Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI aliuliza:- Je, lini Serikali itakarabati au kujenga Mahakama mpya ya Wilaya ya Ukerewe?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Kwanza niipongeze Serikali kupitia Wizara kwa kutupatia pesa za kujenga Mahakama ya Mwanzo Ilangara, ujenzi unaendelea, lakini kwa mpango vilevile wa kutupatia pesa kwa ajili ya kujenga Mahakama kwa mwaka huu, nina swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, kiwanja kilichopatikana kiko mbali na maeneo wanayoishi wananchi na kuna eneo ambalo linatumika sasa linalomilikiwa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya na yuko tayari kulitoa kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama. Wizara iko tayari kujadiliana na kukaa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ili eneo hili lenye ukubwa wa mira za mraba zaidi ya 3,300 liweze kutumika kwa ajili ya ujenzi wa Mahakama hiyo? Nashukuru.

Name

Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, niseme tu kwamba, eneo ambalo tunakwenda kujenga hii Mahakama ya Ukerewe lipo Airport, Kata ya Mkirizya, na tayari tathmini imeshafanyika na wananchi wamekwishafidiwa kwa ajili ya ujenzi. Sasa suala analolisema Mheshimiwa kwamba, kuna kiwanja kingine tuone namna gani ya ku-shift na huku tumeshalipa fidia kwa wananchi tayari kwa ujenzi, inaweza ikawa ni changamoto.

Mheshimiwa Spika, hata hivyo, naomba nilichukue tulifanyie kazi kama tunaweza ku-shift, maana kule wananchi wameshafidiwa tayari kwa kujenga, sasa ku-shift mahali pengine inawezekana kukawa na masuala ya gharama na kadhalika, ikawa changamoto, lakini hata hivyo naomba nilichukue.