Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, lini Serikali itaimarisha Mawasiliano ikiwemo Minara ya Simu na usikivu wa Radio ya Taifa (TBC) – Kondoa?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY J. MAKOA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi, kuuliza maswali ya nyongeza. Nina maswali mawili, kama Mbunge wa Jimbo la Kondoa Mjini, nimewauliza wenzangu kule Kondoa, kwamba yapo majengo yaliyokamilika na mitambo na vitu vingine kama hivi vimejengwa Kondoa, lakini sifahamu huo mradi mkubwa namna hiyo umefanywa halafu Mwakilishi wa Wananchi na hata Mkuu wa Wilaya hana habari. Sasa ninataka kujua, je, majengo haya yamejengwa wapi? Na mitambo hii imejengwa wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, majibu ya kusema tathmini itaanza, ninapenda kufahamu hapa nyuma tumeambiwa Serikali imetoa minara mingi sana kwenye nchi hii karibu wilaya zote. Hapa ninapokuambia jimbo langu si vijiji ni mitaa, kwenye minara mitano iliyokwenda Kondoa hakuna mnara hata mmoja ambao unakwenda kwenye Mtaa wa Jimbo la Kondoa Mjini. Wewe ni shahidi ukitoka Dodoma kilomita 30 tu, kuelekea huko tayari mawasiliano yote yanakatika barabara hii ni kubwa. Sasa ninataka nijue Serikali inawaambia nini Wananchi wa Kondoa Mjini na Mitaa yake ambayo haina mawasiliano? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Juma Makoa, Mbunge wa Kondoa Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninampongeza sana Mheshimiwa Mbunge, kwa kweli alivyoingia tu Bungeni hoja yake ya kwanza ilikuwa nikuhakikisha kwamba Kondoa wana Mtambo ambao utaenda kuhudumia Wananchi wa Kondoa, ili TBC iweze kusikika kwa ajili ya wananchi wake. Serikali ilipokea ombi lake na tayari Serikali imeshajenga, imejenga mnara imejenga jengo na pia, imeshaweka jenereta. Eneo gani mtambo huu umejengwa? Ukiwa unaelekea Arusha upande wa kulia pale ambapo majengo ya halmashauri yanapojengwa pale, kwenye kona pale na ndio mtambo wetu upo na mnara wetu upo pale. Mimi mwenyewe ninaufahamu na nilishafika pale. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ninachoweza kusema ni jambo moja kwamba ninawaomba TBC wanapoenda kutekeleza miradi ya maendeleo ndani ya Majimbo ya Waheshimiwa Wabunge wahakikishe wanawashirikisha Waheshimiwa Wabunge pamoja na Madiwani na Ofisi za Halmashauri ili kuhakikisha kwamba miradi hii inakuwa nishirikishi. Kwa hiyo, hayo ni maelekezo yangu kwa TBC. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, ni kweli tumeshafanya tathmini. Tunapofanya tathmini hatua ya pili nikupata fedha kwa ajili ya kufikisha huduma ya mawasiliano. Maeneo yetu bado ni mengi ambayo bado yana changamoto. Kipaumbele cha Mheshimiwa Rais, ilikuwa ni kuhakikisha maeneo ya mipakani, kuhakikisha maeneo ambayo yapo vijijini. Vile vile, kuhakikisha tunawashawishi watoa huduma wakawekeze katika maeneo ya mjini ili kuhakikisha kwamba haya maeneo yote yana huduma ya mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ninampa matumaini Mheshimiwa Mbunge, kwamba jambo lake la Kondoa ni jambo la Serikali ya Chama Cha Mapinduzi na tunalipokea tutaenda kulifanyia kazi na kuchukua hatua stahiki ili wananchi wa Kondao wapate huduma ya mawasiliano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, lini Serikali itaimarisha Mawasiliano ikiwemo Minara ya Simu na usikivu wa Radio ya Taifa (TBC) – Kondoa?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na ninakushukuru kwa kunipa nafasi ili niulize Serikali swali moja. Usikivu wa TBC ndani ya Mkoa wa Rukwa ni wa taabu na hususani katika Wilaya ya Kalambo hakuna kabisa, najua kuna juhudi za Serikali kujenga mtambo pale Kijiji cha Mkoi. Je, ujenzi huo utaanza lini ili Wananchi wa Mkoa wa Rukwa wapate usikivu wa TBC? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kandege, Mbunge wa Kalambo, kama ifuatavyo:

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa amekuwa mstari wa mbele kuwatetea sana wananchi wake na anahitaji wasikilize TBC Taifa. Sisi kama Serikali tulilipokea ombi lake na tulishaliingiza kwenye bajeti. Hivyo, ninamuomba Mheshimiwa Mbunge awe na subira wakati utekelezaji utakapoanza basi tunashirikisha kwa hatua zaidi, ahsante sana. (Makofi

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, lini Serikali itaimarisha Mawasiliano ikiwemo Minara ya Simu na usikivu wa Radio ya Taifa (TBC) – Kondoa?

Supplementary Question 3

MHE. STELLA S. FIYAO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninashukuru. Maeneo mengi ya Wilaya ya Ileje, kuna changamoto kubwa ya mawasiliano ni upi mpango wa Serikali kupeleka miundombinu ya mawasiliano ya kutosha ili kurahishisha huduma kwa wananchi wa Wilaya ya Ileje?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge, ni Mjumbe wa Kamati ya Miundombinu na kwa bahati nzuri amekuwa mshauri mzuri sana katika Wizara yetu kuhakikisha kwamba tunatatua changamoto za mawasiliano. Jambo jema kabisa ni kwamba katika minara ile 758, kati ya Majimbo ambayo yamebahatika sana ni Jimbo la Ileje ambalo limepata minara mitano. Kwa hiyo, ipo katika hatua mbalimbali za utekelezaji, hivyo, tumuombe Mheshimiwa Mbunge aendelee kutupatia ushirikiano kuhakikisha kwamba wananchi wanatoa maeneo bila kuwa na masharti magumu ili tuhakikishe kwamba miradi hii inaanza kwa wakati na kukamilika kwa wakati, ninakushukuru sana. (Makofi)