Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kemirembe Rose Julius Lwota

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KEMIREMBE J. LWOTA Aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha miradi ya maji inayojengwa Wilayani Sengerema katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa inakamilika haraka na kuwanufaisha wananchi wa Buchosa hasa mradi wa maji wa Lumea - Kalebezo na Nyegonge?

Supplementary Question 1

MHE. KEMIREMBE J. LWOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri ila nina maswali mawili ya nyongeza. Mheshimiwa Naibu Spika wote tunafahamu tatizo la maji na tunajua kabisa maji ni uhai na hakuna Mbunge hata mmoja humu ndani ambaye tutamsimamisha ambaye Jimbo lake halina tatizo la maji.
Mheshimiwa Naibu Spika ifike mahali kama Serikali tuwe na vipaumbele vichache ambavyo tutaweza kuvitekeleza kiuhakika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, katika
mradi huo wa Nyamazugo - Buchosa mradi huo wa maji unapita katika vijiji vya Isenyi, Nyamabanda na Nyanzenda ambapo ndiyo chanzo cha maji kinaanza na unaenda kutekelezwa kwenye vijiji vingine zaidi, swali langu, ni lini Serikali itafikisha maji katika vijiji hivi vichache ambavyo maji yanapita na kwenda kutekelezwa kwenye vijiji vingine?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, katika Wilaya ya Sumve kwenye vijiji vya Kadashi na Isunga kumekuwepo na mradi wa maji ambao umekaa unasuasua kwa miaka mingi. Je, ni lini Serikali itamaliza mradi huu wa Wilaya ya Sumve? Ahsante

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, hoja ya Mbunge ni kwamba kuna chanzo cha maji lakini kuna vijiji jirani ambapo maji yanatoka kwamba kwa mujibu wa design vijiji
vile vitakosa maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tufanye rejea ya Mheshimiwa Waziri wa maji kwamba na Waziri wa Nishati na Madini kwamba kwa mkakati wa Serikali ya hivi sasa ni kuhakikisha kwamba maeneo yote ambayo vyanzo vinapatikana basi vitapewa kipaumbele jinsi gani kuweka design kama mwanzo vilisahaulika kuweka utaratibu wa
kuweka design nzuri ya kuhakikisha maeneo yale ambayo vyanzo vinapatikana yaweze kupata maji.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba nikuhakikishie kwamba Serikali hii itafanya kila liwezekanalo wananchi wa eneo lako lile lazima wapate maji kutokana kwamba lazima Serikali iweze kuwahudumia wananchi wale, lakini siyo hivyo tu, na wao watasaidia kuweza kulinda vizuri
chanzo cha maji katika eneo lile. Lakini katika eneo la Sumve ni kwamba kuna mradi wa maji lakini mradi huu unaonekana kwamba haujakamilika, ni commitment ya Serikali na
naomba tufahamu, siyo mradi huo peke yake karibu kuna miradi mingi sana ilianza kutekelezwa lakini mingi ilisimama huku nyuma naona flow ya fedha lilikuwa siyo nzuri, lakini hivi sasa kwa Seriakli ilivyojipanga ni kwamba mradi sasa hivi
mkandarasi akikamilisha kazi, aki-submit certificate maana yake certificate inalipwa na mkandarasi anaendelea kufanya kazi. Kwa hiyo, naomba niwahakikishie kwamba Serikali itajitahidi kwa kadri iwezekanavyo miradi yote ambayo ilikuwa ime-stuck sasa wakandarasi waweze kutimiza wajibu wao, wakamilishe ile miradi, wa-raise certificate zitalipwa ilimradi lengo la miradi iweze kukamilika na miradi hiyo iweze
kuwapata wananchi.

Name

Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Primary Question

MHE. KEMIREMBE J. LWOTA Aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha miradi ya maji inayojengwa Wilayani Sengerema katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa inakamilika haraka na kuwanufaisha wananchi wa Buchosa hasa mradi wa maji wa Lumea - Kalebezo na Nyegonge?

Supplementary Question 2

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Waziri nilitaka kufahamu wakazi wa
Mkoa wa Katavi wamekuwa wakisubiri sana mradi ambao unaendelea kujengwa mradi wa maji wa Ikolongo B, wakazi wa Kata ya Ilembo, Misunkumilo, Kakese pamoja na maeneo mengine mradi huu umepita nyuma ya hizo Kata, lakini wakazi hawa wanakosa maji lakini pia wanatumia maji ambayo ni mchafu ya kutoka kwenye mabwawa pamoja na mito. Sasa naomba unieleze kwamba ni lini mradi huu utakamilika kwa sababu Serikali tayari ilishatenga pesa lakini mradi bado unasuasua? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna baadhi ya sehemu zingine kwamba miradi inasuasua na mnakumbuka kwamba hata Mheshimiwa Rais alivyofika Mkoa wa Lindi aliweza kutoa maelekezo mahususi kwa mkandarasi anaejenga mradi wa maji pale katika Mji wa Lindi na hii ina maana kwamba maana yake ni maeneo mbalimbali kulikuwa na tatizo kubwa hasa baadhi ya wakandarasi wanaoshindwa kutimiza vizuri wajibu wao, wengine wameomba kazi lakini baadae wakienda kule site wanashindwa kutimiza wajibu wao, lakini naomba nikuhakikishie kwamba Serikali hivi sasa inafanya vetting kwa Wakandarasi wote ambao wanashindwa kutimiza wajibu wao, lengo kubwa ni kwamba atakaposhindwa bora atolewe aletwe mkandarasi mwingine aweze kutimiza wajibu wale na Mkandarasi huyu tutaenda ku-assess kazi yake
inaendaje. Lakini hata hivyo ulizungumza ajenda suala zima la kwamba Wananchi wengine ambao wa maeneo yale wanakosa maji, tutafanya mahitaji halisi kuangalia kwa sababu siwezi kuzungumza hapa moja kwa moja kule site
sijaangalia lakini najua suala hilo linamhusu hata ndugu yangu Richard Mbogo, Mbunge wa Nsimbo pale nilivyofika nae ana hoja hiyo hiyo inayolingana ni kwamba tutaangalia kwa kina
tutafanyaje lengo kubwa ni kwamba wananchi wote wa Tanzania kama lengo la Serikali hii kuwatua wakina mama ndoo ya maji liweze kufikia; haliwezi kufikia lazima tupambane wote kwa pamoja, aliyekuwa mzembe tumtoe katika daraja hilo la uzembe awe katika suala zima la sawa sawa wananchi wapate huduma ya maji.

Name

Ezekiel Magolyo Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. KEMIREMBE J. LWOTA Aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha miradi ya maji inayojengwa Wilayani Sengerema katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa inakamilika haraka na kuwanufaisha wananchi wa Buchosa hasa mradi wa maji wa Lumea - Kalebezo na Nyegonge?

Supplementary Question 3

MHE. EZEKIEL M. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Serikali ilikamilisha mradi wa maji wa Ziwa Victoria mwaka 2008 na kwa bahati mbaya kuna baadhi ya vijiji ambavyo bomba limepita kwenye vijiji hivyo vikawa
vimesahaulika na toka mwaka 2014/2015 vijiji kama Kabondo, Mwakuzuka, Matinje, Buluma, Mwaningi ambavyo bomba limepita wala si kilometa 12 bomba limepita kabisa kwenye
vijiji hivyo viliwekwa kwenye mpango kwamba vingepatiwa maji lakini hadi sasa vijiji hivyo havijapata maji kwa sababu fedha hazijatoka.
Mheshimiwa Naibu Spika, nilitaka kusikia uhakikisho kutoka kwa Waziri kwamba ni lini sasa vijiji hivi vitapata maji kama ilivyokuwa imeahidiwa toka miaka yote niliyoisema?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli ajenda inayozungumzia ni suala zima la mradi wa maji wa Ziwa Victoria ambayo hivi sasa hata ukiangalia mradi huu hata watu wa Tabora hujo watakuja kusimama mpaka Sikonge, lakini kuna mpango mkubwa sana wa kuhakikisha kwamba maji haya yanafika mpaka Tabora mpaka Sikonge, lakini kuna changamoto ya baadhi ya vijiji vingine vilivyopitiwa lakini maji havikupata na Mheshimiwa Waziri wa maji alikuwa
akizungumza mara kadhaa hapa Bungeni kwamba lengo kubwa la Serikali ni kuangalia kwa sababu maji yanakwenda kwa utaratibu maalum, lazima yafike katika tanki halafu yaweze kurudi kwahiyo yote inatakiwa ku-design ili iweze kufanyika lakini Waziri hapa alizungumza mara kadhaa kwamba kuangalia jinsi gani watu wote waliopitiwa katika bomba la Ziwa Victoria wataweza kupata maji. Kwa hiyo, naomba nikuhakikishie kwa commitment ya Serikali abayo inaiweka kwa wananchi wa Tanzania na hasa wale wanaopitiwa katika bomba kubwa la Ziwa Victoria
ni kwamba Serikali itafanya kila liwezekanalo kuhakikisha ni jinsi gani maji sasa maji yaweze kuwafikia Wananchi wako na wewe mwisho wa siku ni kwamba tuweze kukuona hapa Bungeni kwa heshima kubwa ya Wasukuma wa kule.

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. KEMIREMBE J. LWOTA Aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha miradi ya maji inayojengwa Wilayani Sengerema katika Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa inakamilika haraka na kuwanufaisha wananchi wa Buchosa hasa mradi wa maji wa Lumea - Kalebezo na Nyegonge?

Supplementary Question 4

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante sana, naomba nimuulize bwana Waziri; katika Wilaya ya Kwimba kuna vijiji kumi ambavyo vilipangiwa kupelekewa maji katika mradi wa vijiji kumi, zaidi ya miaka kumi leo,
naomba leo nijue katika hivi vijiji vya Kadashi, Isunga, Shirima na Mhande mkandarasi hayupo site mpaka leo na kwa sababu nilishafanya mawasiliano na Mheshimiwa Waziri wa Maji mwenyewe kwa muda mwingi, nataka leo anipe majibi kazi hii ya miradi hii ya maji katika Wilaya ya Sumve na Kwimba lini itakamilika?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli anachokisema Mheshimiwa Mbunge haongopi na mimi naomba nikiri kwamba nimefika Jimboni kwake kule na miongoni mwa jambo katika taarifa ambayo niliyosomewa ni changamoto ya maji na hali kadhalika suala zima la vijiji kumi katika suala zima la mpango wa World Bank na ni kwa sababu nimesema hapa nyuma kwamba miradi hii ya maji maeneo mengi sana ilisimama na ilisimama kwa sababu hapa nyuma suala zima la kifedha lilikuwa siyo zuri zaidi, lakini
sasa hivi Serikali katika Mfuko wa Maji tumejipanga vizuri kuhakikisha miradi hii inatekelezeka. Lakini jambo lingine utakuta kuna changamoto ya mkandarasi, kwa hiyo kwa sababu taarifa zimeshakuja Serikalini na Waziri wa Maji taarifa hii anayo sasa kwa kina basi nadhani mpango mzuri utafanywa naamini jambo hili
litafanyika vizuri na miradi hii itakamilika na wananchi wa Jimbo lako watapata maji kwa sababu commitment ya Serikali hii kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji.