Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Amandus Julius Chinguile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa leseni kwa wachimbaji wadogo wa madini Kata za Nditi na Kiegi – Nachingwea na maeneo mengine ya Mkoa wa Lindi?

Supplementary Question 1

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Ziko Leseni zimetolewa kwa ajili ya shughuli za utafiti kwenye maeneo mbalimbali nchini, ikiwemo Jimboni Nachingewa lakini wahusika hawajafanya shughuli hiyo iliyokusudiwa kwa muda mrefu sasa.

Je, Serikali haioni sasa iko haja ya kupitia sheria yetu ili kuweza kuondoa utitiri wa hawa watafiti ambao kimsingi hawatimizi majukumu hayo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kuambatana na mimi baada ya kipindi hiki cha Bunge ili kwenda Jimboni Nachingwea kuona halihalisi iliyoko na kuwatia moyo wachimbaji wadogo wadogo? (Makofi)

Name

Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, napenda kumjibu Mheshimiwa Chinguile, Mbunge makini wa Nachingwea, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu waliopewa leseni na wamezilaza hawazifanyii kazi; mwezi wa tisa na mwezi wa kumi tulitoa kama ndiyo kipindi cha mwisho, waweze aidha kufanyia leseni zao kazi au zifutwe. Tangu tangazo hilo litoke, zaidi ya leseni 7,000 zimeshahuishwa na kuna wale ambao hawajaweza kuhuisha mpaka tarehe 30 mwezi uliopita, mchakato wa kuzifutia hizo leseni unaendelea. Hatukuishia hapo, zilizokwishaharibiwa kwa kutofanyiwa kazi huko nyuma, maeneo zaidi ya 48 zimegawiwa kwa wachimbaji wadogo.

Mheshimiwa Spika, hivyo hata katika jimbo lake, wale ambao watashindwa kuendeleza leseni kwa mujibu wa tangazo hilo la Serikali kupitia Wizara ya Madini, watarudisha hizo leseni na tutawapa wale ambao wako tayari.

Mheshimiwa Spika, kwa swali lake la pili, mimi niko tayari baada ya Bunge hili, nitampangia ratiba. Tutafika huko tuwatie moyo wachimbaji wadogo wanaofanya shughuli zao na kuwahamasisha wengine watumie fursa zilizoko katika Wizara ya Madini kupata uwekezaji ambao utawainua katika Maisha yao. ahsante sana. (Makofi)