Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je, lini Serikali itatenga fedha kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Kijiji cha Magungu – Kiteto?

Supplementary Question 1

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na ninaipongeza Serikali kwa majibu mazuri sana. Hata hivyo, kwa ajili ya kuweka record sawa ni Kituo cha Magungu, siyo Magugu, Magugu ni kwa Mheshimiwa Mwenyekiti pale. Vilevile, jina langu ni Kisau siyo Kisua, Kisua kwa Kichaga ni yule beberu mdogo. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, baada ya kusema hivyo, nina maswali mawili ya nyongeza. Ninawapongeza Wananchi wangu wa Kiteto ni waungwana sana, unajua wananchi kujenga Vituo vya Polisi siyo jambo dogo sana. Kwa kuwa Wananchi wa Kijungu nao wamejenga Kituo cha Polisi na imefikia lenta wametumia milioni 15 mpaka 20. Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa nini, msiweke hiyo bajeti ya 2024/2025 ili kumalizia kama mlivyofanya kwa wenzao wa Magungu hapo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa aliyekuwa IGP, 2014/2015 alitoa ahadi ya kujengwa Kituo cha Polisi Kijiji cha Chekanoa, na kwa kuwa Mji Mdogo wa Matui unahitaji kituo chenye hadhi ya polisi. Ni lini Mheshimiwa Naibu Waziri utatembelea Kiteto ili tukague vituo hivi vya polisi? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ninawapongeza wananchi wa Jimbo la Kiteto, kwa juhudi hizi wanazozifanya kwa ajili ya kuhakikisha uwepo wa usalama wa wananchi na mali zao kwa kujenga vituo hivi vya polisi. Ninamshukuru Mheshimiwa Mbunge, kwa wito wako na nipo tayari baada ya Bunge hili kuunga nawe kutembelea eneo lako la Kiteto. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Kata hii ambayo pia wameanza, ni ahadi yetu kwamba wananchi walionesha juhudi za kuanza tutawaunga mkono kwa kutenga fedha za maendeleo na fedha nyingine kutoka Mfuko wa Tuzo na Tozo ili kukamilisha majengo hayo yaweze kufanya kazi iliyokusudiwa. Kuhusu ahadi ya IGP aliyepita nitamkumbusha IGP aliyepo madamu ilikuwa ni ahadi ya Jeshi la Polisi, ili aweze kusaidiana na wananchi hawa wa Chekanao kujenga kituo hicho kilichoahidiwa, nakushukuru. (Makofi)

Name

Dr. Pius Stephen Chaya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je, lini Serikali itatenga fedha kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Kijiji cha Magungu – Kiteto?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. PIUS S. CHAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipata nafasi hii. Kituo cha Polisi cha Sanza, ni chakavu sana ambacho kipo katika Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni. Nini mkakati wa Serikali wa kuwasaidia Wananchi wa Sanza kujenga kituo kipya cha Polisi? Ahsante sana.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uchakavu wa Kituo hiki na Mheshimiwa ameomba tujenge Kituo Kipya. Naomba anikubalie tufanye tathmini ya kiwango cha uchakavu wa kituo kilichopo. Tutakapobaini gharama za kufanya ukarabati ni kubwa au zinakaribia kulingana na ujenzi wa kituo Kipya. Basi tutaunga mkono juhudi zako kwa kujenga kituo kipya, nashukuru sana. (Makofi)

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je, lini Serikali itatenga fedha kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Kijiji cha Magungu – Kiteto?

Supplementary Question 3

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru sana, Wilaya ya Mbulu ni Wilaya kongwe Serikali ina mkakati gani wa kujenga vituo vya polisi katika Tarafa za Nambis na Tarafa ya Daudi, ili kuweza kupeleka huduma karibu na wananchi? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhamira ya Serikali kila mara tunapokuwa na Vijiji au Miji Midogo inayokuwa kwa kasi hasa katika shughuli za kiuchumi na kuvutia vitendo vya uhalifu kuzingatia kwamba maeneo hayo tunayapa miundombinu ya kulinda usalama wa maisha ya watu na mali zao. Kwa hiyo, Tarafa alizo zitaja Mheshimiwa Mbunge tutazifanyia tathmini na wenzetu wa Mkoa wa Manyara kwa maana ya RPC, kuona kama pana mahitaji tuweze kuzitengea fedha kwenye bajeti zetu ili vituo hivyo viweze kujengwa, ninashukuru. (Makofi)

Name

Mohammed Said Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. EDWARD O. KISAU aliuliza: - Je, lini Serikali itatenga fedha kumalizia ujenzi wa Kituo cha Polisi Kijiji cha Magungu – Kiteto?

Supplementary Question 4

MHE. MOHAMED SAID ISSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru. Kituo cha Polisi Konde kilitengewa bajeti katika mwaka 2022/2023, hakikukarabatiwa, kikatengewa bajeti 2023/2024 mpaka leo hakijakarabatiwa. Nini kauli ya Serikali kuhusiana na suala hili? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge, atafahamu kwamba Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, imefanya juhudi za kujenga na kukarabati vituo katika maeneo mbalimbali yakiwemo maeneo ya Pemba na Unguja. Ni bahati mbaya kwamba bajeti haikutoka ndio maana ukarabati haukuweza kufanyika. Ninaomba nimuahidi bajeti ya mwaka huu itakapotoka Kituo cha Konde kitapewa kipaumbele, ahsante sana. (Makofi)