Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamadi Salim Maalim

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kojani

Primary Question

MHE. HAMADI SALIM MAALIM aliuliza:- Je, ni kwa nini Askari wa Jeshi la Polisi hucheleweshwa maslahi yanayoendana na vyeo vyao pindi wanapomaliza mafunzo kwa ngazi mbalimbali kama vile Koplo, Sajent, Staff Sajenti, Meja na vingine?

Supplementary Question 1

MHE. HAMADI SALIM MAALIM: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri lakini pia naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa Wizara imekubali kwamba kumekuwa na ucheleweshaji wa mishahara kwa askari hawa wanaopandishwa vyeo, ni kwa nini basi askari hawa wacheleweshwe mishahara yao wakati kila bajeti inapopitishwa tayari nyongeza ya mishahara inakuwa tayari imeshaingizwa katika bajeti ile? swali namba moja.
Pamoja na kwamba Wizara pia imekubali kucheleweshwa kwa mishahara kwa askari hawa, kwa nini basi wanaporekebishiwa mishahara yao washindwe kulipa zile arreas za ile miezi ya nyuma au miaka ya nyuma ambayo imepita kabla ya kurekebishiwa mishahara yao?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mbunge kwa kufuatilia na kuwasemea vizuri vijana wazalendo hawa wanaojitolea kwa ajili ya Taifa letu. Mwenyewe nimezunguka katika mikoa mbalimbali na nimepata fursa ya kuwasikiliza. Matatizo ya aina hiyo si hilo tu, lakini kama Wizara tunaandaa utaratibu wa kila mkoa kuwa na watu wanaofuatilia masuala ya askari ili askari yeye kazi yake iwe ni kulitumikia Taifa na kuondokana na ucheleweshwaji wa marekebisho haya ambayo kimsingi yanatokana na taarifa kamili zinazokusanywa zinazohusu mabadiliko hayo kuchelewa kupatikana na kufikia Utumishi ambao wanahusika kwa ujumla wake kutambua nani anatakiwa alipwe kiasi gani.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunapanga si hilo tu la mishahara pamoja na stahili zingine zingine ambazo wanazipata zikiwemo wanapokwenda kufanya kazi nje ya kituo chake, anapokwenda kwenye operation maalum, anapopata haki yake anayo stahili, kuwa na malalamiko mengine hata ya posho anayostahili ambayo inatakiwa kimsingi iendane kwa asilimia ya mshahara wake, mshahara unapopanda posho ile inabaki constant licha ya kwamba ilitakiwa iwe kwenye uwiano wa asilimia.

Name

Upendo Furaha Peneza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMADI SALIM MAALIM aliuliza:- Je, ni kwa nini Askari wa Jeshi la Polisi hucheleweshwa maslahi yanayoendana na vyeo vyao pindi wanapomaliza mafunzo kwa ngazi mbalimbali kama vile Koplo, Sajent, Staff Sajenti, Meja na vingine?

Supplementary Question 2

MHE. UPENDO F. PENEZA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi hii. Pamoja na Serikali kufanya jitihada za kuwapa maslahi watu wa Jeshi la Polisi, lakini askari hawa wamekuwa wakitumia nafasi zao vibaya kwa masuala binafsi, kwa kuwaonea wananchi. Serikali ina mkakati gani sasa wa kutoa elimu kwa wananchi ili kutambua ofisi hizo za malalamiko ili askari hawa waweze kuchukuliwa hatua kwa kuwa wananchi wa Mkoa wa Geita, vijana wa boda boda na watu wengine wamekuwa wakionewa na Polisi kwa masuala binafsi?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, moja, Taasisi ya Jeshi la Polisi ina utaratibu wake mahususi wa kuchukua hatua kwa kila askari anapokuwa amefanya makosa na wanafanya hatua hizo hata licha ya kuwa pamekuwepo na mlalamikaji, kwa sababu suala la nidhamu kwenye Jeshi la Polisi ni jambo la kipaumbele hata bila kulalamikiwa, ndiyo maana utaona Askari wetu wana nidhamu kubwa sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, inapotokea matatizo ya aina hiyo, Jeshi la Polisi linachukua hatua. Hata hivyo, niseme tu kwa Waheshimiwa Wabunge na kwa Watanzania kwa ujumla, tunapodai haki ni vyema sana tukatambua kwamba tuna wajibu wa kutimiza na hivyo itaondoa taratibu za kuwepo malalamiko ya mara kwa mara. Kwa sababu katika maeneo mengine unaweza ukamnyooshea kidole askari, lakini ukifuatilia undani wake unakuja kutambua kwamba pana mtu ambaye hakutimiza wajibu wake vizuri ndiyo maana Askari akachukua hatua. (Makofi)

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Primary Question

MHE. HAMADI SALIM MAALIM aliuliza:- Je, ni kwa nini Askari wa Jeshi la Polisi hucheleweshwa maslahi yanayoendana na vyeo vyao pindi wanapomaliza mafunzo kwa ngazi mbalimbali kama vile Koplo, Sajent, Staff Sajenti, Meja na vingine?

Supplementary Question 3

MHE. MUSSA R. SIMA: Mheshimiwa Naibu Spika nashukuru sana kwa kuniona, naomba kuuliza swali dogo la nyongeza. Askari wetu wanafanya kazi kwenye mazingira magumu sana na wanafanaya kazi kwa muda mrefu bila kupanda vyeo mpaka kustaafu. Je, Serikali haioni haja sasa ya kutathmini upya vigezo vya kuwapandisha vyeo ili kuongeza ufanisi wa kazi?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana kwa kutumia weledi wake kama mtumishi wa umma na kutambua umuhimu wa motisha inayoambatana na upandaji wa vyeo kwa askari kama ilivyo kwa Mtumishi mwingine ili kuweza kuongeza ufanisi. Wazo lake ni zuri, tumelipokea na Mheshimiwa Rais alishaongelea kuhusu kuongeza motisha kwa watumishi wa umma wote hapa nchini mara baada ya kuwa ameshamaliza marekebisho na kutoa dira ya Serikali yake. Sisi wasaidizi wake tunatembea kwenye miguu yake, tunatembea kwenye maneno yake.
Mheshimiwa Naibu Spika, nimwahidi Mheshimiwa Mussa Sima taratibu hizo zitakapoanza kufanyika tutatoa kipaumbele kwa vijana wetu wazalendo wanaolitumikia Taifa kwa uzalendo na kwa moyo wao kwa ajili ya kuhakikisha raia wa Tanzania na mali zao wako salama.