Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Dr. Christine Gabriel Ishengoma
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Tatizo la maji limeendelea kuwa kubwa Morogoro Mjini pamoja na Mji wa Gairo ambapo wanawake wanapata shida sana kutafuta maji:- Je, ni lini tatizo hili la maji litaisha?
Supplementary Question 1
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, licha ya kuongeza ujazo wa mita za maji katika Manispaa ya Morogoro bado kuna sehemu za Lukobe, Kihonda, Kilakala, Folkland, SUA, Mbuyuni na sehemu zingine ambazo hawapati maji. Je, kwa nini hawapati maji wakati wote?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Manispaa ya Morogoro inakua na watu wanaongezeka. Licha ya mradi wa Milenia wa Halmashauri ambao umepita, je, kuna mkakati gani wa kubuni mradi mwingine wa maji kusudi maji yaweze kutosheleza Manispaa ya Morogoro?
Name
Eng. Isack Aloyce Kamwelwe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Katavi
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Sera ya Maji ya mwaka 2002 imeainisha kuhakikisha kwamba nchi yetu ifikapo mwaka 2025 watu wote watakuwa wamepata maji safi na salama. Hiyo itakuwa ni pamoja na wananchi wote wa maeneo ya Morogoro. Maeneo aliyoyataja kwa sasa hivi tunaanza programu ya pili ambayo imeanza Januari, 2016 ya kuendeleza miradi ya maji katika nchi yetu. Katika programu hiyo, tutaendeleza utafutaji wa maji katika Mkoa na Mji wa Morogoro kwa maeneo ambayo yamebaki.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni kweli kabisa kwamba Mkoa wa Morogoro unapanuka na nimwakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba katika mikakati tuliyonayo, tutahakikisha kwamba maeneo yote na wakazi wote wa Mkoa wa Morogoro na Mji wa Morogoro hasa wanapata maji safi na salama. (Makofi)
Name
Devotha Methew Minja
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Tatizo la maji limeendelea kuwa kubwa Morogoro Mjini pamoja na Mji wa Gairo ambapo wanawake wanapata shida sana kutafuta maji:- Je, ni lini tatizo hili la maji litaisha?
Supplementary Question 2
MHE. DEVOTA M. MINJA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii. Pamoja na majibu mazuri aliyotoa Naibu Waziri kuhusu kushughulikia tatizo la maji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi sasa Serikali imekuja na mpango wa kuanzisha Bwawa jipya la Kidunda ambalo litakuwa likitoa huduma ya maji katika mikoa mingine lakini siyo kwa Mkoa wa Morogoro. Serikali haioni kama si vyema kuanzisha bwawa hilo pasipo kwanza kushughulikia kero ya maji ya wananchi hasa wa Manispaa ya Morogoro kuliko kuitumia mito yao kuendelea kutoa huduma katika mabwawa ambayo yatahudumia mikoa mingine nje ya Mkoa wa Morogoro? (Makofi)
Name
Eng. Gerson Hosea Lwenge
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Wanging'ombe
Answer
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, anasema si vyema kuanzisha Bwawa la Kidunda, Serikali iliona ni muhimu sana tuwe na Bwawala Kidunda kwa ajili ya kuhakikisha kwanza wananchi wa Dar es Salaam watapata maji ili muda wote Mto Ruvu uwe unakuwa na maji ya kutosha. Bwawa lile pia tumeshalifanya usanifu siyo kwa ajili ya maji tu lakini pia pamoja na kuzalisha umeme. Kwa hiyo, lina manufaa mengi na hivi sasa tupo mbioni kupata wawekezaji tunaoweza kushirikiana nao tuweze kujenga bwawa lile. Maeneo yale mengine ambayo hayana maji, Naibu Waziri ameshasema vizuri kwamba kwenye programu yetu awamu ya pili tunakwenda kushughulikia tatizo la maji katika maeneo hayo.
Name
Vedastus Mathayo Manyinyi
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Musoma Mjini
Primary Question
MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Tatizo la maji limeendelea kuwa kubwa Morogoro Mjini pamoja na Mji wa Gairo ambapo wanawake wanapata shida sana kutafuta maji:- Je, ni lini tatizo hili la maji litaisha?
Supplementary Question 3
MHE. VEDASTUS M. MANYINYI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza. Pale Musoma Mjini tumekuwa na tatizo la maji kwa muda mrefu na bahati nzuri tumepata mradi ambao tulitegemea toka mwaka jana ungekuwa umekamilika na watu wameanza kupata maji. Je, ni lini sasa Serikali itahakikisha kwamba mradi huo umekamilika kama ilivyokuwa ahadi yake ya toka mwaka jana?
Name
Eng. Isack Aloyce Kamwelwe
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Katavi
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tumeanza kupata fedha, kwa hiyo, wakati wowote ule tutatuma fedha na kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha tutakuwa tumekamilisha mradi huo.
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved