Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mpango mkakati gani wa kunusuru Taifa na janga la mabadiliko ya tabianchi? (b) Je, ni lini Serikali itahakikisha kwamba Ofisi za Majiji, Manispaa, Miji na Halmashauri zinakuwa na Idara ya Usafi na Mazingira inayojitegemea kuliko kuitegemea Taasisi ya NEMC ambayo inaonekana kuzidiwa na majukumu ya kudhibiti na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi? (c) Je, Serikali ilipata ushauri gani kuiondoa Idara ya Mazingira kutoka kwenye Kamati ya awali ya Mazingira, Ardhi, Maliasili na Utalii na badala yake kupelekwa kwa Viwanda na Mazingira?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa Sheria ya Mazingira namba 20 ya mwaka 2004, Kifungu cha 182 na 183 (1) (2) na (3) na kifungu cha 36(1) na (2) tunatambua uwepo wa Maafisa Usafi na Mazingira katika Halmashauri zetu nyingi na kwa kuwa wahitumu hao wanamaliza elimu yao ya vyuo vikuu kwa vyuo vyetu hapa kwa wingi sana toka mwaka 1987, je, ni lini Serikali sasa itatangaza ajira ya wataalam hao ili kukidhi mahitaji ya mkakati aliyotaja Waziri? Swali la kwanza hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa maeneo mengi ya Nchi yetu mazingira yake yameharibika sana na kupelekea kuwepo ukame mkubwa na kusababisha njaa au uhaba wa chakula na hasa katika Jimbo langu la Bunda na Wilaya nzima ya Bunda. Je, Waziri yuko tayari kuitisha kongamano la kimazingira la kushirikisha Wabunge ili kujua hali halisi ya mazingira katika nchi yetu?

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS-MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na suala la Maafisa Mazingira; kama nilivyozungumza wakati nikijibu swali la msingi kwamba Maafisa Mazingira hawa tayari katika Halmashauri zetu wapo. Aidha, nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge katika zile Halmashauri ambazo hawajaweza kuajiri watu hawa basi pale nafasi zitakapoanza kutolewa, Serikali itakapoanza kuajiri tena waajiriwe hawa wa Serikali zile Halmashauri zote zihakikishe kwamba zina Maafisa Mazingira katika Halmashauri husika kama maelekezo ambavyo yamekwishakutolewa. Lakini vilevile na Wizara zote ambazo hazina sekta hii ya mazingira wahakikishe kwamba wana hao maafisa katika sekta hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili kuhusiana na ukame ambao umepelekea uhaba wa chakula na Mheshimiwa Mbunge kupendekeza kwamba liwepo kongamano. Ninaloweza kusema kwamba wananchi wote na Wabunge wote ni lazima tukubali kwamba sasa tupo katika mabadiliko makubwa na tuko kwenye athari kubwa za mabadiliko ya tabianchi ambapo sasa inatupasa sisi sote kuhusiana na kilimo, kilimo chetu sasa hivi ambacho kimekuwa na mvua ya kusuasua kuhakikisha kwamba wananchi hawa wanaelezwa namna ya kutumia taarifa sahihi za wataalam wetu, tafiti zinazofanywa kulingana na mabadiliko ya tabianchi waweze kujua mbegu bora zinazohitajika kwa sasa hivi ili kupambana na huu uhimilivu wa tatizo la tabianchi, mbegu bora hizo zinazozungumzwa katika mazao hayo, lakini vilevile na mazao ambayo yanahimili ukame huo kulingana na mvua ambazo zinanyesha kwa kiwango cha chini sana sasa. Ipo mikoa iliyokuwa inapata mvua ambazo zinanyesha kwa kiasi kikubwa sana lakini leo hii mvua hizo zimekuwa za kusuasua, kwa hiyo, wananchi lazima wafundishwe hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu makongamano na taarifa mbalimbali za kuwahujisha wananchi; Hizo tutaendelea kuzitoa kwa wananchi ili waweze kuwa na tahadhari na hali hii ya sasa hivi ya mabadiliko ya tabianchi na suala la makongamano hilo litazungumzika kulingana na kwamba tumeshaamua kwamba shughuli yoyote ambayo tutaifanya tuhakikishe tunazidhibiti matumizi ya hovyo ya Serikali na hivyo tutahakikisha kwamba elimu hii tunaifikisha bila gharama kubwa sana.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mpango mkakati gani wa kunusuru Taifa na janga la mabadiliko ya tabianchi? (b) Je, ni lini Serikali itahakikisha kwamba Ofisi za Majiji, Manispaa, Miji na Halmashauri zinakuwa na Idara ya Usafi na Mazingira inayojitegemea kuliko kuitegemea Taasisi ya NEMC ambayo inaonekana kuzidiwa na majukumu ya kudhibiti na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi? (c) Je, Serikali ilipata ushauri gani kuiondoa Idara ya Mazingira kutoka kwenye Kamati ya awali ya Mazingira, Ardhi, Maliasili na Utalii na badala yake kupelekwa kwa Viwanda na Mazingira?

Supplementary Question 2

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna asiyetambua kwamba mabadiliko ya tabianchi ni janga la kitaifa na kimataifa. Kwa kutambua hilo binafsi kama Mbunge wa Jimbo la Ngara kwa kushirikiana na wataalam wangu katika Halmashauri yangu ya Ngara tumejipanga kuanzisha programu ya kuwa na vikosi kazi vya kupambana na moto kama kisababishi kikuu cha uharibifu wa mazingira. Programu hiyo ambayo tutaiita Community Fire Brigade kuanzia kwenye ngazi ya vijiji na kata.
Sasa swali, Serikali kupitia Wizara ya Muungano na Mazingira wako tayari ku-support programu hii kwa kutoa fedha kwa sababu lengo ni kuanzisha vitalu, kupanda miti katika maeneo ambayo yameathirika na moto lakini pia
kuanzisha miradi ambayo ni rafiki wa mazingira kwa maana ufugaji wa nyuki kwa malengo matatu, moja, kulinda mazingira; lakini pili, kuinua kipato cha wananchi na tatu, kutoa ajira.
MWENYEKITI: Naomba swali kwa ufupi Mheshimiwa.
MHE. ALEX R. GASHAZA: Tayari nimeshauliza swali…Serikali ipo tayari…
MWENYEKITI: Basi naomba ukae upate majibu!
MHE. ALEX R. GASHAZA: Haya!

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS-MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa kuanzisha mkakati huo katika Jimbo lake na Wabunge wengine waige mfano wa Wabunge kama mtazamo alionao Mheshimiwa Mbunge nimhakikishie kabisa kwamba ofisi yangu haina tatizo lolote, tunaomba huo mkakati wake atuandikie ili tuweze kuona jinsi ya kuuingiza katika mipango ya Serikali tuweze ku-support mpango huo ili kuweze kuhakikisha kwamba mazingira yanalindwa kwa gharama zote kuhakikisha kwamba mazingira yako salama lakini tunapambana nahii hali ya mabadiliko ya tabianchi ambayo kwa kweli inahitaji wadau mbalimbali wote wa Tanzania wote kwa ujumla kuunga mkono jitihada hizi.

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mpango mkakati gani wa kunusuru Taifa na janga la mabadiliko ya tabianchi? (b) Je, ni lini Serikali itahakikisha kwamba Ofisi za Majiji, Manispaa, Miji na Halmashauri zinakuwa na Idara ya Usafi na Mazingira inayojitegemea kuliko kuitegemea Taasisi ya NEMC ambayo inaonekana kuzidiwa na majukumu ya kudhibiti na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi? (c) Je, Serikali ilipata ushauri gani kuiondoa Idara ya Mazingira kutoka kwenye Kamati ya awali ya Mazingira, Ardhi, Maliasili na Utalii na badala yake kupelekwa kwa Viwanda na Mazingira?

Supplementary Question 3

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, katika majibu yake Mheshimiwa Waziri amesema ili kupambana na suala la mmomonyoko wa ardhi katika kingo za bahari Serikali imechukua au itachukua hatua ya kujenga kuta katika kingo za bahari pamoja na kupanda miti ya mikoko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mmomonyoko wa ardhi katika kingo za bahari sasa hivi unakuwa kwa kiasi cha mita mbili kwa mwaka. Kiasi ambacho ni kikubwa sana. Je, Serikali inauwezo gani wa kujenga kuta katika ukanda wote wa bahari ili kuzuia mmomonyoko huu na hiyo elimu ya upandaji hiyo mikoko inatolewa kwa kiasi gani ambayo tunaweza tukakabiliana na kasi hii ya ukuaji wa mmomonyoko katika ardhi?

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS-MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kweli ipo kasi kubwa ya kuongezeka kwa kina cha bahari kumesababisha bahari kwenda kwenye makazi ya watu, kumesababisha mmomonyoko mkubwa sana wa fukwe zetu, lakini imesababisha pia hasara kubwa kwa sababu kuna baadhi ya majengo ya biashara na makazi yako kwenye hatari kubwa ya kumezwa na bahari na miundombinu mingine ya kiuchumi mikubwa kama visima vya gesi ambavyo na vyenyewe viko kwenye hatari vilevile ya kumezwa na bahari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunachofanya kama Wizara ya Mazingira katika pande mbili zote tunayo Idara ya Mazingira ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano, lakini tuna Idara ya Mazingira pia ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Serikali hizi zote kwa pamoja zinaendelea kufanya kazi ya kufanya tathmini ya kuweza kubaini hizi athari kila mahali sasa baada ya kubaini zile athari ambazo zinasababishwa na haya mabadiliko ya tabianchi tunaangalia kwamba ipi tuipe kipaumbele leo ili kuweza kuzuia athari ambazo zinaweza kujitokeza kwa muda mfupi kama sasa hivi tutakubaliana Wabunge wote kwamba hapa na mlitupitishia kwenye bajeti na sasa hivi kuta hizo zimeshaanza kujengwa, ukuta wa Pangani, ukuta wa Ocean Road, ukuta wa Kilimani na ukuta wa Kisiwa Panza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, visiwa hivi vyote ndivyo vilikuwa vipaumbele vyetu kwasababu maeneo haya yalikuwa yamepata athari kubwa na hivyo sasa naona Mbunge wa Pangani hapa ana hofu ni kwamba mkandarasi yuko site sasa hivi amekwisha ku-report sasa hivi ameanzia na Ocean Road na ndiyo huyo huyo ambaye atajenga ukuta wa Pangani ndiyo huyo huyo atayejenga ukuta wa Kilimani pamoja na Kisiwa Panza na anauwezo wa kutosha kufanya kazi hizo kwa muda tuliompa.