Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI (K.n.y. MHE. KASUKU S. BILAGO) aliuliza:- (a) Je, Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 itaanza kutekelezwa lini katika kipengele cha Elimu ya Msingi (Chekechea - Kidato cha Nne)? (b) Je, ni Walimu wangapi wa Sekondari wanahitajika ili kutekeleza Sera hiyo? (c) Je, hali ya miundombinu katika shule zetu ikoje katika kutekeleza Sera hiyo.

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri naomba sasa kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, je, ni lini sasa Serikali itaanza kutekeleza kwa vitendo, Waraka namba tatu (3) wa mwaka 2014 unaoelekeza kwamba kutakuwa na posho ya madaraka kwa ajili ya Walimu Wakuu wa shule za Msingi, Walimu wa Sekondari, Waratibu wa Elimu wa Kata na Wakuu wa Vyuo? Sasa utekelezaji wake utaanza lini maana ni mwaka wa pili sasa unakwenda?
Mheshiminiwa Naibu Spika, swali la pili la nyongeza; kwa kuwa umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari hapa nchini maarufu kwa jina la TAHOSSA ulikuwa ukitumia sehemu za michango, kwa ajili ya kufanya shughuli mbalimbali ikiwemo pamoja na kufanyisha mitihani ya mock na ujirani mwema ambao ililenga sana kuimarisha na kuboresha taaluma. Sasa, kwa kuwa tunaenda na mpango wa elimu bila malipo, je, Serikali iko tayari kuisaidia ruzuku TAHOSSA ili iendelee kufanya kazi zake kwa ufanisi?

Name

Prof. Joyce Lazaro Ndalichako

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kuhusu suala la utekelezaji wa waraka namba tatu wa posho ya madaraka. Hili ni swali jipya halina uhusiano na swali la msingi kwa hiyo majibu yake yataandaliwa na kuletwa katika kipindi kingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na swali la pili la TAHOSSA ambalo linaendana na utekelezaji wa Sera ya Elimu Msingi ya Mwaka 2014, ni kwamba katika mwongozo waraka namba sita umebainisha wazi mgawanyo wa fedha na hivyo basi kama kuna mahitaji yanayohusiana na mitihani, fedha zinazotolewa kwa ajili ya elimu bure kuna kipengele cha mitihani. Kwa hiyo, napenda kuchukua nafasi hii kusisitiza kwamba matumizi ya fedha zinazotolewa kwa ajili ya elimu msingi yazingatie mwongozo uliotolewa.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI (K.n.y. MHE. KASUKU S. BILAGO) aliuliza:- (a) Je, Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 itaanza kutekelezwa lini katika kipengele cha Elimu ya Msingi (Chekechea - Kidato cha Nne)? (b) Je, ni Walimu wangapi wa Sekondari wanahitajika ili kutekeleza Sera hiyo? (c) Je, hali ya miundombinu katika shule zetu ikoje katika kutekeleza Sera hiyo.

Supplementary Question 2

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Nataka kujua elimu shirikishi kuhusiana na wanafunzi wenye uhitaji maalum, kwa sababu shule yetu ya Lugalo iliyopo katika Mkoa wa Iringa ina wanafunzi ambao wana uhitaji maalum, lakini utakuta hawa wanafunzi hawana vifaa vya kujifunzia wala Walimu hawana vifaa vya kuwafundishia. Je, Serikali inasemaje kuhusiana na hilo?

Name

Prof. Joyce Lazaro Ndalichako

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na elimu shirikishi na changamoto za elimu maalum, nadhani nimeeleza wazi dhamira ya Serikali ya kutatua changamoto zilizopo katika utoaji wa elimu kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama Mheshimiwa Ritta Kabati pengine anaona mikakati ambayo tumeiweka kwenye bajeti haitaweza kuondoa changamoto mahususi, ambazo ziko kwenye shule katika eneo lake, nimhakikishie kwamba, niko tayari kuongozana naye ili nione matatizo halisi ili tuweze kuyatatua, kwa sababu hiyo ndiyo dhamira ya Serikali.

Name

Joram Ismael Hongoli

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI (K.n.y. MHE. KASUKU S. BILAGO) aliuliza:- (a) Je, Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 itaanza kutekelezwa lini katika kipengele cha Elimu ya Msingi (Chekechea - Kidato cha Nne)? (b) Je, ni Walimu wangapi wa Sekondari wanahitajika ili kutekeleza Sera hiyo? (c) Je, hali ya miundombinu katika shule zetu ikoje katika kutekeleza Sera hiyo.

Supplementary Question 3

MHE. JORAM I. HONGOLI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa wanafunzi hawa wa awali pia ni elimu ambayo ni msingi na sehemu nyingi wamekuwa wakifundishwa na Walimu waliosomea kufundisha wanafunzi wa shule za msingi na kuna baadhi ya maeneo wamekuwa wakifundishwa na Walimu ambao hawajapata mafunzo. Sasa kwa kuwa tuna chuo ambacho kinatoa Walimu, au tuna vyuo ambavyo vinatoa Walimu wa shule za awali, ni kwa nini Serikali isiajiri Walimu wa shule za awali katika shule zote nchini ili waweze kufundisha vizuri kwa sababu hawa wana mafunzo maalum kwa ajili ya wanafunzi wa elimu ya awali?

Name

Prof. Joyce Lazaro Ndalichako

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Answer

WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba Walimu wa elimu ya awali wanahitaji kuwa na mafunzo maalum, lakini napenda kulihakikishia Bunge lako Tukufu kwamba, Walimu wote wanaofundisha shule za msingi wanakuwa na course ya lazima ambayo inahusiana na ufundishaji wa elimu ya awali. Kwa hiyo, kwa sasa hivi ambapo wale walimu ambao wamefanya kama course maalum (specialization) hawapo wa kutosha, bado Walimu wa shule za msingi wana uwezo wa kufundisha kwa sababu ni somo la lazima kila Mwalimu wa shule ya msingi lazima achukue somo la elimu ya awali.
Mheshimiwa Naibu Spika, pia napenda kumfahamisha Mbunge pamoja na Bunge lako Tukufu kwamba, sasa hivi tayari Serikali imepanua wigo wa utoaji wa mafunzo ya elimu ya awali kwa Walimu na sasa hivi tuna vyuo tisa ambavyo vinatoa mafunzo na Walimu hawa watahitimu mwaka 2018, ndipo watakamilisha masomo yao.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI (K.n.y. MHE. KASUKU S. BILAGO) aliuliza:- (a) Je, Sera ya Elimu na Mafunzo ya Mwaka 2014 itaanza kutekelezwa lini katika kipengele cha Elimu ya Msingi (Chekechea - Kidato cha Nne)? (b) Je, ni Walimu wangapi wa Sekondari wanahitajika ili kutekeleza Sera hiyo? (c) Je, hali ya miundombinu katika shule zetu ikoje katika kutekeleza Sera hiyo.

Supplementary Question 4

MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Nataka kujua, kwa kuwa sekondari nyingi sasa zina maabara na baadhi ya sekondari hizo kata zake zimekwishapitiwa na umeme, lakini Sekondari hazina umeme ni jukumu la Wizara au ni nani mwenye jukumu la kuingiza umeme kwenye shule hizo? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge juu ya mchakato wa shule hizi za sekondari ambazo zina maabara. Ni kwamba katika mchakato wa utengenezaji wa bajeti za Halmashauri, Halmashauri inatakiwa itenge bajeti ya kutosha kwa ajili ya uwekaji wa umeme katika shule hizo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hata hivyo Waziri wa Nishati na Madini wiki iliyopita alizungumza wazi kwamba tutaweka kipaumbele kwa kupitia Wizara ya Nishati na Madini, kuhakikisha kwamba Halmashauri zinafanya hivyo. Pia Wizara ya Nishati na Madini itaweka kipaumbele ili shule hizi zote ziwe na umeme katika nchi yetu.