Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Janejelly Ntate James

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JANEJELLY J. NTATE aliuliza: - Je, lini Serikali itaweka mkakati maalum wa kumaliza mashtaka katika Bodi na Mahakama za Rufaa za Kodi?

Supplementary Question 1

MHE. JANEJELLY J. NTATE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri ya Serikali lakini bado kuna hela nyingi ziko pale kwenye hizi TRAT na TRAB. Kuna shilingi bilioni 600 zipo TRAB na shilingi trilioni 2.29 bado zipo TRAT.

(a) Je, Serikali mnatupa muda gani wa kuwa mmemaliza hizi hela zirudi kwenye Mfuko wa Serikali zikafanye kazi za maendeleo? (Makofi)

(b) Katika kuchelewesha huku na kusuasua, hamuoni kwamba tunaharibu mahusiano mema ya Serikali na wafanyabiashara ambao ndiyo tegemeo letu la mapato? (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA: Mheshimiwa Spika, kwanza ninampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia jambo hili ambalo ni muhimu sana na amejenga hoja za Kibunge. Niliyaepuka haya maneno ya TRAT na TRAB lakini kwa kuwa ameshayasema ngoja niyasema tu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, moja; fedha zile ambazo zipo zinabishaniwa kabla hazijaamuliwa haziwi fedha za Serikali ni fedha zinazobishaniwa, na katika kubishaniwa kwake na hivi sasa tumeanzisha Ofisi hiyo ya Msuluhishi, kimsingi Serikali inataka kujenga mahusiano mazuri na walipakodi, kwa sababu Serikali ingenyoosha mkono tu kwamba hapa tunachokadiria sisi ndiyo tunataka ulipe, hiyo ndiyo ingeharibu mahusiano na walipakodi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo zitakuwa fedha za Serikali mpaka pale ambapo mkono mwingine whether TRAB ama TRAT itakaposema kwamba hii sasa ni fedha ya Serikali, lakini ikiwa bado inabishaniwa Serikali inatoa fursa ya haki kutendeka na vyombo hivyo vinaongozwa na watu ambao ni maarufu katika tasnia ya sheria. Kwa hiyo, tunaamini haki itaendelea kutendeka.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kuharakisha ndiyo tumetengeneza utaratibu wa kuanzisha hizi sessions maalum ili haya mambo yasiwe yanakaa sana, kwa sababu yanaondoa utulivu katika ufanyaji wa biashara.

Mheshimiwa Spika, lingine kama ambavyo nimeweka kwenye jibu la msingi, uwepo wa ofisi hii ambayo wafanyabiashara wameitamani siku nyingi ya Msuluhishi wa Masuala ya Kikodi, tunaamini na yenyewe itaenda kupunguza mrundikano wa masuala yanayobishaniwa kwa sababu sasa maeneo ambako makadirio hawakuridhiana yataenda kwa mtu mwingine ambaye hayuko kwenye mfumo ule wa kukadiria.