Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka Gari la Zimamoto Handeni Mjini?

Supplementary Question 1

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa, magari matano ni machache sana kwa mikoa yote na Wilaya zote zenye uhitaji, je, Mheshimiwa Naibu Waziri anatuhakikishiaje wananchi wa Handeni Mjini, kwamba magari haya matano yatakapowasili moja litapelekwa Handeni Mjini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; mwaka wa fedha 2023/2024 umebakiza miezi minne tu kukamilika, je, Serikali ipo katika mchakato gani wa manunuzi kwa magari haya matano ya zimamoto? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Reuben Kwagilwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeshasema kwenye jibu la msingi katika haya magari pamoja na uchache wake, Handeni mtazingatiwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka niwaeleze Waheshimiwa Wabunge kwa ujumla kwamba Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan imeridhia kupata mkopo wenye masharti nafuu wa zaidi ya Dola za Kimarekani milioni 100 zitakazowezesha kupata magari na vitendea kazi vingine kwa ajili ya kuliimarisha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji. Mara vifaa hivyo vitakapopatikana, mikoa yote na Wilaya zote ambazo hazina vitendea kazi hivyo watapata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali la pili kuhusu mchakato wa manunuzi umefikia wapi, nataka nikuhakikishie, mchakato wa manunuzi uko hatua nzuri. Mara hizo fedha zitakapopatikana kutoka Hazina malipo yatafanyika ili tuweze kupata vifaa hivyo kabla mwaka wa fedha haujamalizika, nashukuru.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka Gari la Zimamoto Handeni Mjini?

Supplementary Question 2

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi, nina swali kwa Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba, Jimbo la Ndanda lenye kata 16 tunacho Kituo cha Polisi kimoja tu kilichopo Ndanda. Hata hivyo, majengo ya Kituo cha Polisi pamoja na nyumba ya Mkuu wa Kituo cha Polisi Ndanda, kwa maana ya OCS, ni mali ya Wamisionari wa Benediktini wa Ndanda. Kutokana na umuhimu na ukubwa wa Jimbo la Ndanda, kuna haja ya kuwa na Kituo cha Polisi kwenye Kata ya Chiwale. Nini msimamo wa Serikali wa kujenga Kituo cha Polisi kwenye Kata ya Chiwale?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo tunaongea kwa nyakati tofauti, ni dhamira ya Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuhakikisha kwamba kata zote na tarafa za kimkakati zinajengewa vituo vya Polisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nyakati tofauti nimeongea na Mheshimiwa Mbunge wa Ndanda na ninamshukuru sana kwa namna anavyofuatilia suala la usalama wa raia wa jimbo lake; na kwa vile kuna mfuko wa jimbo kidogo ambao anapata, wajitahidi tu kuanzisha ujenzi na Wizara ya Mambo ya Ndani kupitia Jeshi la Polisi lita-support ujenzi wa hicho kituo hadi kitakapomalizika, nashukuru.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka Gari la Zimamoto Handeni Mjini?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Wilaya ya Tarime inajumuisha Halmashauri ya Mji wa Tarime, Mji wa Sirari, Nyamwaga na Nyamongo, miji ambayo inakua kwa kasi kubwa sana na kusababisha ujenzi wa makazi au hoteli za ghorofa, lakini tumekuwa hatuna gari la zimamoto, na mara kadhaa tunapopata majanga ya moto inasababisha maafa makubwa bila msaada wowote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kujua sasa, katika haya magari matano ambayo Waziri amesema hapa, ni lini Tarime itapata, maana mara kadhaa nimesimama nikiomba gari la zimamoto kwenda Tarime? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimeeleza kwenye jibu la msingi la nyongeza kwamba Serikali ina mpango wa kutumia zaidi ya shilingi bilioni 200 kununua magari na vitendea kazi vingine kuwezesha Jeshi la Zimamoto na Uokoaji. Kwa hiyo, fedha hizo zitakapopatikana, Wilaya ya Tarime ni moja ya Wilaya zitakazonufaika, na ninaamini zitapatikana kabla ya mwaka huu wa fedha haujakamilika, nashukuru.