Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Je, lini Serikali italeta Bungeni sheria mahsusi kwa ajili ya kuwalinda wananchi dhidi ya ukatili wa kijinsia?

Supplementary Question 1

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, nina swali moja tu la nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, kwa vile makosa haya ya ukatili wa kijinsia sasa yanaendana na makosa ya kuporomoka kwa maadili.

Je, Serikali haioni haja ya kuboresha sheria hii iliyopo sasa ili kuchanganya tiba ya makosa haya yanayotokana na kuporomoka kwa maadili? (Makofi)

Name

Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba nijibu swali la nyongeza kuwa Serikali inaona haja ya kuboresha sheria hizi, hivi sasa tupo katika mchakato wa kupitia taarifa maalum ya masuala ya maadili.

Mheshimiwa Spika, utakumbuka katika Bunge hili tulizungumza sana kuhusu masuala ya maadili, masuala ya mahusiano ya jinsia moja. Nimeshaunda timu maalum pale Wizarani na wanaandaa taarifa kuona namna gani sheria hizi tuendelee kuziboresha. Kwa hiyo, haja ya kuboresha ipo na ndiyo jukumu la msingi la Bunge. Kazi ya Bunge ni kutunga sheria, kazi ya Bunge ni kurekebisha sheria, kwa hiyo, suala la kuangalia kama ipo haja au haipo kwa kweli, nichukue nafasi hii kusema tu kwamba, hilo ndilo jukumu la msingi kabisa la Wizara yangu na tunaendelea kuangalia namna gani tuendelee kuziboresha sheria zetu.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE K.n.y. MHE. EMMANUEL A. MWAKASAKA aliuliza:- Je, lini Serikali italeta Bungeni sheria mahsusi kwa ajili ya kuwalinda wananchi dhidi ya ukatili wa kijinsia?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Karagwe imeathirika sana na ukatili wa kubakwa watoto kuanzia miaka mitatu mpaka nane, wakati huu ambapo sheria haijatungwa, hatua zipi za haraka zitachukuliwa ili kunusuru kizazi hiki?

Name

Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, si kwamba sheria haijatungwa, ni kwamba sheria tunazo mbalimbali za masuala ya ukatili, lakini swali la msingi lilitaka sheria zote hizi za masuala ya ukatili wa kijinsia ziwe kwenye sheria hii moja. Sheria ya Mtoto inaelezea masuala ya ukatili kwa mtoto, Sheria ya Ndoa inaelezea ukatili ndani ya masuala ya ndoa. Pia tunayo Sheria ya Kanuni ya Adhabu, huko nyuma tulikuwa na Sheria ya Masuala ya Kujamiiana na yale yote makosa ya kujamiiana (Sexual Offence Act.) tukaingiza kwenye Penal Code. Kwa hiyo, niseme tu kwamba, sheria tunazo na kifungu 131 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu kinaelezea vizuri kabisa masuala ya ukatili.

Mheshimiwa Spika, ninampongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwamba, yako maeneo kuna ukatili wa watoto. Nichukue nafasi hii kusema tu kwamba, maeneo yote ambako kuna ukatili wa watoto kwanza tunaomba taarifa zifike katika vituo vyetu vya Polisi na vituo vyote vya haki jinai. Tunayo sheria hata ya kumlinda mtoa taarifa, tunaita Whistleblowers Act. Kwa hiyo, Sheria hii ya Penal Code hivi sasa ipo na kwa kweli, inakidhi haja pale ambapo mtoto amefanyiwa ukatili tena chini ya miaka kumi, sheria inaeleza wazi kabisa ni kifungo cha maisha.

Mheshimiwa Spika, hoja ilikuwa ni kuzichanganya sheria zote ziwepo kwenye sheria hii moja. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa na kumpongeza kwamba, kujali watoto ni suala la msingi sana, lakini pia sheria zilizopo kwa kweli kwa sasa zinakidhi haja ya makosa haya ya ukatili wa kijinsia. (Makofi)