Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jonas Van Zeeland

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha kusambaza umeme kwenye Kata za Kikeo, Kinda na MaskatI – Mvomero?

Supplementary Question 1

MHE. JONAS V. ZEELAND: Mheshimiwa Spika, naomba niulize maswali mawili madogo ya nyongeza.

Swali la kwanza; kwa kuwa Mvomero ni miongoni mwa Wilaya ambazo ziko vijijini; na kwa kuwa, Kijiji cha Madizini, Lusanga, Manyinga, Turiani, Kilimanjaro na Kichangani, havikuwahi kupata hadhi ya kisheria kuwa miji midogo; Mheshimiwa Naibu Waziri, huoni sasa kuna haja ya kutoa maelekezo wananchi wa vijiji hivi walipie umeme kwa shilingi 27,000 badala ya kulipia umeme kwa shilingi 321,000? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Wananchi wa Tarafa ya Turiani wamekuwa wanapata adha kubwa sana ya kukatika kwa umeme: Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, huoni sasa ni wakati muafaka kutenga bajeti ya kwenda kuboresha miundombinu hii inayotoka Morogoro kuelekea Turiani ya kupeleka umeme kwa sababu miundombinu hii ni ya muda mrefu na imechakaa kwa kiwango kikubwa sana? Nashukuru sana. (Makofi)

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jonas Zeeland, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na Vijiji vya Madizini, Lusanga, Manyinga, Kilimanjaro, Kichangani na Turiani, vilitolewa tangazo, lakini havijaidhinishwa kama miji midogo. Kwa hiyo, niwaelekeze TANESCO Mkoa wa Morogoro kuendelea kuwa-charge wananchi 27,000 kwa maeneo haya yote ambayo hayajaidhinishwa kama miji kidogo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na suala la pili la line ya umeme inayotoka Turiani kwenda Kilosa na Gairo, mwaka huu wa fedha tumetenga bajeti ya matengenezo. Nikuahidi, kama matengenezo hayatakamilika, mwaka ujao wa fedha tutaendelea kutenga bajeti ili kuhakikisha tunaboresha miundombinu hii ili wananchi waendelee kupata umeme wa uhakika, ahsante. (Makofi)

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha kusambaza umeme kwenye Kata za Kikeo, Kinda na MaskatI – Mvomero?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona; ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye vitongoji zaidi ya asilimia 70 katika Wilaya ya Kyerwa?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Oliver Semuguruka, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tayari Serikali tumeanza mpango wa kupeleka umeme kwenye vitongoji vyote vilivyobakia 36,000. Kwa kuanza, tumeanza kwa miradiya ujazilizi ambayo tumeshaweka wakandarasi na vilevile tunategemea kuendelea kutafuta wakandarasi kwa Mradi wa Vitongoji 15 kwenye kila jimbo. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, vitongoji katika Jimbo la Kyerwa na vyenyewe vitafikiwa, ahsante. (Makofi)

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha kusambaza umeme kwenye Kata za Kikeo, Kinda na MaskatI – Mvomero?

Supplementary Question 3

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, napenda kujua, lini wananchi wa Jimbo la Bunda watapata umeme wa REA II C kwa vijiji 147?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Getere, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa mradi wetu wa II C tumetenga vitongoji 17 na kwa mradi ujao pia, vitongoji 15 Jimbo la Bunda litapata. Kwa hiyo, kwa kuanzia wataanza na vitongoji 32, ahsante.

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha kusambaza umeme kwenye Kata za Kikeo, Kinda na MaskatI – Mvomero?

Supplementary Question 4

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa, tulisema mpaka mwezi wa 12 mwaka huu, vijiji vyote vitakuwa vimepata umeme na bado kuna vijiji kama Kiteto hatujapata umeme. Nini kauli ya Serikali kwa mpango huu wa mwezi wa 12 vijiji vyote vipate umeme?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Edward Olelekaita, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli, Wakandarasi wote ambao tumewapatia mikataba ya kwisha Desemba 30, kupeleka umeme kwenye vijiji vyote, lazima wakamilishe kupeleka umeme kulingana na mikataba yao. Wale ambao walipewa ziada mpaka Juni, 2024 wata-cross kwenda 2024. Niwaelekeze Wakandarasi wote, yeyote ambaye hatahakikisha anamaliza mkataba wake kwa muda, bila sababu za msingi, hatutasita kuchukua hatua na kuweza kutokuendelea na mkataba wake ikifika Desemba, 30 mwaka huu, ahsante.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha kusambaza umeme kwenye Kata za Kikeo, Kinda na MaskatI – Mvomero?

Supplementary Question 5

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa kuwa vitongoji vinavyopewa umeme ni vile ambavyo line za umeme kubwa tayari zilishapita, lakini kwenye jimbo langu kuna Kitongoji kama Nindi na Songeapori ambavyo viko mpakani na kuna changamoto kubwa za kiusalama.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuvisaidia vitongoji hivi viwili kwa jicho la kipekee? (Makofi)

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Stella Manyanya, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, vitongoji hivi viwili kwa kweli, vimekaa kimkakati. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwa awamu hii ya ujazilizi utaweka addition scope ili vitongoji hivi viweze kufikiwa na umeme kwa umahususi wake, ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha kusambaza umeme kwenye Kata za Kikeo, Kinda na MaskatI – Mvomero?

Supplementary Question 6

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi ya swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, usambazaji wa umeme wa REA katika Kata ya Nanjirinji na Kata ya Likawage, umekwama kwa sababu ya mgogoro kati ya TFS pamoja na mkandarasi. Nini Kauli ya Serikali katika kutatua mgogoro huu ili wananchi wapate umeme huo? (Makofi)

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Kassinge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge nikuahidi, nitafuatilia suala hili ili kuhakikisha linatatuliwa kwa wakati na wananchi waweze kupata umeme katika maeneo yao, ahsante.

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JONAS V. ZEELAND aliuliza:- Je, lini Serikali itakamilisha kusambaza umeme kwenye Kata za Kikeo, Kinda na MaskatI – Mvomero?

Supplementary Question 7

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, je, ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye vijiji sita vilivyobakia kwenye Tarafa ya Mikumi?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mkandarasi katika vijiji hivi yuko site anaendelea na kazi. Nimhakikishie tu, ifikapo Juni, 2024 vijiji hivi vyote vitakuwa vimepatiwa umeme, ahsante.