Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa muda mfupi na mrefu wa kukarabati Mradi wa Maji wa Makonde Mkoani Mtwara?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza. kazi aliyopewa sasa hivi Mkandarasi ambaye anafanya ukarabati mkubwa ni kupeleka maji katika matenki makubwa na hakuna fedha za distribution.

Je, Serikali ina mpango gani wa dharura kutenga fedha nyingi kwa ajili ya usambazaji wa maji kwenye vijiji husika na mradi huo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili ni kutaka kujua maendeleo ya mradi wa kutoa maji Mto Ruvuma na kupeleka Mtwara Manispaa ambao utanufaisha Wilaya ya Mtwara na Halmashauri ya Mji wa Nanyamba.

Je, mradi huu utaanza kutekelezwa lini? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Chikota kama ifuatavyio: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, distribution, katika miradi yote ambayo fedha zinaanzisha miradi ya kutengeneza vyanzo, distribution huwa zinafanywa na mamlaka zetu. Hivyo Mheshimiwa Mbunge mpango wa Wizara ni kuhakikisha mara baada ya kukamilika eneo la kwanza la utekelezaji, namna ya kufanya distribution ndiyo kazi ambayo itafuata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali la pili, maendeleo ya matumizi ya Mto Ruvuma kupeleka maji Mtwara, hiki ni kipaumbele cha Wizara. Mto Ruvuma ni Mto ambao tunautegemea sana kama chanzo cha uhakika hivyo na chenyewe pia kitaendelea kutumika kadri fedha tunavyopata kwenye Wizara, tutahakikisha tunatekeleza Mradi huu wa Maji wa Mto Ruvuma.