Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eric James Shigongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buchosa

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: - Je, lini Serikali itawamegea eneo Wananchi wa Visiwa vya Maisome katika Hifadhi ya Kisiwa cha Maisome?

Supplementary Question 1

MHE. ERIC J. SHIGONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nimemwelewa vizuri sana Mheshimiwa Naibu Waziri, ni kwamba Serikali imekubali kutoa hekta 2943.8 kwa wananchi wa Kisiwa cha Maisome. Kwa niaba ya wananchi hao naomba niwasilishe furaha yao kwa Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa Bunge lako Tukufu kwani kwa muda mrefu wameishi kwa mateso sana wakiwa hawana eneo la malisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa swali langu ni moja tu ni lini? Ni lini? Ni lini, kwa mara tatu mchakato huu wa kuweka mpaka utatekelezwa ili wananchi waifurahie Serikali yao? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa sheria, zoezi hili linapaswa kuchukua miezi sita. Siku 90 za kuweka mipaka, kutengeneza ramani na vilevile siku 90 ambayo ndiyo itahusisha lile tangazo nililolisema. Tumefika hatua nzuri, naomba Mheshimiwa Mbunge atupe muda, tunalikamilisha muda siyo mrefu.

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. ERIC J. SHIGONGO aliuliza: - Je, lini Serikali itawamegea eneo Wananchi wa Visiwa vya Maisome katika Hifadhi ya Kisiwa cha Maisome?

Supplementary Question 2

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Ni Septemba niliuliza swali Na. 76 juu ya wananchi ambao wamevamia Msitu wa Bono uliopo Kijiji cha Mswaki kwenye Kata ya Msanja na Serikali ilisema itawaondoa itakapofika Desemba 30, kwa maana ya mwaka 2022. Nataka kujua: Ni nani ambaye anazuia kuondoa wananchi wale ambao wanafanya uharibifu mkubwa na msitu huo tunaoutegemea kwa ajili ya mvua? Ahsante.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, bado Serikali inasimamia maazimio yake yale kwamba wananchi wale wataondolewa kwenye msitu ule. Naomba Mheshimiwa Mbunge, atupe fursa tulifanyie kazi ili tutekeleze kusudio letu.