Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JULIANA D. SHONZA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka Kitengo cha Watoto Njiti katika Hospitali ya Wilaya ya Mbozi?

Supplementary Question 1

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kuwa Hospitali yetu ya Wilaya ya Mbozi ni chakavu sana kama ambavyo Mheshimiwa Waziri alivyosema na hizi fedha ambazo zimetengwa kwa kweli ni kidogo. Sasa nataka nifahamu kwamba Serikali ina mpango gani au mkakati gani wa kudumu kuhakikisha kwamba majengo yote ya Hospitali ya Wilaya ya Mbozi yanakarabatiwa? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama alivyosema Mheshimiwa Juliana Daniel Shonza kwamba Hospitali ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi ni hospitali kongwe ni hospitali chakavu. Ndiyo maana kwa utashi na mapenzi mema ya Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ameainisha hospitali hiyo miongoni mwa hospitali 19 nchini kote za kipaumbele kwa ajili ya kutenga fedha kuhakikisha majengo yanakarabatiwa na kuwa na hadhi ya hospitali ya halmashauri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana Mheshimiwa Rais tayari ameshatenga shilingi milioni 900 katika bajeti ya mwaka huu na itapelekwa kwa ajili ya ukarabati. Tutaendelea kutenga fedha kwa awamu kuhakikisha majengo yote ya Hospitali ya Halmashauri ya Mbozi inakarabatiwa na kutoa huduma nzuri kwa wananchi wa Mbozi, ahsante.