Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

John Peter Kadutu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. JOHN P. KADUTU aliuliza:- Katika Jimbo la Ulyankulu, Kata za Milambo, Igombemkulu na Kamindo bado hazijafanya uchaguzi:- Je, ni lini Kata hizo zitafanya uchaguzi?

Supplementary Question 1

MHE. JOHN P. KADUTU: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninamuomba awahakikishie wananchi wa Kata hizo kwa sababu siyo wote ni wakimbizi, ni lini zoezi hilo la naturalization litakamilika ili kusudi nao wapate kutimiza haki yao ya kidemokrasia?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, mchakato pale ulikuwa ni mpana sana, kama alivyosema pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba zoezi lile lilikamilika na kuhakikisha Kata zinapatikana lakini ilikuwa ni baada ya uchaguzi, baada ya hapo kuna zoezi kubwa la integration ambalo linafanyika ambalo lina-involve pesa na awali mchakato uliokuwa unaendelea ni suala zima la kupata fedha kutoka Benki ya Dunia.
Mheshimiwa Spika, lakini kwa sababu Serikali ime-invest vya kutosha kuhakikisha wakimbizi hawa wanakuwepo maeneo haya kipindi chote, maana yake Serikali ya Tanzania ilitumia jukumu kubwa la kiutu na kiubinadamu na resources nyingi sana kuhakikisha wakimbizi hawa wanakuwepo, lakini suala la kuhakikisha unajenga miundombinu ni jambo lina-involve pesa.
Kwa hiyo, Serikali iko katika mchakato kuangalia jinsi gani tutafanya, suala la kujenga structure zikamilike baadaye basi uchaguzi uweze kufanyika, kwamba sasa eneo lile uchaguzi ufanyike rasmi baada ya kuwa na muundo rasmi wa Serikali za Mitaa. Ahsante.
SPIKA: Ahsante sana, tunaendelea na Ofisi ya Rais, TAMISEMI, swali linaulizwa na Mheshimiwa Mwita Mwikabe Waitara, Mbunge wa Ukonga, kwa niaba yake tafadhali endelea.