Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Primary Question

MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza:- Je, ni kwa kiwango gani Serikali imejiimarisha kukagua miamala ya uhamishaji wa bei ya mauzo ya bidhaa na huduma baina ya makampuni ya Kimataifa.

Supplementary Question 1

MHE. LUHAGA J. MPINA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri kwa kweli ya Naibu Waziri lakini ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, maboresho aliyoyasema Mheshimiwa Naibu Waziri ni makubwa. Je, hayo maboresho yametusaidia kuongeza kaguzi kiasi gani ikilinganishwa na kaguzi zilizokuwepo ambayo ilikuwa ni asilimia 1.2 kati ya makampuni 504 yanayojihusisha na miamala ya transfer pricing?

Swali la pili, Je, maboresho hayo yaliyofanywa na TRA yametuwezesha kuokoa fedha kiasi gani zilizokuwa zinapotea kutokana na kukosekana uwezo ndani ya nchi wa kukagua miamala ya transfer pricing?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Luhaga Joelson Mpina, kama ifuatavyo:-

Maboresho hayo ambayo tumefanya kupitia TRA yameongeza asilimia 4.5, mwaka uliopita kabla kufanya maboresho hayo ilikuwa tuko asilimia 1.2 lakini sasa tuko asilimia 4.5 kwa hiyo ni hatua kubwa sana ambayo tumepiga.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili ni suala la kitakwimu naomba tumpelekee kwa maandishi. (Makofi)

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. LUHAGA J. MPINA aliuliza:- Je, ni kwa kiwango gani Serikali imejiimarisha kukagua miamala ya uhamishaji wa bei ya mauzo ya bidhaa na huduma baina ya makampuni ya Kimataifa.

Supplementary Question 2

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali katika huduma za miamala hapa kwetu nchini, mara nyingi mashine za huduma kwenye maeneo ya huduma za fedha, zinaonyesha kwa muda huu hatutakuwa na huduma ya upatikanaji wa risiti.

Je, kama ni tatizo la kimfumo Serikali haioni kuwa inapoteza mapato?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama kulikuwa na tatizo hilo la risiti ilikuwa ni tatizo la muda mfupi na tayari tatizo hilo tumeshaliweka sawa. Sasa manunuzi yoyote yatakuwa yanatolewa risiti kwa njia ya elektroniki bila shaka nikutoe shaka Mheshimiwa Mbunge, kwa sasa hakutokuwa na mwanya wowote wa kupoteza mapato yetu. (Makofi)