Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Serikali inatambua uwepo wa Wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji ambao wanatekeleza majukumu yao moja kwa moja na wananchi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalipa posho viongozi hao kama inavyofanya kwa Madiwani?

Supplementary Question 1

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Pamoja
na majibu mazuri ya Serikali, sote tunajua kazi za Wenyeviti, wamekuwa wanafanya kazi nzuri sana katika mitaa na vijiji vyetu, lakini hakuna hata siku moja wamelipwa posho.
Nataka Serikali iniambie leo ni lini itapanga kiwango cha kuwalipa Wenyeviti hawa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Wenyeviti hawa wamekuwa wakifanya kazi katika mazingira
magumu sana, wakati huo hawa ndio wasimamizi namba moja wa usalama katika vijiji na vitongoji vyetu, wanatatua migogoro kila siku, watoto wa mitaani wakipotea, wanapelekwa kwenye Wenyeviti, tukigombana usiku break ya kwanza kwa Wenyeviti, sote tunajua kazi za Wenyeviti.
Je, Serikali ipo tayari kuwapa hata usafiri angalau baiskeli za kuwasaidia?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni kweli kama anavyosema Mheshimiwa Bupe, Wenyeviti wetu wanafanya kazi kubwa sana katika vijiji, hili jambo halipingiki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kusema lini? Naomba nizungumze wazi, kwa sababu tulikuwa na changamoto
kubwa hapa nyuma, hata ukija kuangalia Halmashauri zetu, hata kupeleka zile fedha, Halmashauri nyingine ilikuwa
inaonekana kama ni hisani. Ndiyo maana sasa hivi tunafanya haya marekebisho na muswada huu utaingia Bungeni wakati wowote. Hivi sasa umeshaiva na wadau wameshiriki vya kutosha. Katika Sura ya 290 kifungu cha 54 kinafanyiwa marekebisho na Waziri mwenye dhamana sasa atapewa utaratibu wa kuweka kama misingi ya kisheria, kuzielekeza Halmashauri sasa kupeleka zile fedha. Mwisho wa siku ni kwamba aidha, Halmshauri wataweza kupata hasa Wenyeviti wetu wa vijiji ambao tunatambua kwamba wanafanya kazi kubwa sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika suala la usafiri, ni kweli kama nilivyosema ni kwamba utakuta sehemu nyingine
Mwenyekiti wa Kijiji anatoka kitongoji kimoja anakwenda kitongoji kingine, changamoto yake ni kubwa. Vilevile kwa sababu kama tutaweka utaratibu mzuri wa kisheria na hata ukiangalia sheria, sehemu inayozungumza mambo ya expenditure pale, inazungumza kama kuna matumizi ya fedha nyingine zinazoweza kutumika kwa maslahi mapana ya kujenga eneo hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika utaratibu huo tukishafanikiwa vizuri, basi tutatoa maelekezo ya kutosha kuona jinsi gani tutafanya, tutaangalia na rasilimali fedha zilizopatikana angalau kama itawezekana baadhi ya vipando hasa baiskeli, lakini maelekezo hayo yatakuja baada ya kurekebisha sheria yetu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge jambo, lako ni la msingi na Serikali tunalifanyia kazi kama nilivyozungumza.

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Serikali inatambua uwepo wa Wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji ambao wanatekeleza majukumu yao moja kwa moja na wananchi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalipa posho viongozi hao kama inavyofanya kwa Madiwani?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya
Mheshimiwa Waziri, Halmashauri nyingi zina mapato kidogo na kwa vile baadhi ya vyanzo vya mapato Serikali Kuu
imevichukua, kwa hiyo, ina maana kwamba baadhi ya Halmashauri hazitaweza kulipa Wenyeviti kwa mujibu wa
majibu ya Mheshimiwa Waziri alivyosema hapa. (Makofi)
Je, Serikali ina mpango gani mbadala kuhakikisha kwamba Wenyeviti wote, regardless wanatoka kwenye
Halmashauri ipi na wenyewe waweze kupata malipo kama haya?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kuna wakati mwingine marejesho yanakuwa siyo rafiki sana, ndiyo maana katika utaratibu wa sasa inawezekana Wabunge wengine watauliza kwamba property tax imechukuliwa imeenda Serikali Kuu, tunafanyaje na haijaridi? Hili hata Waziri wa Fedha baadaye akija ku-table bajeti yake hapa katika mjadala mpana baadaye, itaonekana ni jinsi gani tutafanya. Lengo letu ni kuziwezesha Halmashauri zetu cha kutosha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu changamoto hii hata Waheshimiwa Wabunge wengine wanaweza
wakasimama baadaye wakasema hata Madiwani wengine wamekopeshwa kwenye mabenki, wanataka kupelekewa mahakamani, ndiyo maana nasema katika mchakato huu mpana, mara baada ya kurekebisha sheria, kwa sababu sheria ile itakuja hapa mtaona kwamba Waziri mwenye dhamana atakuwa anapata fursa ya kuhakikisha Halmashauri zinaenda vizuri, kwa sababu zimewekwa kwa mujibu wa Katiba, Ibara ya 145 na utelekezaji wake Ibara ya 146.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Waziri mwenye dhamana amepewa mamlaka hiyo kwa utaratibu wa sheria
za nchi Sura namba 287 na 288 ile ya vijijini na ile ya miji. Kwa hiyo, katika kurekebisha Sheria ya Fedha, itamsaidia sana Waziri mwenye dhamana kufanya maamuzi hayo mwisho wasiku kwa kuangalia jiografia ya Halmashauri hizi ambapo zenyewe zinatofautiana katika nguvu ya kimapato.
Halmashauri ya Ilala huwezi ukafananisha na Halmashauri ya Kakonko kwa mwalimu wangu pale, hizi zinatofautiana. Kwa hiyo, Waziri mwenye dhamana atakuwa anapata nafasi nzuri kuiangalia nchi kwa upana wake na kuangalia hizi Halmashauri, Madiwani na Wenyeviti ili kazi iende vizuri.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA aliuliza:- Serikali inatambua uwepo wa Wenyeviti wa Vitongoji na Vijiji ambao wanatekeleza majukumu yao moja kwa moja na wananchi. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwalipa posho viongozi hao kama inavyofanya kwa Madiwani?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na kilio cha muda mrefu cha Madiwani nchini kutokupata nyongeza ya
posho kwa muda mrefu. Ni ukweli usiopingika kwamba Madiwani hawa wamekuwa wakifanya kazi kubwa hasa
kutusaidia sisi Wabunge tukiwa huku Bungeni muda mrefu, lakini Madiwani hawa wamekuwa wanasimamia fedha
nyingi sana zinazopelekwa katika Halmashauri zetu, lakini wameachwa hawana mafunzo, hawana vitendea kazi na
posho zao haziongezeki.
Je, Serikali sasa iko tayari kumaliza kilio cha Madiwani cha muda mrefu katika nchi hii?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli
anavyosema Mheshimiwa Paresso na tukifanya reference ya mwaka 2002 kulikuwa na Tume iliyokuwa inaitwa Tume ya Lubeleje ambaye ni Mbunge senior yuko hapa. Tume hiyo iliundwa na iliweza kubaini mambo hayo. Bahati nzuri katika mikitano yetu ya ALART miwili tuliyofanyia hapa Dodoma na Musoma, jambo hilo vilevile lilijitokeza. Serikali hivi hatuwezi kutoa kauli hapa haraka haraka kwa sababu mchakato huu wa bajeti tutakuja ku-table bajeti na mambo mengine tutajadili kwa pamoja hapa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kazi ya Madiwani ni kubwa na Serikali inaona hilo, lakini tutajadiliana kwa upana
katika mchakato wa bajeti tuone ni nini tunafanya, way forward katika suala zima la Madiwani wetu katika Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania.