sir Edward Twining na mpaka leo haujafanyiwa maboresho. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuukarabati na kuwa wa kisasa ukizingatiwa kwamba uwanja huo ulikuwa ukitumika kwa ajili ya michezo ya Afrika Mashariki?

Supplementary Question 3

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa sababu tunao uwanja wetu wa Taifa (Dar es Salaam) ambao ni wa kimataifa na ili kuutangaza uwanja huo, na ili kutangaza utalii na kuongeza ajira kwa nini Serikali sasa isije na mpango wa kuziomba Balozi zetu nje ili timu zao za Taifa huko ziliko zije kuutumia uwanja wetu wa mpira wa uwanja wa Taifa, na wakimaliza kucheza mpira au baada ya kucheza mpira wachezaji hao waende kwenye hifadhi zetu ili watangaze utalii wa nchi yetu kupitia uwanja wa Taifa?

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, HABARI UTAMADUNI SANAA NA
MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, wazo lake ni zuri, tumelichukua na tutakwenda kulifanyia kazi na tutarejesha majibu, ahsante sana.