Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA aliuliza: - Je, lini Tanzania itajiunga na Mkataba wa Budapest ili kujiimarisha na mapambano dhidi ya makosa ya kimtandao?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali la nyongeza. Nimshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri, niishukuru Serikali kwa majibu mazuri; lakini swali moja la nyongeza. Kuna hasara gani kwa Serikali yetu au kwa nchi yetu kujiunga na Mkataba wa Budapest ambao upo leo tukisubiri huo wa Umoja wa Mataifa ambao bado na una matatizo makubwa ambao haujakamilika? tujiunge na wa Budapest kusudi ikitokea tatizo hapa kati kati tuwe salama.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Jasson Samson Rweikiza, Mbunge wa Bukoba Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Awamu ya Sita ingependa kujiunga na Mikataba ya Kimataifa kama nchi zingine zinavyofanya lakini tunachokiangalia ni kutazama kwa kina huu Mkataba tunapoenda kujiunga nao una tija gani kwa Watanzania. Kwa hasara ambayo inaweza ikapatikana, kwanza kabisa katika Mkataba huu tulitamani kwamba tujiunge lakini Budapest Convention wameongeza itifaki, wanasema additional protocol of disclosure of electronic evidence. Maana yake kwamba inaruhusu mataifa mengine kuingilia mifumo yenu na kupata evidence on real time, hii ni hasara kubwa sana kwa nchi ambazo bado tuko nyuma kiteknolojia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo lingine, mkataba huu wakati unaanzishwa umejengwa katika hiyo pin context haukuwa na ushirikishwaji wa mataifa mengine; kwa hiyo ni ngumu sana kama Taifa kwenda kujiunga na Mkataba huu. Lakini tunafanya nini kuhakikisha kwamba hasara kama hizi hatuwezi kuzipata? Ni kweli kabisa kutojiunga nao inawezekana tunapohitaji kupata ushirikiano inapotokea mtu amefanya kosa yupo katika nchi za kwao hatuwezi kupata ushirikiano; na tunafanya nini kama Serikali?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali tunaenda kujiunga na Mkataba na Malabo Convention. Mkataba huu umeongelea maudhui ya kuhakikisha kwamba tuwe na electronic transaction act, ambayo tayari Tanzania tunayo, tuwe na cyber security act ambayo Tanzania tunayo, tuwe na personal data protection act, Tanzania tayari tunayo; na sasa tayari tumeishapokea maoni kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ili tukamilishe ili tuweze ku-ratify kama nchi; na huu ni Mkataba ambao umetokana na African Union. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na huo sasa, tukishakamilisha kujiunga na Mkataba wa African Union maana yake sasa tutaenda kujiunga na ule mkataba, kama nilivyojibu katika jibu la msingi, tutajiunga na ule Umoja wa Mataifa. Ambapo maana yake European, African Union wote kwa pamoja tutakuwa tunauwezo wa kupata ushirikiano pale ambapo tunakuwa tunashughulikia makosa ya kimtandao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. (Makofi)