Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mattar Ali Salum

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Shaurimoyo

Primary Question

MHE. MATTAR ALI SALUM aliuliza:- Je, ni lini Serikali itamalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Mkokotoni kilichoko Unguja?

Supplementary Question 1

MHE. MATTAR ALI SALUM: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kunipa nafasi hii ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa tunafahamu majengo haya yanazidi kuwa magofu na baadaye gharama, fedha za Serikali zinapotea kwa wingi kwa sababu haya baadaye yanabomoka tu, vilevile watu wanafugia ng‟ombe. Je, Mheshimiwa Waziri, ni lini Wizara itampatia Mkandarasi huyu amalize kituo hiki? Je, Wizara itachukua jitihada gani kuhakikisha kituo hiki kinamalizwa mapema? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kituo hiki ambacho kimeanza kujengwa mwaka 2011 kimechukua muda mrefu kukamilika. Hata hivyo, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Mkokotoni, Mheshimiwa Juma Hija ambaye naye amekuwa akifuatilia kwa karibu ujenzi wa kituo hiki. Nilichomwambia ambacho naendelea kukizungumza hapa mbele ya Bunge lako Tukufu ni kwamba, ni kweli tumempatia tayari Mkandarasi karibu shilingi milioni 50 ili kuweza kukamilisha hiki kituo, lakini bado kuna deni ambalo anahitajika alipwe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumefikiria kwamba, katika bajeti ya mwaka 2016/2017, tuweze kushughulikia madeni ya Wakandarasi mbalimbali ambao wamekuwa wakifanya kazi za vituo katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu ikiwemo Mkandarasi ambaye anajenga Kituo hiki cha Mkokotoni.