Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza:- Hapa Tanzania kumekuwepo na migogoro mbalimbali ya ardhi kati ya wawekezaji na wananchi, wakulima na wafugaji, hifadhi na wananchi na baina ya wananchi wenyewe:- (a) Je, Serikali ina mikakati gani ya kupanga matumizi bora na endelevu ya ardhi ili kuondokana na migogoro? (b) Je, Serikali ina mikakati gani ya kuondokana na tatizo la maendeleo ya miji kutokuendana na kasi ya ukuaji wa miji?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Spika, ninashukuru kwa kunipatia fursa ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Moja ya chanzo cha migogoro ya ardhi hapa nchini unatokana na kwamba katika nchi yetu sasa hivi kuna umiliki wa asili ambao unatambulika kwa mujibu wa sheria kama customary right of occupancy na umiliki kwa kupitia hati ambao unajulikana kama granted right of occupancy. Changamoto imekuwa ni kwamba katika umiliki wa asili umekuwa haupewi uzito ule ambao unastahili je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba umiliki wa asili unatambuliwa, unalindwa na kuhakikisha kwamba wamiliki wa asili wanaweza kutumia hati zao zile kwa ajili ya shughuli za kiuchumi.

Swali la pili, ujenzi holela kwenye maeneo mengi hususani katika Jiji la Dar es Salaam limekuwa ni kero kubwa sana. Sasa na moja ya changamoto ni kwamba kumekuwa na hali ambayo watumishi wapimaji pamoja na watumishi Maafisa Ardhi kushiriki katika mikakati hiyo.

Je, Serikali ina mkakati gani na nakumbuka kwamba Mheshimiwa Waziri alishawahi kutoa kauli ya kuwawezesha baadhi ya Wenyeviti wa Serikali za Mitaa pamoja na Waheshimiwa Madiwani kusimamia shughuli ya Mipango Miji na kuwapa ramani ili waweze kusimamia maeneo ya umma na kuzuia uvamizi, je, utekelezaji wa jambo hili umefikia hatua gani?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, sehemu ya kwanza Mheshimiwa ameulizia swali la miliki za asili ili kuwawezesha wananchi wetu, Wizara yangu iko katika mpango kabambe ambao unaendelea katika Halmashauri zote za kuwezesha upimaji katika maeneo ambayo yapo watu waweze kupimiwa na kumilikishwa kulingana na hali halisi katika maeneo wanayoishi. Aidha katika vipao mbele vya upangaji wa miji pia, mpaka sasa Wizara yangu imeshapima Majiji matano, Manispaa 15, Miji 15 na Miji midogo 79, yote hii ni katika kuhakikisha kwamba kunakua na mipango mizuri ambayo itaepusha ujenzi holela na ukuaji holela wa Miji yetu katika maeneo ya nchi hii.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza:- Hapa Tanzania kumekuwepo na migogoro mbalimbali ya ardhi kati ya wawekezaji na wananchi, wakulima na wafugaji, hifadhi na wananchi na baina ya wananchi wenyewe:- (a) Je, Serikali ina mikakati gani ya kupanga matumizi bora na endelevu ya ardhi ili kuondokana na migogoro? (b) Je, Serikali ina mikakati gani ya kuondokana na tatizo la maendeleo ya miji kutokuendana na kasi ya ukuaji wa miji?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE: Mheshimiwa Spika, niliuliza kuhusiana na umiliki wa asili na mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba umiliki wa asili unalindwa, kuenziwa na kutumika kwa wananchi kwa ajili za maendeleo. Lakini la pili, ni kuwawezesha wananchi, Serikali ilitoa tamko kupitia Waziri kwamba Wenyeviti wa Serikali za Mitaa watawezeshwa na kupewa ramani ili waweze kusimamia maeneo yao na kuzuia uvamizi wa maeneo, hilo swali halikuweza kujibiwa.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, nadhani katika kujibu nimeeleza pengine labda hakusikia vizuri, naomba niseme kwamba, suala la maeneo kulindwa kama ambavyo Mheshimiwa Waziri alielekeza tayari katika Jiji la Dar es salaam kwa kuanzia Wenyeviti wote wale wa Mitaa watawezeshwa kupewa ramani za maeneo yao, ili waweze kila mmoja kulinda eneo lake, aweze kutambua wapi ni eneo la makazi, wapi ni eneo la wazi, wapi ambapo pamepangwa kwa ajili ya kujenga ili watu waepukane na kuvamia viwanja na kufanya ujenzi usio na utaratibu.

Mheshimiwa Spika, swali lake lingine aliongelea suala la umilikishaji wa asili kwa maana ya kupata zile hati za kimila, nadhani nimeliongelea kwamba Halmshauri zinaendelea katika utaratibu huo na ndiyo maana kumekuwa na msisitizo wa kuwa na zile masjala katika maeneo yao ili pale ambapo mwananchi anakuwa amepimiwa eneo lake na tayari Kijiji kinakuwa au Mtaa unakuwa na hati yake, basi waweke pia na eneo la kuhifadhi. Maana yake huwezi kuwa na Mmliki wa Asili na kutoa hati ambazo huna namna ya kuweza kuzihifadhi, maeneo yote wameelekezwa kuwa na masjala ambazo zitatunza na tunaimani kwamba hati hizi zinawapa uwezo wananchi kiuchumi kwa hiyo suala hilo Wizara inaitilia kipaumbele ni wajibu wa Halmashauri zote kuzingatia na kufuata utaratibu huo.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. DKT. FAUSTINE E. NDUGULILE aliuliza:- Hapa Tanzania kumekuwepo na migogoro mbalimbali ya ardhi kati ya wawekezaji na wananchi, wakulima na wafugaji, hifadhi na wananchi na baina ya wananchi wenyewe:- (a) Je, Serikali ina mikakati gani ya kupanga matumizi bora na endelevu ya ardhi ili kuondokana na migogoro? (b) Je, Serikali ina mikakati gani ya kuondokana na tatizo la maendeleo ya miji kutokuendana na kasi ya ukuaji wa miji?

Supplementary Question 3

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Spika, nashukuru kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa muda mrefu kumekuwa na migogoro katika nchi yetu baina ya wananchi na hifadhi, lakini tatizo hili limekuwa haliishi kwa Wizara hizi mbili ya Ardhi na Maliasili kukaa pamoja na kumaliza matatizo haya.

Nahitaji kufahamu kutoka kwa Serikali ni lini Wizara hizi mbili watakaa pamoja kumaliza migogoro ya Wananchi katika Vijiji ambavyo vinapakana na hifadhi mfano, Wananchi wangu wa Wilaya ya Babati na hifadhi ya Tarangire.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Gekul, Mbunge wa Babati na Mjumbe wa Kamati ya Ardhi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba iko migogoro inayosababishwa na mipaka kati ya Vijiji na Hifadhi za Misitu, Hifadhi za Wanyama na migogoro hiyo tunaijua na ni kweli kwamba hata katika maeneo anayotoka Mheshimiwa Mbunge ya Tarangire na sehemu nyingine tuliiona hiyo. Sasa tumekubaliana ndani ya Serikali katika awamu hii ni kuhakikisha kwamba aina hii ya migogoro yote tunaiondoa, na ndiyo maana nimeandika barua kuwapeni Waheshimiwa Wabunge nafikiri mtapewa leo. Nimeomba kila Mbunge aniambie aina ya migogoro iliyopo katika maeneo yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, najua kama Serikali tuna utaratibu wetu wa kupata taarifa lakini nilitaka nipate taarifa za pande mbili. Iko migogoro kati ya vijiji na vijiji, iko migogoro kati ya mipaka ya vijiji na vijiji na Wilaya, iko migogoro kati ya vijiji na Hifadhi za Misitu na wanyamapori na mengine, kwa maana hiyo tukipata hizo taarifa na zile tulizoagiza Mikoani sisi kama Serikali tutakaa pamoja.

Najua hapa tunahusika, Waziri mwenzangu wa Maliasili anahusika, Waziri wa TAMISEMI anahusika tutakaa pamoja na tutaunda timu na sisi tutakwenda pamoja kuhakikisha kwamba tunaondoa migogoro hii kwa manufaa ya Wananchi wetu.