Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maftaha Abdallah Nachuma

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA Aliuliza:- Gesi inayochakatwa Mtwara huweza kuzalisha viwanda vidogo vidogo ikiwemo mbolea na kwa miaka mingi wananchi wa Mtwara wamekosa fursa ya ajira ukilinganisha na maeneo mengine ya Tanzania kama vile Arusha, Mwanza, Kilimanjaro na kadhalika. Je, ni lini Serikali itasitisha usafirishaji wa gesi kutoka Mtwara kwenda Kinyerezi ili wana Mtwara waweze kunufaika na ajira zinazotokana na uchakataji wa gesi hiyo asilia kufanyika Mtwara na Seriakli kujenga viwanda vitokanavyo na gesi Mtwara?

Supplementary Question 1

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante, nishukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, hata hivyo nina maswali mawili ya nyongeza.
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2013 wananchi wa Mtwara waliweza kuandamana kwa kiasi kikubwa sana Mtwara na Lindi wakidai namna gani kwamba rasilimali hii gesi inaweza kuwanufaisha na tunashukuru hivi sasa manufaa
hayo yanaanza kuonekana. Nilikuwa naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba ule mpango wa kuwapa wawekezaji ambao wana nia ya kuwekeza Mtwara gesi waweze kutengeneza ama wajenge viwanda vya mbolea umefikia wapi mpaka hivi sasa?
(b)Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa naomba kujua, kulikuwa na mkakati na mwaka jana tulielezwa ndani ya Bunge hili kwamba kuna usambazaji wa gesi asilia kwenda majumbani kwa mana kwamba mikoa ya Dar es Salaam na maeneo mengine. Nilikuwa naomba kujua mkakati huu kwa Mkoa wa Mtwara na Lindi upoje kwa sababu tulipewa tu taarifa kwamba upembuzi yakinifu umeshaanza nataka kujua mimi kama Mbunge sina taarifa nao. Ahsante sana.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Maftaha kwa kweli kati ya Wabunge ambao wanahangaikia sana maslahi ya wananchi wake ni pamoja na Mheshimiwa Maftaha. Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusuaiana na maswali yake ya msingi kabisa, kwanza kabisa ujenzi wa kiwanda cha mbolea Mtwara; nataka tu nimwambie Mheshimiwa Maftaha pamoja na wananchi wa Mtwara na Lindi kwamba hatu ailiyofikiwa sasa hivi; kwanza kuna
Kampuni ya HELM kutoka Ujerumini imeshapata eneo kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanda cha mbolea na makadirio ya kukamilisha ujenzi huo ni mwaka 2020 lakini hata hivyo nimwambie tu hatua ambazo zinafanywa na Serikali. La kwanza kabisa; Serikali kupitia TPDC wanafanya majadiliano sasa ya kuelewana sasa bei ya kununua gesi kati ya TPDC pamoja na Kampuni ya HELM itakayojenga kiwanda hicho na kwa sasa wameshaonesha kutenga jumla ya dola za Kimarekani milioni 200 kwa kampuni hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini taratibu za kuuziana gesi wakishamaliza kujenga ujenzi huo 2020 wataweza kupewa gesi na mahitaji ya kiwanda hicho cha mbolea inafikia milioni 80 futi za ujazo mpaka 104; kwa hiyo matarajio yapo na wananchi wa Mtwara watanufaika na kiwanda
hicho.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala la pili; ni kweli kabisa tulitarajia sana tuanze usambazaji wa gesi majumbani katika mji wa Mtwara na Lindi na Dar es Salaam pia, lakini tumefikia hatua nzuri. Upembuzi yakinifu umekamilika, matarajio yameshapatikana na kwa sasa Mtwara na Lindi wanahitaji milioni tano za gesi hadi kumi futi za ujazo ambazo zinagharimu shilingi bilioni mbili, Kwa hiyo kuanzia Julai mwaka huu, Wananchi wa Mtwara, Lindi na Dar es Salaam wataanza sasa kupata gesi ya majumbani. Na Mheshimiwa Maftaha wale wananchi wako wale wa Mbawala chini pamoja na Mtajitambua wataanza kupata gesi asilia.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA Aliuliza:- Gesi inayochakatwa Mtwara huweza kuzalisha viwanda vidogo vidogo ikiwemo mbolea na kwa miaka mingi wananchi wa Mtwara wamekosa fursa ya ajira ukilinganisha na maeneo mengine ya Tanzania kama vile Arusha, Mwanza, Kilimanjaro na kadhalika. Je, ni lini Serikali itasitisha usafirishaji wa gesi kutoka Mtwara kwenda Kinyerezi ili wana Mtwara waweze kunufaika na ajira zinazotokana na uchakataji wa gesi hiyo asilia kufanyika Mtwara na Seriakli kujenga viwanda vitokanavyo na gesi Mtwara?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza kwenye swali la msingi.
Mheshimiwa Naibu Spika, eneo la Ziwa Tanganyika ni eneo ambalo kumefanyika utafiti wa gesi na mafuta hasa kwenye Tarafa ya Karema. Eneo hilo kuna uhakika wa kupatikana mafuta na gesi, je, Serikali inawaambia nini wananchi wa Mkoa wa Katavi na ukanda mzima wa Ziwa
Tanganyika juu ya utafiti ambao umefanywa mpaka sasa? Ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa utafiti umeshaanza kufanyika katika Ziwa Tanganyika ili kugundua gesi iliyopo na makampuni yaliyopita kufanya ni makampuni mawili ya Chuo Kikuu cha Ujerumani pamoja na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na wanajiolojia wa Tanzania pamoja na TPDC.
Mheshimiwa Naibu Spika, kinachofanyika sasa ni
kuanza kufanya appraisal ili kujiridhisha na gesi iliyopatikana. Zipo dalili za kugundua lakini kinachofanyika sasa niappraisal na shughuli ya kukamilisha appraisal itafanyika mwezi Agosti
mwaka huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo baada ya Agosti mwaka huu Mheshimiwa Kakoso wananchi wanaozunguka Ziwa Tanganyika wataanza kupata gesi asilia katika maeneo hayo.

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA Aliuliza:- Gesi inayochakatwa Mtwara huweza kuzalisha viwanda vidogo vidogo ikiwemo mbolea na kwa miaka mingi wananchi wa Mtwara wamekosa fursa ya ajira ukilinganisha na maeneo mengine ya Tanzania kama vile Arusha, Mwanza, Kilimanjaro na kadhalika. Je, ni lini Serikali itasitisha usafirishaji wa gesi kutoka Mtwara kwenda Kinyerezi ili wana Mtwara waweze kunufaika na ajira zinazotokana na uchakataji wa gesi hiyo asilia kufanyika Mtwara na Seriakli kujenga viwanda vitokanavyo na gesi Mtwara?

Supplementary Question 3

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kuuliza swali la nyongeza kama ifuatavyo; zipo hisia kwa wananchi wa Mkoa wa Mtwara kwamba Wizara ya Nishati na Madini haina nia ya dhati na kiwanda cha mbolea
cha Msanga Mkuu cha HELM ambacho amekielezea uwekezaji wake. Kwa sababu majadiliano yamechukua muda mrefu na ujenzi ambao ameusema utakamilika mwaka 2020 kuanza kwake ujenzi itategemea makubaliano ya bei ya kuuziana gesi.
Je, anatoa kauli gani juu ya hisia za wananchi wa
Mtwara kwamba kiwanda hcho hakitazamwi vizuri ndani ya Wizara yake hasa ukizingatia hata kwenye jibu lake la msingi hakukitaja kiwanda hicho?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Hawa Ghasia katika jibu langu la nyongeza nimeeleza mikakati ya Serikali ya kujenga kiwanda hicho.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia nimeeleza hatua ya majadiliano ya gesi kwa sasa nikupe taarifa Mheshimiwa Hawa Ghasia na mimi nakushukuru sana unavyohangaikia maendeleo ya wananchi wa Mtwara Vijijini, Kampuni ya
Helmo kutoka Ujerumani inapendekeza kwa sasa hivi ichukue gesi kwa dola 2.6 wakati ukifanya hivyo Mheshimiwa Hawa na wewe unajua makadirio ya gharama ya chini kabisa
katika standard price ulimwenguni kote na hapa kwetu ni dola 4.2.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Mheshimiwa Ghasia nikuhakikishie tu jitihada za makusudi zinafanyika kuhakikisha kwamba wananchi wa Mtwara wanapata gesi, lakini matumizi ya mbolea pia. Kwa hiyo, hatua tunayochukua majadiliano kati ya Kampuni ya HELM kwa kiwanda cha mbolea pamoja na Serikali yatakuwa yamekamilika na kiwanda cha mbolea kitaanza sasa kutekeza katika ujenzi.
Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2020 waliosema ni makadirio yao ya kampuni kuwa wamesha-set taratibu zote na ujenzi wa kiwanda hicho kukamilika. lLakini jitihada za Serikali ziko pale pale. Ahsante sana.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. MAFTAHA A. NACHUMA Aliuliza:- Gesi inayochakatwa Mtwara huweza kuzalisha viwanda vidogo vidogo ikiwemo mbolea na kwa miaka mingi wananchi wa Mtwara wamekosa fursa ya ajira ukilinganisha na maeneo mengine ya Tanzania kama vile Arusha, Mwanza, Kilimanjaro na kadhalika. Je, ni lini Serikali itasitisha usafirishaji wa gesi kutoka Mtwara kwenda Kinyerezi ili wana Mtwara waweze kunufaika na ajira zinazotokana na uchakataji wa gesi hiyo asilia kufanyika Mtwara na Seriakli kujenga viwanda vitokanavyo na gesi Mtwara?

Supplementary Question 4

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.
Wilaya ya Liwale iko katika Mkoa wa Lindi na ndiyo Wilaya pekee ambayo bado mpaka leo hii inatumia umeme wa mafuta na mashine zile tumezitoa Rufiji, mashine zile zimechoka. Nini kauli ya Serikali kuipatia umeme wa gesi Wilaya ya Liwale ili tuweze kuwa na umeme wa uhakika?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, hadi sasa katika umeme tunaotumia hapa nchini 50% ya umeme tunaotumia unatokana na rasilimali ya gesi.
Kwa hiyo, hata huko Liwale tunachofanya sasa hivi tunajenga miundombinu ya kusafirisha umeme kutoka Mtwara kuja Lindi utakaokwenda katika Wilaya za Liwale, Tandahimba, Nanyumbu pamoja na Masasi umbali wa kilometa 80 ili kupunguza umbali wa kilometa 206 zilizopo sasa. Lengo ni kuunganisha umeme wa gesi katika maeneo yote ya Mtwara na Lindi na maeneo ya jirani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Mheshimiwa
Mbunge wa Liwale tunakuhakikishia kwamba kwa sasa hivi hata wananchi wa Liwale sasa wataanza kutumia umeme wa gesi.