Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA Aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Handeni inahudumia wagonjwa kutoka Kilindi, Mziha, Wegero na Handeni yenyewe. Je, ni lini Serikali itaipatia vifaa tiba na wauguzi wa kutosha hospitali hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Spika, ahsante.
Kwa kuwa Serikali imeshatoa kibali cha kupeleka wauguzi kule na ukizingatia kwamba hospitali ina upungufu wa wauguzi zaidi ya asilimia 60. Je, ni lini Serikali itakuwa tayari kupeleka hao wahudumu ukizingatia kwamba hali ya kule siyo nzuri kwa sasa? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema wenzetu wa Handeni waliomba kibali. Naomba niseme kwamba ni vibali katika kada mbalimbali zimeombwa, lakini naomba niwahakikishie wazi kwamba, kwa sababu mchakato wa utoaji wa vibali ulishaanza katika sekta ya elimu hasa katika suala zima la walimu wa sayansi, kwa kadri Serikali itakavyoona inafaa tutajitahidi kuhakikisha tunapeleka nguvu na hasa vile vibali ambavyo vimebainishwa.
Ofisi ya Utumishi ikishatoa go ahead katika maeneo mbalimbali, tutashiriki kuona ni jinsi gani tutafanya kuongeza watumishi, tukijua kwamba siyo sekta ya afya peke yake isipokuwa kada mbalimbali zina matatizo makubwa sana na hivyo ni jukumu la Serikali kuhakikisha kwamba tunafanya kila iwezekanavyo ili wananchi waweze kupata huduma inayostahiki. Kwa hiyo, Mheshimiwa Omari naomba ondoa hofu katika hilo.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. OMARI A. KIGODA Aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Handeni inahudumia wagonjwa kutoka Kilindi, Mziha, Wegero na Handeni yenyewe. Je, ni lini Serikali itaipatia vifaa tiba na wauguzi wa kutosha hospitali hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, changamoto katika sekta ya afya ukiacha vifaa tiba, sasa hivi pameibuka changamoto kubwa mpya, ambao wananchi wanakuwa wakilipa bima zao za afya, wanakwenda katika hospitali, wanaandikiwa tu dawa lakini wanashindwa kupatiwa pale. Kwa hiyo, nilitaka nijue ipi ni kauli ya Serikali kwa wananchi ambao wamelipia bima zao lakini hawapati matibabu katika hospitali husika?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

shimiwa Spika, ningependa kujibu swali la Mheshimiwa Silinde kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, mwananchi yeyote ambaye ana kadi ya Bima ya Afya anatakiwa kupata huduma zote za afya bure ikiwemo vipimo. Nikiri kwamba katika baadhi ya vituo vya afya vya umma, hasa nadhani unazungumzia CHF tuna changamoto ya upatikanaji wa dawa zote katika vituo vyetu, ndiyo maana Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya una maduka ya dawa ambapo kama umeiokosa ile dawa katika hospitali husika unatakiwa kwenda katika duka la dawa ambalo limetambuliwa na NHIF.
Mheshimiwa Spika, kwa CHF kidogo hapo niseme kuna changamoto. Kwenye mikoa ambapo tumeenda kwenye Bima ya Afya iliyoboreshwa wao wanaweza wakapata dawa katika maduka ya dawa, kwa hiyo tunaifanyia kazi changamoto hii.