Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza:- Upanuzi wa hospitali ya Mkoa ya Pwani ijulikanayo kama Hospitali ya Tumbi umesimama kwa takribani miaka mitatu, sasa nondo na zege la msingi na nguzo zinaoza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo ili kuondoa hasara na kuleta tija katika huduma ya afya Kibaha?

Supplementary Question 1

MHE. SILVESTRY F. KOKA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali na kwa niaba ya wananchi wa Kibaha nishukuru kwa kutupatia hiyo 1.4 bilioni katika upanuzi wa hospitali hii, nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, hospitali ya Tumbi inapokea takribani asilimia nane hadi 10 ya majeruhi wote Tanzania. Licha ya miundombinu hafifu katika chumba cha kupokelea majeruhi hospitali hii imekuwa ikijitahidi kupokea majeruhi na kuwatibia na kwa mujibu wa taratibu majeruhi hutibiwa bila kutozwa chochote na hatimaye Serikali inapaswa kurejesha fedha hizi kwa hospitali ikiwa pamoja na Hospitali ya Tumbi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa takribani miaka mitano fedha hizi hazijarejeshwa katika hospitali hii, jambo ambalo limepelekea huduma kuwa hafifu na za kubabaisha. Je, Serikali sasa itarejesha lini fedha hizi ikiwa ni pamoja na special package kulingana na idadi kubwa ya majeruhi yanayokwenda katika hospitali hii?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kituo cha afya mkoani ambacho kinahudumia takribani wakazi 150,000 wa Mji wa Kibaha kina miundombinu hafifu, wagonjwa wanalala chini jambo ambalo linapelekea hata wagonjwa wengine kupewa rufaa pasipostahili kwa ajili ya kukosa miundombinu ya kutolea huduma.
Je, Serikali sasa ina mpango gani wa kupandisha hadhi kituo hiki ikiwa ni pamoja na kukipatia miundombinu na vifaa tiba ili kiweze kukabili na kuwahudumia wananchi wa kibaha ambao ni mji unaokua kwa kazi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli maswali yake Mheshimiwa Koka ni maswali ya msingi. Hospitali ya Kibaha ni hospitali ambayo iko pembeni mwa Barabara Kuu ya Morogoro, na karibuni katika kipindi kirefu sana tumeshuhudia ajali nyingi zikijitokeza katika maeneo haya. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge unalolizungumza ni jambo la kweli kabisa. Katika swali lako la kwanza Serikali tutafanya analysis ili kuisaidia hospitali hii iweze kufanya vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu suala la special package ya kusaidia hospitali hii, nadhani Serikali nayo itafanya kwa kina ili jambo hili liweze kwenda vizuri ili Hospitali hii ya Tumbi iweze kutoa huduma kwa wananchi kama inavyokusudiwa. Naamini si wananchi wa Mkoa wa Pwani au wa Kibaha peke yake, hapana, ni wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao wengi wao wakipata ajali hospitali hiyo ndiyo limekuwa kimbilio la karibu zaidi kabla mtu mgonjwa hajafikishwa katika Hospitali ya Muhimbili.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu swali lake la pili, juu ya kituo cha afya cha mkoani; ni kweli na mimi niliweza kufika kituo kile mwaka jana mwanzoni. Sasa hivi mgonjwa yeyote hataruhusiwa kwenda Hospitali ya Tumbi mara baada ya Hospitali hii kupandishwa. Kila mgonjwa wa Kibaha Vijijini lazima atibiwe katika kituo hiki ndipo apewe referral na yule wa Kibaha Mjini atibiwe kituoni pale ndipo apewe referral; lakini kituo kile cha afya kina changamoto kubwa sana. Bahati nzuri watu kutoka Wizara ya Afya walikuja pale kufanya analysis kuangalia ni jinsi gani kinaweza kupandishwa hadhi kuwa hospitali ya Wilaya.
Mheshimiwa Naibu Spika, bahati mbaya pale awali ilionekana ina upungufu mkubwa, ikiwepo wodi ya wazazi, lakini Mbunge nikushukuru sana kwa juhudi kubwa uliyofanya na wananchi wako na viongozi wako, wodi ya wazazi sasa hivi pale imejengwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo ni kwamba katika bajeti ya mwaka huu wa fedha, licha ya kujengwa ile wodi ya wazazi, lakini mmetenga karibu 700,000,000. Katika milioni 700 karibu milioni mia mbili arobaini na, ni kwa ajili ya ukarabati, mtajenga theatre ambapo kabla hospitali hii haijapandishwa kuwa hospitali ya Wilaya lazima kuwe na theatre room na bajeti ya mwaka huu pia mmetenga bajeti hiyo, lakini mmetenga bajeti ya kununua standby generator.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naomba niseme kwamba katika bajeti ya mwaka huu naamini kwamba tutasukuma kwa kadri iwezekanavyo ili pesa hizi ziweze kupatikana ili miundombinu ile ikamilike ili Kituo cha Afya cha Mkoani kiwe na hadhi ya Hospitali ya Wilaya ili wananchi wa Kibaha waweze kupata huduma bora katika maeneo haya. Ahsante sana.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza:- Upanuzi wa hospitali ya Mkoa ya Pwani ijulikanayo kama Hospitali ya Tumbi umesimama kwa takribani miaka mitatu, sasa nondo na zege la msingi na nguzo zinaoza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo ili kuondoa hasara na kuleta tija katika huduma ya afya Kibaha?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Hospitali ya Tumbi ni hospitali ambayo ilikuwepo tangu enzi za Nordic countries, wakati huo ikiwa chini ya Nordic countries kama chini ya shirika. Ilikuwa inatoa huduma nzuri sana, lakini mpaka sasa hivi huduma yao imefifia, je, Serikali ina mpango gani wa kufuatilia huduma za Hospitali ya Tumbi ambayo inatolewa kwa wananchi?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza tukumbuke kwamba, Mheshimiwa Mbunge alikuwa Mkuu wa Mkoa ule wa Pwani kipindi hicho na naamini kwamba anaijua vizuri hospitali hiyo ndiyo maana swali lake limekuwa la msingi sana juu ya kuiboresha hospitali hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kwamba mwanzo ilikuwa inatoa huduma nzuri zaidi, lakini tukikumbuka zamani population ya watu waliokuwa wakitibiwa katika hospitali hiyo ni tofauti na hivi sasa. Hivi sasa takriban wagonjwa kati ya 300 mpaka 500 wanafika pale kila siku na wengine wanaolazwa. Kwa hiyo, idadi ya watu wanaotibiwa kwa sasa hivi ni kubwa zaidi kuliko hapo mwanzo na ndio maana sasa hivi Serikali imehakikisha inashirikiana na wadau mbalimbali.
Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kumshukuru Mbunge wa Kibaha Mjini na Serikali kwa ujumla, katika harakati zilizofanyika angalau sasa hivi kuna mashirika mbalimbali kama wenzetu kutoka Korea na taasisi zingine wametusaidia vifaa mbalimbali kwa lengo la kuboresha hospitali ile.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la awali ni kwamba, mwaka huu tumetenga shilingi bilioni 1.4, lakini tutaendelea kuhakikisha tunafanya kila liwezekanalo hadhi ya Hospitali ya Tumbi iweze kuwa nzuri zaidi kwa sababu sio Wanapwani wanaotibiwa pale peke yake isipokuwa wananchi wote ambao wanapita katika ukanda wa barabara hiyo, wakipata matatizo hospitali ya Rufaa ya Tumbi ni Hospitali ya karibu ambayo ni kimbilio la wananchi wengi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge, naomba nikuahidi kwamba Serikali inalitazama kwa macho ya karibu zaidi jambo hilo na ndiyo maana Waziri wetu wa Afya, Naibu Waziri, walikwenda pale na Waziri wangu wa nchi alifika pale katika kutembelea Shirika la Elimu Kibaha kuangalia changamoto za pale. Katika mwaka huu wa fedha tutapambana kwa kadri iwezekanavyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika bajeti ya mwaka uliopita ilitengwa milioni 700 haikuweza kupatikana, tutapambana mwaka huu ili bajeti iweze kupatikana ili hadhi ya Hospitali ya Tumbi iwe kama vile ilivyokuwa pale awali.

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza:- Upanuzi wa hospitali ya Mkoa ya Pwani ijulikanayo kama Hospitali ya Tumbi umesimama kwa takribani miaka mitatu, sasa nondo na zege la msingi na nguzo zinaoza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha ujenzi wa hospitali hiyo ili kuondoa hasara na kuleta tija katika huduma ya afya Kibaha?

Supplementary Question 3

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri naomba kuuliza swali dogo. Kwa kuwa sasa kuna wimbi kubwa la ujenzi wa vituo vya afya katika ngazi za kata, kwa mfano, Wilaya yetu ya Mbulu ina tarafa tano, ni kwa nini Serikali isifanye utaratibu wa kupitia tarafa zote hizo tano na kuona ni kituo gani cha afya chenye mahitaji madogo ya fedha ili iweze kutoa huduma kwa kutengewa fedha za kutosha? Kwa mfano tarafa zote zina vituo vingi lakini hakuna kituo kinachotoa huduma stahiki? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ushauri wa Mheshimiwa Mbunge tumeupokea kwanza na ndiyo maana wiki iliyopita kamati ya Bunge ya Bajeti, Wizara ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI pamoja na Wizara ya Afya tulikuwa tuna kikao cha pamoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, kikao kile kililenga kubaini kwanza maboma yaliyokuwepo yote kabla hayajakamilishwa. Najua Mheshimiwa Mbunge una-concern kubwa ya maboma katika maeneo yako. Tumefanya tathmini ya maboma yote yaliyojengwa, lakini hayajakamilika, pia tathmini ya zahanati na tathmini ya vituo vya afya vina hali gani. Lengo letu ni kuwa na kituo cha afya ambacho mtu hata huduma za operation ziweze kufanyika vizuri katika maeneo husika. Kwa hiyo, jambo hilo sasa tumelifanya kwa pamoja na Kamati ya Bunge imeelekeza. Lengo kubwa ni kupata fedha za kuboresha huduma ya afya katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo ni kwamba kinachotakiwa kufanyika ni wataalam wetu na Wabunge wetu kutushauri, kwamba ikiwezekana tu-review ramani za majengo yetu. Wakati mwingine inaonekana kujenga kituo cha afya gharama yake inakuwa kubwa kumbe inawezekana kwamba, isiwe friendly kwa mazingira husika. Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge ni kwamba, Serikali tunalifanyia kazi na kwamba tutateua baadhi ya vituo, tuviweke katika hadhi nzuri ili viweze kutoa huduma bora na viwe kimbilio ya wananchi katika maeneo yao.