Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA (K.n.y. MHE. MENDRAD L. KIGOLA) aliuliza:- Mradi wa maji katika Kata ya Mtwango umechukua muda mrefu bila kukamilika na wananchi wanaendelea kupata shida ya maji:- Je, ni lini mradi huo utakamilika na kukabidhiwa kwa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa, Kata ya Litapunga, Halmashauri ya Nsimbo, vijiji vingi havina maji. Je, ni lini Serikali itapeleka miradi Kata ya Itapunga, ili akinamama wale waweze kupata unafuu wa maisha?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo la Nsimbo maana yake Jimbo liko pana najua na vijiji viko vingi. Na Katika bajeti zetu za TAMISEMI tulielezea baadhi ya miradi ya maji, lakini na wenzetu wa Wizara ya Maji wameelezea mipango yao katika ujenzi wa maji. Na ni kwamba tulikuwa na programu ya maji ya awamu ya kwanza sasa tunaingia katika programu ya maji ya awamu ya pili.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika program ya maji ya awamu ya kwanza kuna maeneo mengine maji tulikosa, visima vilichimbwa, lakini maji hayakupatikana! Katika programu ya Awamu ya II tunaenda mbali zaidi, maana yake maeneo ambayo yalikosa maji yaweze kupata maji. Maeneo yaliyokuwa hayana maji maana yake hawana miradi ile ya maji ni lazima kujielekeza kuweka miradi ya maji.
Mheshimiwa Naibu Spika, na lengo kubwa ni nini? Tulichokipanga katika kipindi hiki lengo kubwa tulikuwa na ile, principal yetu ni kwamba, lazima tumuondoe mama ndoo kichwani. Nikijua kwamba Nsimbo ina changamoto kubwa sana kama ilivyokuwa Korogwe, Kisarawe, Bahi na kama ilivyokuwa maeneo mengine yote, jukumu letu kubwa ni kwamba, sisi tutafanya analysis jinsi gani tutafanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, maeneo uliyoyazungumza tutaangalia kwa pamoja kwamba kuna miradi gani ambayo imetengwa kwa sasa hivi, lakini ni jijsi gani tutafanya tuyafikie maeneo ya watu mbalimbali kwa sababu lengo letu kubwa ni kumuondoa mama ndoo kichwani, kutumia fursa mbalimbali, kama visima vilikuwa vinachimbwa, na vilikuwa vimepatikana basi tunaangalia alternative way, kama kutumia malambo au kutumia chanzo kingine cha karibu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nikuahidi Mheshimiwa Mbunge na bahati nzuri mnafanya ushirikiano mzuri wewe na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo pale na yeye tulikuwa na kikao mpaka hata kesho tulipanga kuweza kuonanan katika mambo mengine ya ukusanyaji wa mapato. Lakini hayo ni miongoni mwa mambo mengine ambayo tutaenda kuyaangalia; lengo kubwa ni kwamba kuwapatia wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania maji kwa hiyo, tumelichukua swali lako kwenda kulifanyia kazi.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA (K.n.y. MHE. MENDRAD L. KIGOLA) aliuliza:- Mradi wa maji katika Kata ya Mtwango umechukua muda mrefu bila kukamilika na wananchi wanaendelea kupata shida ya maji:- Je, ni lini mradi huo utakamilika na kukabidhiwa kwa wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi, ili niweze kuuliza swali moja la nyongeza pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.
Kwa kuwa Naibu Waziri umeshatembelea Wilaya ya Mpwapwa na Wilaya ya Mpwapwa kuna vijiji ambavyo vina matatizo makubwa sana ya maji; kwa mfano Kijiji cha Tibwetangula, Lupeta, Bumila, Makutupa, Nana, Chimai, Salaza, Iyoma, Ngalamilo, Chamanga na Majami.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri utatembelea maeneo hayo, ili uone shida ya maji wanayopata wananchi wa Jimbo la Mpwapwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimshukuru Mbunge huyu, tulifanya ziara ya pamoja pale katika sekondari yetu ya Mpwapwa tukabaini wanafunzi wanashindwa hata kufanya mitihani vizuri kwa sababu, maji hawapati. Reason behind kuna connection ya maji ya shilingi milioni nne tu! Tumeshirikiananae kwa pamoja, juzi hapa nimekwenda, sasa vijana wa sekondari ya Mpwapwa wanapata maji. Kwa hiyo, Mheshimiwa Lubeleje nakushukuru kwa uongozi wako mzuri, mradi ule umekamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sambamba na hilo kweli, ukiangalia katika jimbo lake lile, ni pana! Jimbo lile sasa hivi na Jimbo la Kibwakwe lote linafanya Halmashauri ya Mpwapwa. Na nilipotembelea nikuhakikishie Mheshimiwa Lubeleje, nilifika mpaka katika Kijiji cha Makutupa, pale hata ukitokea msiba pale kupata maji maana yake wananchi wanaenda kuyapata maji mbali zaidi. Lakini Jimbo lako Mheshimiwa Lubeleje ni kwamba ukiliangalia jiografia yake lina tatizo kubwa sana, lakini hata nikapita maeneo mengine ya Chamkoroma kule watu msitu wamekata wote, maana yake hata vyanzo vya maji vya mtiririko maana yake vimepotea. Sasa nini tutafanya? Ulichoniomba nitembelee kule, lakini nakwambia nimeshatembelea in advance mpaka maeneo ya kambi kule ndani nikavuka na ule mto! Tutaendelea kufanya hivyo tena, lengo kubwa ni kubaini hizo changamoto kwa pamoja, tujadili kwa pamoja, tuondoe matatizo ya wananchi wetu.

Name

Godfrey William Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA (K.n.y. MHE. MENDRAD L. KIGOLA) aliuliza:- Mradi wa maji katika Kata ya Mtwango umechukua muda mrefu bila kukamilika na wananchi wanaendelea kupata shida ya maji:- Je, ni lini mradi huo utakamilika na kukabidhiwa kwa wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. GODFREY W. MGIMWA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Tatizo ambalo lipo katika Jimbo la Mheshimiwa Mendrad Lutengano, ni sawasawa na tatizo ambalo liko katika Jimbo langu la Kalenga. Ningeomba kujua Miradi ya Maji ya Weru, Itengulinyi, Supilo, itakamilika lini kwa sababu wakandarasi wamekuwa wakipiga makelele na kudai pesa zao za malipo?
Ningependa kujua kutoka kwa Mheshimiwa Waziri, ni lini sasa Wakandarasi hawa watalipwa, ili kwamba, miradi iweze kuendelea na wananchi wangu waweze kupata maji? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna miradi ya maji mingi sana ilisimama. Wakandarasi wali-demobilize mitambo kutoka maeneo ya miradi na sababu kubwa ilifanya kwamba, flow ya fedha, wakandarasi walifanya kazi walikuwa hawajalipwa, certificates zilienda Wizarani, lakini watu walikuwa hawajalipwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, jukumu letu kubwa tulilofanya ni kuhakikisha pesa zinakusanywa kama nilivyosema awali. Hivi sasa nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge wakandarasi wote karibuni sasa hivi kila Halmashauri pesa sasa zimeshapelekwa, ilimradi wakandarasi waweze kurudi site.
Mheshimiwa Naibu Spika, juzi nilikuwa na Naibu Waziri wa Maji hapa tukifanya mjadala katika hayo, imeonekana sasa hivi hali imeenda vizuri zaidi. Kama tutafanya analysis kama huko Makete kama watu hawajaanza kurudi site, lakini ni kwamba kweli wakandarasi walitoa mitambo mwanzo, lakini fedha sasa hivi baada ya makusanyo mazuri tumeshapeleka site huko ilimradi wakandarasi walipwe, kazi iweze kuendelea. Tutaangalia kama huku katika Jimbo lako kama kuna matatizo kidogo bado yapo, tutaangalia jinsi gani tutafanya kuyatatua kwa pamoja.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini sambamba na hili niweze kuzungumzia hata pale kwa ndugu yangu wa Mufindi pale, ndugu yangu Mheshimiwa Chumi, kulikuwa na suala la pampu pale, tumefanya harakati, hivi sasa ile pampu inafungwa baada ya kupata uhakiki wa kutosha. Lengo letu ni kwamba, miradi yote ikamilike na wananchi waweze kupata maji.

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri – TAMISEMI, kuhusu Jimbo la Kalenga tayari nimeshaongea na Mheshimiwa Mbunge na tumeangalia vitabu, tumeshapeleka shilingi milioni 365. Nikawa nimemuomba Mheshimiwa amfahamishe Mkurugenzi kwamba, kama kuna certificate zozote walizonazo mezani watuletee, ili tuweze kukamilisha malipo Wakandarasi waendelee na kazi.