Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Masoud Abdalla Salim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtambile

Primary Question

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM (K.n.y. MHE. MARYAM SALUM MSABAHA) Aliuliza:- Tangu mwaka 2005 kumekuwa na changamoto nyingi katika kero za Muungano:- Je, mpaka mwaka 2016 ni kero ngapi zimeshapatiwa ufumbuzi wa kudumu?

Supplementary Question 1

MHE. MASOUD ABDALLAH SALIM: Mheshimiwa Spika nakushukuru, nina maswali madogo mawili ya nyongeza
kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, la kwanza; kwa kuwa Mheshimiwa Waziri ameliambia Bunge na kuwaambia Watanzania kwamba kuna kero 11 ambazo zimeshapatiwa ufumbuzi, naomba Mheshimiwa Waziri ututajie kero zote 11
ambazo tayari zimeshapatiwa ufumbuzi.
Mheshimiwa Spika, la pili; Mheshimiwa Waziri, Benki Kuu ni chombo cha Muungano na kilianzishwa mwaka 1966
baada ya kuvunjika kwa Bodi ya Sarafu ya Afrika Mashariki yaani East African Currency Board. Tangu kipindi hicho gawio la upande wa pili yaani ya Zanzibar imeonekana kwamba gawiwo (shares) hilo la upande wa pili hazitolewi kama ambavyo tulivyoweka shares zetu.
Mheshimiwa Spika, ni tatizo gani la msingi lililopelekea shares zetu za upande wa Zanzibar, kulingana na fedha ambazo tuliziweka, kwamba fedha hizi hazitolewi kama tulivyopangiwa au inavyotakikana kupatiwa sisi kutoka Zanzibar? Kama ni hivyo, sababu hizo ni kwa nini basi isionekane kwamba kuna haja ya haraka kuweza kupatiwa
ufumbuzi na fedha hizo kutolewa upande wa Zanzibar, naomba majibu ya haraka.

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali ambalo limeulizwa na Mheshimiwa Mbunge la kwanza kama ulivyonielekeza ambapo ameomba kujua hizo
kero 11 ni zipi ambazo zimeshapatiwa ufumbuzi naomba kuzisema kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kero za Muungano zilizopatiwa ufumbuzi ni:-
(1) Utekelezaji wa sheria ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.
(2) utekelezaji wa Merchant Shipping Act katika Jamhuri ya Muungano na uwezo wa Zanzibar kujiunga yaani
International Maritime Organization (IMO).
(3) Uvuvi kwenye ukanda wa uchumi wa bahari kuu.
(4) Ushiriki wa Zanzibar katika Jumuiya ya Afrika Mashariki
(5) Uwezo wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kukopa ndani na nje ya nchi.
(6) Wafanyabiashara wa Zanzibar kulalamika kutozwa kodi mara mbili.
(7) Mfuko wa maendeleo ya Jimbo wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
(8) Ongezeko la gharama za umeme kutoka TANESCO kwenda ZECO.
(9) Ushiriki wa Zanzibar na Taasisi za Kimataifa
(10) Ajira ya Watumishi wa Zanzibar katika Taasisi za Muungano.
(11) Utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi asilia. Ahsante.