Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. RASHID ALI ABDALLAH aliuliza:- Nchi inakuwa na amani pale ambapo kuna ulinzi imara. Je, ni utaratibu upi mzuri wa kuimarisha ulinzi Bungeni?

Supplementary Question 1

MHE. RASHID ALI ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Kanuni ya 145(a) na (b), yeyote ambaye anaingia katika maeneo ya Bunge au ukumbini ni lazima akaguliwe. Kwa utaratibu huo huo, magari ya Mawaziri na ya Wabunge wakati mwingine hukaguliwa kwa kutumia mbwa. Unapotumia mbwa kukagua magari wakati mwingine hudondosha mate na yale mate ni najisi tunaita muhalladha na najisi ile haiondoki mpaka uoshe mara saba na mara moja uhakikishe unatia mchanga. Je, hakuna utaratibu mwingine mzuri wa ku-check magari haya hasa kwa wale waislamu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika Bunge lililopita tulishuhudia Mbunge mwenzetu akivamiwa katika maeneo anayoishi na kuharibiwa gari lake. Je, Bunge lina utaratibu gani kuhakikisha kwamba Wabunge hawa wanapata ulinzi au usalama wao unalindwaje kwenye maeneo yao wakiwa katika Bunge hili?

Name

Charles Muhangwa Kitwanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Rashid Abdallah kwa observation yake ya msingi kabisa ambayo ni ya kiimani. Kwa kuwa ameuliza hakuna utaratibu mwingine na sisi kama Serikali pamoja na Bunge tuseme tumepokea ushauri ili tuli-digest jambo hilo huku tukiangalia maslahi mapana kwani imani inatuhusu na ulinzi unatuhusu. Kwa hiyo, ni jambo ambalo sote tutaliangalia tufikie muafaka mzuri. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, hili la pili kuhusu Mbunge kuvamiwa, taarifa zake tunazo na tunachofanya ni kuimarisha ulinzi katika mazingira ya Wabunge wetu ili kuhakikisha kwamba wako katika maeneo salama. Niwahakikishie tu Wabunge kwamba wako mikono salama na kwa kuwa mnafanya kazi vizuri na sisi tunahakikisha kwamba wanakuwa salama. Niwatangazie tu Watanzania kwamba Wabunge hawa wanachapa kazi na jana wamechapa kazi mpaka saa sita usiku, wameunganisha kikao hiki. Kwa hiyo, wanapokutana nao huko uraiani watambue kwamba Wabunge hawa ni wachapakazi. Niwaambie vijana wangu kwamba hata wanapokuwa barabarani hawa Wabunge wakiona wako speed wawaambieni tu tunawahitaji lakini watambue ni kutokana na uchapakazi wao wanawahi mikutano.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RASHID ALI ABDALLAH aliuliza:- Nchi inakuwa na amani pale ambapo kuna ulinzi imara. Je, ni utaratibu upi mzuri wa kuimarisha ulinzi Bungeni?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa katika suala zima la ulinzi tunategemea sana askari wetu, lakini tumekuwa tukishuhudia askari wetu wakipoteza maisha wakiwa kazini wakati mwingine kwa kupambana na majambazi au wakipata ajali kwenye misafara mbalimbali. Nataka kufahamu Serikali ina utaratibu gani wa kuhudumia familia za askari hawa wanaopoteza maisha wakiwa kazini kama kusomesha watoto na huduma na huduma nyingine muhimu?

Name

Charles Muhangwa Kitwanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze sana Mheshimiwa Catherine kwa kulileta jambo hilo. Ni kweli kumekuwepo na matatizo hayo na sisi kama Wizara niliwaelekeza wataalam wangu kuangalia maeneo ambayo yanahusu sheria na yale yanayohusu sehemu ya bima kwa ajili ya askari wetu ili kuweza kusaidia askari kwanza akiwa bado yuko kazini, pale anapopata ajali kazini kuweza kuhudumiwa katika maumivu anayoyapata. Nilipozunguka nilipata taarifa kwamba kuna askari wanaumia kazini wanaambiwa bima haiingii kwenye baadhi ya vipimo ama katika baadhi ya dawa wanazotaka.
Kwa hiyo, hili la kuzihudumia familia wanapokuwa wamepata ajali tunaliangalia kwa mapana kisheria ili familia hizo zisiyumbe baada ya kuwa askari wetu amepata ajali.

Name

Savelina Slivanus Mwijage

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RASHID ALI ABDALLAH aliuliza:- Nchi inakuwa na amani pale ambapo kuna ulinzi imara. Je, ni utaratibu upi mzuri wa kuimarisha ulinzi Bungeni?

Supplementary Question 3

MHE. SAVELINA S. MWIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kabla sijauliza swali langu, naomba kuwashukuru wale wote ambao wanatoa misaada kwa Wilaya yangu ya Bukoba Mjini na naomba Watanzania wote na wasio Watanzania waangalie kwa jicho la huruma Bukoba Mjini. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa naomba kumuuuliza Mheshimiwa Waziri, kwa kuwa Wizara yake inalinda raia na mali zao, hivi sasa Wilaya ya Bukoba Mjini watu wote wanalala nje na matatizo wanayoyapata ni kuibiwa mali zao na askari wanakwenda na kukamata wale watu ambao wanawasaidia wale wahanga. Je, Wizara yake imejipangaje kwenda kukabiliana na janga hili Bukuba Mjini kwa kuwalinda raia?

Name

Charles Muhangwa Kitwanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Mheshimiwa Mbunge wa jambo alilolileta ambalo liko muda huu. Niseme tu tangu tukio limetokea Wizara ya Mambo ya Ndani kwa kushirikiana na Kamati za Ulinzi na Usalama Mkoa na Wilaya wameimarisha ulinzi katika maeneo husika. Kwa kuwa watu ni wengi inatokea katika kutafuta namna ya kujiridhisha kujua yupi anayeenda kwa ajili ya kutoa huduma na yupi anayeenda kwa ajili ya kukwapua ama kuchukua vile ambavyo vimezagaazagaa, kwa hiyo, ndiyo maana utaona kuna mwingiliano wa aina hiyo, lakini nia ya Wizara pamoja na Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya ni kuhakikisha kwamba watu hawa ambao wamepata matatizo wao pamoja na mali zao wanakuwa katika hali ya usalama.