Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuzipatia magari ya wagonjwa Hospitali za Wilaya za Liwale, Nachingwea na Kilwa?

Supplementary Question 1

MHE. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali. Naomba kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mkoa wa Lindi una maeneo mengi sana yaliyoko mbali na hospitali za Wilaya yakiwepo Kilimarondo kule Nachingwea, Nanjilinji Kilwa, Milola kule Mchinga; je, Serikali itatupa kipaumbele kutupatia magari hayo yaliyoongezwa katika maeneo hayo? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Tecla Mohamed Ungele, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, magari haya yatakayoletwa kuna halmashauri zitapata magari zaidi ya moja. Sababu ya halmashauri hizo kupata magari zaidi ya moja itakuwa ni kukidhi vigezo vya kitaalamu, ikiwemo umbali kutoka kituo hicho kwenda kituo kingine cha jirani, lakini pia population ya eneo hilo pamoja na mazingira ya kijiografia. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Ungele kwamba, tutafanya tathmini kwa Halmashauri hizo alizozitaja ili kuona kama zinakidhi vigezo hivyo. Ahsante.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuzipatia magari ya wagonjwa Hospitali za Wilaya za Liwale, Nachingwea na Kilwa?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Hospitali ya Mkoa wa Simiyu muda mrefu hatuna gari la kukusanya damu salama; je, ni lini Serikali itatununulia gari la kukusanya damu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, magari katika hospitali za rufaa za mikoa yanaratibiwa na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, lakini kwa kushirikiana kwa karibu na Wizara ya Afya. Kwa hiyo, kwa sababu hospitali hii iko chini ya Wizara ya Afya tutawasiliana na Wizara ya Afya ili tuone uwezekano wa kupata gari hilo kwa ajili ya huduma za damu. Ahsante.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuzipatia magari ya wagonjwa Hospitali za Wilaya za Liwale, Nachingwea na Kilwa?

Supplementary Question 3

MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Naomba niulize swali la nyongeza.

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka magari ya wagonjwa katika Jimbo la Mbulu Mji na Mbulu Vijijini?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asia Halamga, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, magari mawili yatanunuliwa na kupelekwa Halmashauri ya Mbulu Mjini na Mbulu Vijijini. Ahsante.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuzipatia magari ya wagonjwa Hospitali za Wilaya za Liwale, Nachingwea na Kilwa?

Supplementary Question 4

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na mimi kunipa nafasi niulize swali la nyongeza: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na uhitaji mkubwa wa gari la wagonjwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Liwale lakini tunayo shida kubwa ya magari ya chanjo. Watoto sasahivi ni miaka miwili hawapati chanjo kwa sababu ya ukosefu wa gari; je, Serikali haioni umuhimu wa kutupatia gari kwa ajili ya chanjo za watoto?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kuchauka, Mbunge wa Jimbo la Liwale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mbali na magari 195 ya wagonjwa Serikali itanunua magari mengine 204 kwa ajili ya shughuli za usimamizi, lakini pia shughuli za chanjo. Kwa hiyo pamoja na halmashauri zote kupata magari ya wagonjwa kutakuwa na gari jingine ambalo litakuwa kwa ajili ya shughuli za usimamizi na shughuli za chanjo. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Kuchauka kwamba, gari hilo pia litakuja sambamba na gari la wagonjwa.

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuzipatia magari ya wagonjwa Hospitali za Wilaya za Liwale, Nachingwea na Kilwa?

Supplementary Question 5

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya Likombe kilichopo Mtwara ndicho pia kinatumika kama hospitali ya Wilaya kwa sababu katika Wilaya hiyo hakuna hpspitali ya Wilaya;

Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa kwa sababu kuna wagonjwa wengi hasa akinamama wanaotaka kujifungua?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hokororo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba, Kituo cha Afya cha Likombe kina-serve kama hospitali ya halmashauri kwa sababu hatuna hospitali ya manispaa. Hata hivyo, nimhakikishie kwamba Manispaa ya Mtwara ni moja ya halmashauri zitakazopata gari la wagonjwa. Kwa hiyo nimuelekeze mkurugenzi kuhakikisha unazingatia vigezo ikiwezekana wapeleke gari hili katika kituo hiki kwa kadiri ya vigezo ambavyo vimewekwa na Serikali. ahsante.