Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daimu Iddi Mpakate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kusini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Katika Hospitali ya Wilaya ya Tunduru kulikuwa na Chuo cha MCH kilichokuwa kikitoa mafunzo ya taaluma mbalimbali za afya kwa vijana wengi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru lakini mwaka 1980 chuo hicho kiliungua moto:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukikarabati chuo hicho ili kiweze kuendelea kutoa wataalam wa afya kama hapo awali?

Supplementary Question 1

MHE. DAIMU I. MPAKATE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa chuo kile hakikukidhi haja ya kukikarabati na kwa kuwa katika majibu ya msingi yamesema kwamba eneo la chuo lilikuwa dogo. Je, Serikali haioni haja ya kujenga chuo kipya kwa sababu Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ina maeneo mengi ambayo yangeweza kujengwa chuo hicho? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru ina upungufu mkubwa sana wa wafanyakazi katika Idara ya Afya kwa zaidi ya 70%. Ni kwa nini sasa Serikali isitoe upendeleo maalum kwa ajili ya Wilaya ya Tunduru na kwa vijana wa Tunduru ili waweze kuhudhuria mafunzo hayo katika vyuo ambavyo vimefufuliwa?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inayo haja ya kujenga vyuo vipya kwa ajili ya kutoa mafunzo ya watumishi kwenye sekta ya afya, si tu kwa Tunduru lakini ni kwa nchi nzima. Bahati mbaya sana Mpango wa MCH Aider Training ulipoanzishwa mwaka 1973 ulilenga kuzalisha wataalam wa kutoa huduma za uzazi kwa akinamama vijijini kwenye zahanati ambazo zilikuwa zinaanzishwa kwenye mpango ule kutokana na Azimio la Alma-Ata miaka hiyo na Azimio la Afya kwa Wote enzi za miaka ya 70.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango ule umebadilika na hatuwezi kujenga tena chuo kwenye kila mkoa kwa sababu mpango wa kujenga Vyuo vya MCH Serikali iliazimia kujenga chuo kwenye kila mkoa ili kuwazalisha hawa MCH Aider kwa kuwapa kozi ya mwaka mmoja na nusu kwa haraka ili tuwapate kwa wingi zaidi waweze kuwahi kwenda kuokoa maisha ya akinamama wajawazito na watoto. Mpango ule haupo tena na kwa maana hiyo vyuo vya afya sasa hivi haviwezi kuwa ni vyuo vya afya kwa kila mkoa bali vinakuwa ni vyuo vya afya vya kitaifa na utaratibu sasa hivi tunashirikisha pia sekta binafsi ambao nao wanaanzisha vyuo kwa ajili ya kutoa mafunzo ya taaluma mbalimbali za kwenye sekta ya afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili ni kwamba Tunduru wapate watumishi kwenye sekta ya afya, hili ni katika mipango ya Serikali ambayo ni endelevu. Kadri ambavyo tutapewa vibali vya kuajiri watumishi kwenye sekta hii ndivyo ambavyo tutaendelea kuajiri watumishi wapya na kuwatawanya si Tunduru peke yake bali ni kwenye wilaya zote hapa nchini.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Katika Hospitali ya Wilaya ya Tunduru kulikuwa na Chuo cha MCH kilichokuwa kikitoa mafunzo ya taaluma mbalimbali za afya kwa vijana wengi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru lakini mwaka 1980 chuo hicho kiliungua moto:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukikarabati chuo hicho ili kiweze kuendelea kutoa wataalam wa afya kama hapo awali?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Mbali na changamoto ambayo inakikabili Chuo cha Maendeleo ya Jamii - Kisangwa kuhusiana na kutopata fedha za uendeshaji, karakana na kadhalika lakini chuo hicho pia hakina gari. Hivi tunavyozungumza aliyekuwa Mkuu wa Chuo alijiuzia VX kwa Sh. 600,000/= na kufanya Mkuu wa Chuo wa sasa hivi asiwe na gari na kusababisha shughuli za chuo zisiende. Je, Serikali iko tayari kushughulikia ufisadi huu kwa sababu hakuna VX inayouzwa Sh. 600,000/= na kupeleka gari ili chuo hicho kiendeshe shughuli zake vizuri?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa swali kutoka kwa rafiki yangu Mheshimiwa Ester Amos Bulaya kuhusu kile anachopenda kukiita ufisadi. Majibu ya Serikali ni kwamba kwenye kuuza mali za umma ambazo zimemaliza muda wake na ama zimekuwa classified kama ni dilapidated ama mali zilizochoka unajulikana na umeandikwa. Kwa hivyo, kama Mheshimiwa Mbunge ana ushahidi kwamba utaratibu huu ambao umeandikwa kwenye sheria mbalimbali za kuuza mali za Serikali zilizochakaa haukufuatwa, naomba anikabidhi nyaraka alizonazo ili niweze kufuatilia na kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria za nchi yetu.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. DAIMU I. MPAKATE aliuliza:- Katika Hospitali ya Wilaya ya Tunduru kulikuwa na Chuo cha MCH kilichokuwa kikitoa mafunzo ya taaluma mbalimbali za afya kwa vijana wengi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru lakini mwaka 1980 chuo hicho kiliungua moto:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukikarabati chuo hicho ili kiweze kuendelea kutoa wataalam wa afya kama hapo awali?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa sasa wanafunzi wa vyuo vikuu wamekuwa wengi ukizingatia Chuo hiki cha Maendeleo ya Jamii Tengeru kimeanza kujaa. Je, Serikali ina mpango gani wa kupandisha vyuo vidogo vya diploma kama vile vya Monduli CDTI ili kuwa university kuweza kuwa-accommodate vijana waweze kusoma kwa wingi maana elimu inayotolewa na vyuo hivi ni nzuri sana kwa ajili ya Taifa letu?

Name

Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Serikali haina utaratibu wa kuendelea kuvipandisha vyuo vya taaluma za kati kuwa vyuo vya kutoa degree kwa sababu Serikali ya Awamu ya Tano haiamini kwamba inahitaji watu wengi zaidi wenye degree kwenye soko la ajira, hapana! Serikali ya Awamu ya Tano inahitaji watu wengi zaidi wenye ujuzi kwa ajili ya ku-support uchumi wa viwanda na maendeleo ya kilimo na maendeleo ya biashara na ujasiriamali vijijini. Kwa hivyo, tutaendelea kuvijengea uwezo vyuo vyetu vya CDTI nchi nzima ili viendelee kutoa kozi kwenye ngazi hii ya wanataaluma na watu wenye ujuzi wa kati ili ku-support uchumi wa viwanda ambao tunaujenga kwa sasa.