Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. JANETH M. MASSABURI aliuliza: - Je, magari mangapi ya Zimamoto yanahitajika kukidhi mahitaji halisi nchini?

Supplementary Question 1

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali ya nyongeza. Kwa kuwa matatizo ya moto yamekuwa mengi sana katika nchi yetu na hasa katika maeneo ya shule na masoko, lakini kumekuwa na changamoto kubwa ya magari ya zimamoto kufika maeneo ya tukio bila ya kuwa na maji. Tatizo hili limekuwa ni kubwa kiasi kwamba watu wanakata tamaa na Jeshi lao la Zimamoto. Je, ni nini kauli ya Serikali kuhusiana na changamoto hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Kwa kuwa katika nchi yetu kumekuwa na miradi mingi ya kimkakati ya Serikali kama vile standard gauge, Bwawa la Mwalimu Nyerere pamoja na bomba lile la mafuta la Chongoleani Hoima, je, Serikali imejipanga vipi katika kuweka tahadhari ya moto katika maeneo hayo? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali la mwanzo la kwamba magari yanafika yakiwa hayana maji, naomba leo nisaidie kuweka sawa hisia hizo kwa kusema yafuatayo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kawaida gari lenye uwezo wa kubeba lita 5,000 litakapofika kwenye eneo lenye athari ya moto, kwa pressure yake linaweza likazima moto kwa dakika mbili maji yale huwa yamekwisha. Sasa wananchi wana-tend kuamini kwamba halina maji linaenda kutafuta maji mengine. Ila ni kwa sababu dakika mbili tu lita 5,000 zinakuwa zimemalizika. Haiwezekani gari yetu iende kwenye tukio la kuzima moto halafu haina maji na kiuzoefu gari linapokuwa lime-park, always linakuwa na maji. Kwa hiyo, wananchi waondoe dhana hiyo potofu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, juu ya kuchelewa kufika ni changamoto ya miundombinu yetu, lakini na shughuli za kibinadamu zinazofanyika kwenye maeneo ambayo gari hilo linapita. Kama kila mwananchi ataelewa na akasaidia kufungua njia wakati wa dhararu kama hizo, tatizo kama hili litapungua.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu Serikali kuzingatia miradi ya kimkakati ikiwemo Bwawa la Mwalimu Nyerere, SGR, bomba la Chongoleani, napenda nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na Wabunge wote kwamba maeneo yenye uwekezaji wa kimkakati kama hizi kwa maana ya vital installation kuweka tahadhari ya kudhibiti matukio ya kuzima moto ni kipaumbele cha juu cha Serikali. Kwa hiyo, namhakikishia Bwawa la Mwalimu Nyerere na miradi mingine kama hiyo itazingatiwa katika kuwekewa magari na vifaa vya kuzima moto na uokoaji, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. JANETH M. MASSABURI aliuliza: - Je, magari mangapi ya Zimamoto yanahitajika kukidhi mahitaji halisi nchini?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana. Wilaya ya Muleba ni kati ya wilaya kubwa lakini haina gari la zimamoto. Ni lini Serikali itatupatia gari la zimamoto? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika majibu ya msingi nimeeleza mpango wa Serikali kutumia zaidi ya dola za Kimarekani milioni 100 kununua magari ya kuzima moto na vifaa vingine kwa ajili ya uokoaji, na tutakapokuwa tumepata mkopo huo na kununua magari hayo, Wilaya ya Muleba anapotoka Mheshimiwa Kikoyo itazingatiwa, ahsante sana. (Makofi)

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. JANETH M. MASSABURI aliuliza: - Je, magari mangapi ya Zimamoto yanahitajika kukidhi mahitaji halisi nchini?

Supplementary Question 3

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, ninashukuru kwa kunipa nafasi.

Ni lini Serikali itanunua gari la Zimamoto katika Mkoa wa Rukwa, kwa sababu Mkoa wa Rukwa hauna gari la Zimamoto hata moja? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua kwamba Rukwa haina gari kwa maana ya gari zima linalofanya kazi. Gari lipo ni bovu linaendelea kutengenezwa hatua kwa hatua. Ninamhakikishia Mheshimiwa Bupe kwamba mara magari haya yatakaponunuliwa Mkoa wako utazingatiwa katika mgao, nashukuru sana. (Makofi)