Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. QAMBALO W. QULWI (K.n.y. MHE. CECILIA D. PARESSO) aliuliza:- Wilaya ya Karatu inapakana na Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro ambapo watalii wengi hutembelea hifadhi na kufanya Wilaya hii kupata fursa ya kujengwa hoteli za kitalii, pamoja na hoteli hizo kujengwa ndani ya Halmashauri ya Wilaya, Halmashauri hiyo hainufaiki na uwekezaji huo. (a) Je, Halmashauri hiyo hairuhusiwi kutoza hotel levy? (b) Je, nini mkakati wa Serikali kuitangaza Wilaya hii kutokana na uwekezaji wa hoteli nyingi, nzuri na za kisasa zilizopo katika Wilaya hii?

Supplementary Question 1

MHE. QAMBALO W. QULWI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza. Mheshimiwa Mwenyekiti, ni fursa kubwa kwa Halmashauri hasa kama ile ya Karatu yenye vivutio vingi vya kitalii na hizi hoteli za kitalii hasa katika kipindi hiki ambacho Halmashauri zetu nyingi zinachechemea katika eneo la mapato ya ndani. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, huoni sasa umefika wakati wa kubadilisha sheria hiyo ili kodi hiyo ya hotel levy ikusanywe na Halmashauri zetu ili iweze kuchangia katika eneo lile la mapato ya ndani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika swali la msingi uliulizwa suala la Serikali inamkakati gani, lakini majibu bado yamerudi kwa Halmashauri ya Karatu kujitangaza pamoja na kwamba kuna kipengele kidogo cha Serikali kusaidia. Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri zetu nyingi hazina mapato ya kutosha ya ndani, je, Mheshimiwa Waziri tunachouliza, ni mkakati wa Serikali wa kutangaza hoteli zile za kisasa ili wale wageni badala ya kulala hata Nairobi waje Karatu ili waondokee pale kwenda Ngorongoro na Manyara? Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, nadhani yote ni mchakato huu wote mpana kwa sisi Waheshimiwa Wabunge kama tukiona kuna haja ya kubadilisha sheria basi nadhani katika mawazo ya pamoja tutafanya hilo kwa pamoja kwa lengo la Halmashauri zetu, lakini hilo ni takwa la kisheria, kwa hiyo, ni sisi wenyewe kufanya maamuzi katika hilo na mchakato huo ukianza inawezekana kila mtu kutakuwa na michango mbalimbali kama ya wadau nini kifanyike. Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili la utangazaji, ni kweli nimezungumza kwamba website ya Karatu lakini kuna mipango mbalimbali ya Serikali na mpango mkubwa sasa hivi hata ukipitia shirika letu la ndege katika suala zima ambalo wenzetu wa Maliasili na Utalii mara nyingi sana wameamua katika shirika letu la ndege liwe miongoni mwa mojawapo kutangaza vivutio mbalimbali vya kitalii. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, katika mpango wa kutangaza vitu mbalimbali vya kitalii hapa kama Serikali ina mipango mipana sana kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii na hilo naomba niseme kwa suala la Karatu tutalipa kama special preference kwa ajili eneo lile lina hoteli nyingi zaidi lakini ni eneo la kimkakati mtu akifika pale anapata faraja anakuwa na sehemu nzuri ya kulala, hana mashaka ya aina yoyote. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi naamini Serikali yetu kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii itaongeza upana wake wa utangazaji wa vivutio vyetu vya utalii, lengo kubwa tuweze kukuza uchumi wa nchi yetu kwa sababu tunategemea kwamba kwa fursa tulizonazo za vyanzo vya kitalii tukitangaza vizuri tutakwenda mbele zaidi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge naomba niungane na hoja yako, kama Serikali tutafanya mpango mpana kuhakikisha mambo yanakwenda vizuri katika nchi yetu.

Name

Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. QAMBALO W. QULWI (K.n.y. MHE. CECILIA D. PARESSO) aliuliza:- Wilaya ya Karatu inapakana na Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro ambapo watalii wengi hutembelea hifadhi na kufanya Wilaya hii kupata fursa ya kujengwa hoteli za kitalii, pamoja na hoteli hizo kujengwa ndani ya Halmashauri ya Wilaya, Halmashauri hiyo hainufaiki na uwekezaji huo. (a) Je, Halmashauri hiyo hairuhusiwi kutoza hotel levy? (b) Je, nini mkakati wa Serikali kuitangaza Wilaya hii kutokana na uwekezaji wa hoteli nyingi, nzuri na za kisasa zilizopo katika Wilaya hii?

Supplementary Question 2

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, ninaomba kumuuliza Mheshimiwa Waziri, pengine Waziri wa Maliasili na Utalii au Waziri; katika Wilaya ya Serengeti ndani ya mbuga yetu ya wanyama ya Serengeti kuna mahoteli mengi na makampuni mengi ambayo kisheria wanatakiwa kulipa service levy, lakini kwa muda mrefu walikuwa mahakamani wakikataa na kupinga kulipa ushuru wa service levy. Sasa Serikali imewashinda, tumewashinda yale makampuni lakini mpaka sasa yale makampuni yanagoma kulipa ushuru wa service levy. Je, Wizara ya TAMISEMI na Wizara ya Maliasili na Utalii inaweza kutusaidiaje sisi Halmashauri ya Wilaya ya Serengeti ili waweze kulipa arrears?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli hapo siku za nyuma tumekuwa na hiyo changamoto ya hotels kutofuata utaratibu ambao tulikuwa tumeshauweka na kwa kweli ni kwa mujibu wa sheria kwamba, walipaswa kulipa zile kodi mbalimbali kwa utaratibu ambao Mheshimiwa Mbunge anauzungumzia lakini ni kweli suala hili lilifika mahakamani na hukumu ilitolewa na mahakama sasa kwa bahati mbaya utekelezaji wa hukumu haukuweza kuendelea kwa sababu tulikuwa na changamoto ya kutokuwa na bodi ambayo kwa mujibu wa sheria ndiyo inayopaswa kufanya maamuzi na kuchukua hatua. Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe taarifa kwa ujumla kwamba tayari bodi imekwishaundwa, Mheshimiwa Rais alishateua Mwenyekiti wa Bodi na bodi imekamilika iko tayari na kwamba hivi karibuni suala hilo litapatiwa ufumbuzi na majibu yatapatikana na bila shaka hakuna mashaka tutakwenda kutekeleza ile hukumu kama ilivyotolewa na mahakama.

Name

Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. QAMBALO W. QULWI (K.n.y. MHE. CECILIA D. PARESSO) aliuliza:- Wilaya ya Karatu inapakana na Mamlaka ya Hifadhi Ngorongoro ambapo watalii wengi hutembelea hifadhi na kufanya Wilaya hii kupata fursa ya kujengwa hoteli za kitalii, pamoja na hoteli hizo kujengwa ndani ya Halmashauri ya Wilaya, Halmashauri hiyo hainufaiki na uwekezaji huo. (a) Je, Halmashauri hiyo hairuhusiwi kutoza hotel levy? (b) Je, nini mkakati wa Serikali kuitangaza Wilaya hii kutokana na uwekezaji wa hoteli nyingi, nzuri na za kisasa zilizopo katika Wilaya hii?

Supplementary Question 3

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naungana na Waheshimiwa Wabunge wenzangu waliouliza swali hilo hilo la 0.3 percent service levy. Naomba kuuliza, je, Serikali itakuwa tayari pamoja na hiyo bodi mpya kuundwa, tunashukuru imeundwa kuwanyima leseni hoteli zote za kitalii ambazo zinafanya biashara ndani ya maeneo yetu ya halmashauri zote nchini ambao hawajalipa arrears za nyuma na kila mwaka kabla hawajapatiwa leseni mpya kama ilivyokuwa kwenye kodi nyingine, wasipewe leseni kabla ya kuhakikisha kwamba kodi zote za halmashauri zetu zimelipwa?

Name

Eng. Ramo Matala Makani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu inaendeshwa kwa mujibu wa Sheria na kila jambo ambalo ni kubwa linagusa maslahi ya wananchi, linagusa maslahi ya Taifa ni vizuri tukaliacha likaenda kwa kufuata taratibu za kisheria. Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa kuwa tumesema kwamba madamu bodi imeshaundwa, tunakwenda kupitia hukumu lakini pia kwa kuzingatia Sheria zilizopo tunaenda kuangalia namna ambavyo maslahi ya Taifa yanazingatiwa. Ikiwa kutakuwa kuna mapungufu kwenye Sheria basi tunaweza kulazimika kufanya maerekebisho ya Sheria lakini kama Sheria iko vizuri basi tutatekeleza Sheria jinsi inavyosema ili mradi tu mwisho wa siku maslahi na maslahi ya jamii yaweze kulindwa.