Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza: - Je, ni lini Halmashauri ya Mji Mdogo wa Tukuyu itapewa mamlaka kamili baada ya kukamilisha taratibu na kukidhi vigezo?

Supplementary Question 1

MHE. ANTON A. MWANTONA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nifanye marekebisho kidogo, siyo Halmashauri ya Mji wa Tukuyu ni Mji wa Tukuyu, kwa mujibu wa taratibu na sheria nataka nijue majukumu hasa miji midogo ni nini? Wale watumishi wa miji midogo wanatakiwa wafanye majukumu gani hasa katika ukusanyaji wa mapato ya ndani pamoja na matumizi yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niiombe Serikali kama ingeweza ikaandaa mwongozo ambao utasaidia hii miji midogo kuweza kujitegemea na kukua ili hatimaye baadae wawe na uwezo kuwahudumia wananchi katika maeneo yao ya kiutawala hasa katika ukusanyaji wa mapato na matumizi na kuyasimamia matumizi hayo, ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Anton Albert Mwantona, Mbunge wa Jimbo la Rungwe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mamlaka za miji midogo zilianzishwa kwa mujibu wa sheria na zina majukumu yake na zina Baraza la Madiwani wa Mamlaka ya Mji Mdogo. Pia zina mtendaji wa mamlaka lakini pia zina mwenyekiti wa mamlaka ya mji mdogo. Kazi zao pamoja na majukumu mengine ni pamoja na kuhakikisha kwamba zinakusanya mapato katika eneo lao la utawala katika mitaa yao. Pia kuwasilisha mapato hayo katika account ya halmashauri mama ambapo mkurugenzi wa halmashauri ndiye accounting officer wa halmashauri hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kusimamia miradi ya maendeleo ambayo inatekelezwa katika mitaa ambayo inaunda mamlaka ya mji mdogo, Mamlaka ya Mji Mdogo ni hatua ya kwanza ya kuelekea kupata kibali au kupandishwa hadhi kuwa Halmashauri ya Mji. Kwa hiyo, hii ni hatua ya mwanzo wakati wanajenga uwezo wao kujiendesha kuelekea kwenye Halmashauri ya Mji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swala la pili; kuhusu mwongozo wa miji hii kujitegemea, kwa sababu hii ni hatua ya kukua kuelekea kwenye Halmashauri ya Mji maana yake ukishafika hatua ya Halmashauri ya Mji wanakuwa na mkurugenzi ambaye ndiye accounting officer na inakuwa ni Baraza la Madiwani la halmashauri ya mji mambalo lina majukumu yote kwa mujibu wa sheria za Serikali za Mitaa, ahsante.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza: - Je, ni lini Halmashauri ya Mji Mdogo wa Tukuyu itapewa mamlaka kamili baada ya kukamilisha taratibu na kukidhi vigezo?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana natambua kwamba kijiji ni mamlaka ya utawala, kata ni mamlaka ya utawala na halmashauri ya mji au ya wilaya au jiji ni mamlaka ya utawala. Nafahamu msimamo wa Serikali kuhusu uendeshwaji wa mamlaka za kiutawala. Sasa swali langu, jimbo siyo mamlaka ya utawala, Jimbo langu la Sikonge ili nifike kwenye tarafa ile ya mradi natembea kilometre 200, ili nifike kwenye Kata ya mbali kabisa mpakani mwa Singida natembea kilometre 400. Sasa swali langu ni kwamba kwa nini Serikali hairuhusu uanzishwaji wa majimbo mapya ili uwakilishi wa wananchi uwe mzuri zaidi hapa Bungeni?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Kakunda Mbunge wa Jimbo la Sikonge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli na ni sahihi kama Mheshimiwa Mbunge alivyosema kuhusiana na mamlaka za utawala katika ngazi za vijiji, kata, halmashauri na maeneo mengine. Pili, jimbo ni eneo ambalo linauwakilishi wa wananchi na yeye ndiyo Mbunge wa jimbo hilo. Namshauri kwa sababu taratibu za kuomba majimbo mapya zinafahamika nimuombe tu Mheshimiwa Mbunge afuate taratibu zile na kufikisha mahala ambapo kuna mamlaka hiyo hiyo ili waweze kuona uwezekano wa kuchukua hatua hizo kwa mujibu wa mahitaji ya jimbo lake, ahsante.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. ANTON A. MWANTONA aliuliza: - Je, ni lini Halmashauri ya Mji Mdogo wa Tukuyu itapewa mamlaka kamili baada ya kukamilisha taratibu na kukidhi vigezo?

Supplementary Question 3

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mamlaka ya Mji Mdogo wa Mikumi ina zaidi ya umri wa miaka 20 na mchakato wa kuomba halmashauri ulishapita katika ngazi ya wilaya, mokoa na TAMISEMI na kwa kuwa Jimbo la Mikumi au Tarafa ya Mikumi siyo halmashauri wala siyo makao makuu ya wilaya imepitwa na fursa zote za miradi ya kimkakati. Je, nini mpango wa Serikali katika kukumbuka miji hii ambayo haina hadhi ya wilaya au halmashauri katika miradi mikubwa ya kimkakati kama TACTICs na miradi mingine?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dennis Londo Mbunge wa Jimbo la Mikumi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, uanzishwaji wa mamlaka za miji midogo ikiwemo Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mikumi ulianzishwa kwa dhamira njema ya Serikali kuhakikisha kwamba inasogeza huduma za jamii karibu zaidi na wananchi. Hiyo ndiyo sababu ya msingi Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mikumi ilianzishwa lakini pia na mamlaka za miji midogo maeneo mengine kote nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niwapongeze Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mikumi kwa kuwepo kazini kwa zidi ya miaka 20 lakini pia kwa kuwasilisha maombi ya kuomba kuwa Halmashauri ya Mji wa Mikumi kwa kufuata taratibu zote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI tunatambua kwamba Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mikumi ishawasilisha maombi yao na taratibu zinazoendelea sasa ni kujiridhisha na vigezo hivyo. Pale wakati utakapofika kwa ajili ya kuanzisha Halmashauri ya Mji wa Mikumi basi hatua hizo zitachukuliwa kwa manufaa ya wananchi wa Mikumi, ahsante.