Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rose Cyprian Tweve

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza:- Ni azma ya Serikali ya CCM kumuinua mwanamke kiuchumi na azma hiyo ilipelekea Serikali kuanzisha Benki ya Wanawake. Je, Serikali haioni kuwa sasa ni wakati muafaka kufungua madirisha ya benki hiyo mikoani hasa Mkoa wa Iringa ambapo kuna Community Bank (MUCOB) iliyopo Wilayani Mufindi?

Supplementary Question 1

MHE. ROSE C. TWEVE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Kwako Mheshimiwa Naibu Waziri, pamoja na majibu hayo mazuri pia nikupongeze umekuwa champion mzuri wa vijana, watoto na wanawake na unatambua kuwa wanawake wengi hususani Mkoa wa Iringa wanakiu kubwa ya kujitafutia maendeleo ya kwao pamoja na watoto wao. Na kikwazo kikubwa kimekuwa upatikanaji wa hii mitaji na mikopo yenye riba nafuu. Pamoja na jitihada za Serikali za kufungua hivi vituo viwili pale Mkoa wa Iringa na kama ulivyokiri huu mchakato wa kufungua dirisha pale MUCOB umechukua muda mrefu, sasa ningeomba pia utupe kipaumbele na time frame ni lini sasa pale MUCOB tutegemee kituo hiki ili hawa akinamama waepukane nah ii adha ya kupata mitaji yao? Ahsante sana.

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, namshukuru Mheshimiwa Rose Tweve kwanza kwa kunipa compliment, mara chache sana Wabunge huwa wanawapongeza Serikali wanapofanya vizuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, time frame ni mpaka tutakapopata fedha kwa ajili ya kutunisha mtaji wa benki yetu. Lakini jambo la faraja ni kwamba kwa ahadi niliyoitoa hapa hapa Bungeni kwake yeye mwenyewe na kwa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwamba tuna-cosider kufungua dirisha pale MUCOB bado iko pale pale na ndio maana tumeiingiza kwenye mpango mkakati wetu.

Name

Faida Mohammed Bakar

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ROSE C. TWEVE aliuliza:- Ni azma ya Serikali ya CCM kumuinua mwanamke kiuchumi na azma hiyo ilipelekea Serikali kuanzisha Benki ya Wanawake. Je, Serikali haioni kuwa sasa ni wakati muafaka kufungua madirisha ya benki hiyo mikoani hasa Mkoa wa Iringa ambapo kuna Community Bank (MUCOB) iliyopo Wilayani Mufindi?

Supplementary Question 2

MHE. FAIDA MOHAMMED BAKAR: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.kwa kuwa ni miaka mingi sasa kila tunapoulizia kuhusiana na suala hili la Benki ya Wanawake kuanzishwa Zanzibar, mimi mwenyewe nimeulizia mara nne mpaka leo tawi hili halijafunguliwa kule Zanzibar. Na kuna mara moja niliulizia Mheshimiwa Waziri Ummy alinijibu kwamba ilitakiwa Serikali ya Zanzibar ichangie shilingi milioni 10. Nataka niulize ile shilingi milioni 10 ishalipwa ili hii benki ianzishwe au kama haitolipa hiyo shilingi milioni 10 ndio basi wanawake wa Zanzibar hatutopata benki hii? Mchakato wake ukoje?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante! Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Faida kwa kuuliza swali hili mara nyingi sana. Nina uhakika ndio maana wanawake wa Zanzibar wameendelea kumchagua kuja kuwawakilisha hapa Bungeni kwa sababu amekuwa balozi wao. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, jibu letu ni kwamba shilingi milioni 10 bado haijapatikana lakini azma yetu ya kufungua tawi Zanzibar iko pale pale na Mheshimiwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan amejitolea kutupa eneo kwa ajili kufungulia tawi hilo la benki yetu pale Zanzibar; tutaendelea kufuatilia kwa ukaribu. Na nitakapofanya ziara kwa ajili ya kufuatilia tumekwama wapi kwa ajili ya tawi hili la Zanzibar nitamshirikisha Mheshimiwa Faida.