Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema Gerald Mwandabila

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:- Je, Serikali ina Mkakati gani wa kufanya utafiti maalum katika Mji wa Tunduma ili kubaini ni namna gani unaweza kuchangia kukuza uchumi wa nchi?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA G. MWANDABILA: Mheshimiwa Spika, kulingana na majibu ambayo yametolewa na Waziri, nataka kufahamu, ni upi mkakati maalum na wa haraka wa Serikali kuuingiza Mkoa wa Songwe kiujumla wake katika mpango wa uwekezaji wa kimkakati?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, nataka kufahamu: Je, Serikali imeshafanya vitu gani katika kuongeza biashara na uwekezaji katika Mkoa wa Songwe katika maeneo yafuatayo: eneo la madini, dhahabu na makaa ya mawe, kilimo cha mpunga, uvunaji wa chumvi na mazao mengine ya kibiashara yanayoendelea katika Mkoa wa Songwe? Ahsante.

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, maswali ya nyongeza yanahusu fursa za uwekezaji katika Mkoa wa Songwe na ametaja maeneo specific; madini, chumvi na kadhalika.
Mheshimiwa Spika, ninahitaji kumwandalia taarifa hizi kwa kina ili nisije nikatoa majibu ambayo ni ya kurukaruka. Kwa hiyo, naomba tupate nafasi kwa sababu kwa kweli ni swali ambalo ni jipya kidogo, ahsante.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Primary Question

MHE. NEEMA G. MWANDABILA aliuliza:- Je, Serikali ina Mkakati gani wa kufanya utafiti maalum katika Mji wa Tunduma ili kubaini ni namna gani unaweza kuchangia kukuza uchumi wa nchi?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa nami niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Manispaa ya Ilemela katika kuunga mkono uwekezaji ilitenga eneo la ekari 52 katika eneo la Nyamungoro, eneo lenye miundombinu yote; maji, barabara na liko kwenye main road ya kwenda Musoma kwa ajili ya kuweka industrial park na tayari andiko lilishafika katika Ofisi za Serikali; ni lini mradi huu utatekelezwa ili tuongeze ajira na kukuza TEHAMA kwa watu wa Mwanza na ukizingatia ni ukanda wa maziwa makuu ni hub katika eneo hilo? (Makofi)

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MIPANGO NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, maendeleo ya Industrial Park tunafanya pamoja na Wizara ya Viwanda, ipo chini ya EPZA. Nalifahamu hili eneo na nilishafika na tayari lipo katika Taasisi yetu ya EPZA wakilifanyia kazi, linaenda kwenye bodi na baada ya hapo tutalitolea maelekezo maalum kwamba ni lini hasa ratiba itatoka ya utekelezaji. Naamini katika mpango na bajeti ambao tutawasilisha kwenye Mkutano ujao, tutaeleza mpango maalum kuhusu Industrial Park ya Manispaa ambayo Mheshimiwa Angeline Mabula ameieleza.