Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuweka Kituo cha Forodha Kakozi Momba ili kuunga mkono jitihada za kujenga Soko la Mazao la Kimataifa?

Supplementary Question 1

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa nafasi, kwa kuwa Julai, 2021 Waziri wa Fedha na Mipango alifanya ziara na kutembelea Kituo hicho cha Forodha na majibu ya Serikali yanasema kwamba, wanafanya tathmini kwa kina.

Je, tathmini hiyo ya kina itachukua muda gani kukamilika (time frame)?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kutokana na umuhimu wa Kituo chenyewe cha Forodha cha Tunduma, kwa sababu kimebeba nchi nyingi za Kusini mwa Afrika - SADC na kituo kile kuonekana kuzidiwa katika kutoa huduma za forodha. Je, Serikali haioni kuna haja na uharaka sana wa kuongeza Kituo kingine cha Forodha kwenye ule mpaka ambako ni Kakozi, kwa ajili ya kunusuru mapato yanayopotea na kuongeza mapato kwa Taifa? Ahsante.

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Condester. Hata hivyo, kabla ya kujibu naomba nimpongeze sana kwa namna anavyofuatilia kituo hiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, tathmini itakamilika ndani ya mwaka huu wa fedha. Nimwombe tu Mheshimiwa Mbunge awe na subira, Serikali iko kazini na atapata mrejesho.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, naomba nimwelekeze Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania, aangalie uharaka wa ujenzi wa kituo hicho huko Kakozi – Momba, endapo atajiridhisha kutokana na tathmini yake.