Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. HAMISI S. TALETALE aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Ngerengere?

Supplementary Question 1

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama yote hayo wanayafahamu, sasa ni zaidi ya mwaka wa tatu tumesimama hapa kuomba Kituo cha Afya cha Ngerengere, hakina jengo la Huduma ya Mama na Mtoto, Mortuary hakuna. Wakazi wa Kata ya Ngerengere ni 15,000, Kata ya jirani ya Kidugalo ni 8,000, leo hii Mheshimiwa Waziri anajibu majibu ambayo anafahamu tatizo liko wapi, mpaka nashindwa kuelewa. Naomba kumwuliza swali Mheshimiwa Waziri; je, ni lini mtakwenda kutatua hili tatizo? Siyo kwamba majibu mnayo na utatuzi hakuna, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hamisi Shabani Taletale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wa upanuzi wa Kituo cha Afya cha Ngerengere. Nasi kama Serikali, taarifa hii tunaifahamu na ndiyo maana tulitoa maelekezo kwa Mkurugenzi, kuongeza eneo la ujenzi wa Kituo cha Afya, ekari 4 na nusu hazitoshi kujenga Kituo cha Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kituo cha Afya hiki kilikuwa ni cha Mission, kwa hiyo, kilichukuliwa na Serikali kikiwa tayari kinatoka Mission. Namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba mara hili eneo la ekari mbili la Posta ambalo halijaendelezwa, ambalo liko mkabala kabisa na Kituo hiki, likishachukuliwa na kuwa na ekari sita na nusu, basi mapema iwezekanavyo tutatafuta fedha kwa ajili ya kuongeza majengo haya ambayo yanapungua katika Kituo cha Afya cha Ngerengere, ahsante. (Makofi)

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMISI S. TALETALE aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Ngerengere?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi nami niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Kata ya Mbande ya Chamazi katika Mkoa wa Dar es Salaam ni kata ambayo ina idadi kubwa ya watu, lakini wana Zahanati ya Mbande: Ni lini sasa Serikali itaipandisha Zahanati ya Mbande kuwa Kituo cha Afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mama Mariam Kisangi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba idadi ya wananchi katika Kata ya Mbande kule Chamazi ni kubwa na Zahanati ile ya Mbande kwa kweli inazidiwa na idadi ya wananchi na sisi Ofisi ya Rais, TAMISEMI tumeshaainisha kwamba eneo la Zahanati ya Mbande ni sehemu ya eneo la kimkakati kuona uwezekano wa kujenga Kituo cha Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hilo tunalifanyia kazi na tutahakikisha kwamba tunatafuta eneo linalotosheleza kama lile la Zahanati linatosha ama tunahitaji kupata eneo lingine kwa ajili ya kujenga Kituo cha Afya kwa manufaa ya wananchi walio wengi katika eneo lile, ahsante. (Makofi)

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. HAMISI S. TALETALE aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Ngerengere?

Supplementary Question 3

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa mwenyekiti, wananchi wa Kata ya Kabwe wana changamoto ya kijiografia na wanapata shida kubwa sana ya matibabu kuja Hospitali ya Wilaya; na ile ni ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kujengewa Kituo cha Afya. Ni lini mtapeleka fedha kumalizia kujenga kituo hicho ili wananchi wapate huduma?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Khenani, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba ahadi zinazotolewa na viongozi wetu wa Kitaifa ni kipaumbele katika utekelezaji. Kwa sababu hii ni ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, na ninakumbuka nilikuwa kwenye ziara yake, nakuhakikishia tayari tumeshaingiza kwenye Mpango Mkakati kwa ajili ya kutafuta fedha na kwenda kujenga Kituo cha Afya katika Kata ya Kabwe, ahsante. (Makofi)

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. HAMISI S. TALETALE aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Ngerengere?

Supplementary Question 4

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, kwa kuwa Tarafa ya Ndagalu Kata ya Ng’haya, Serikali ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu ilitoa fedha kwa ajili ya kuweka miundombinu kwenye Zahanati ya Ng’haya ili kuipandisha hadhi kuwa Kituo cha Afya.

Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya kukamilisha miundombinu ya zahanati hiyo kuwa Kituo cha Afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kiswaga, Mbunge wa Magu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, natumia nafasi hii kumsisitiza na kumkumbusha Mkurugenzi wa Halmashauri ya Magu, kwamba tulishawaelekeza kwanza kufanya tathmini ya majengo yanayopungua kwenye ile zahanati ili iwe na hadhi ya kupandishwa kuwa Kituo cha Afya. Kwa hiyo, nitafuatilia Mheshimiwa Kiswaga, tuweze kuona wamefikia hatua gani kwa maana ya Mkurugenzi na timu yake, pia tuone namna gani tunapata fedha, iwe ni kwa mapato ya ndani ya Halmashauri au kwa fedha kutoka Serikali Kuu ili tuweze kupandisha hadhi hii Zahanati ya Ng’haya iweze kuwa Kituo cha Afya, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Alfred James Kimea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. HAMISI S. TALETALE aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Ngerengere?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mwaka 2021 Kata ya Mgombezi kwenye Jimbo langu la Korogwe Mjini walipatiwa shilingi milioni 250 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya. Baadhi ya majengo yalijengwa lakini mpaka sasa tunapoongea, shilingi milioni 250 za ziada hazijafika kwenye ile Kata ya Mgombezi, zaidi ya miaka miwili. Nataka kumuuliza Mheshimiwa Waziri, je, ni lini Serikali itatuletea shilingi milioni 250 zilizobaki ili kwenda kumalizia Kituo cha Afya cha Mgombezi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Kimea, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba kuna Vituo vya Afya katika Majimbo mengi hapa nchini ambavyo vilipewa shilingi milioni 250 mwaka wa fedha 2021/2022 na majengo ya shilingi milioni 250 yamekamilika, yameanza huduma za awali za OPD kwenye baadhi ya Vituo lakini kuna majengo yanayohitajika kwa ajili ya kukamilisha ngazi ya Kituo cha Afya. Naomba kumhakikishie Mheshimiwa Kimea kwamba tunatambua Vituo vyote ambavyo vimepata shilingi milioni 250 na bado shilingi milioni 250.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametupa kibali kuweka kwenye bajeti ambayo tunaanza kuipanga hivi karibuni, kuhakikisha Vituo vyote vya Afya vilivyopata shilingi 250 na bado shilingi milioni 250, vinapelekewa mwaka ujao wa fedha ili vituo vile viweze kukamilika, ahsante. (Makofi)

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMISI S. TALETALE aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Ngerengere?

Supplementary Question 6

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana; Mji wa Mafinga ni Mji ambao unakuwa kwa kasi kubwa sana. Kuna Kituo cha Afya cha Upendo ambacho wananchi walishaanza kukijenga. Ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo hicho?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Grace Tendega, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, namhakikishia tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inathamini nguvu za wananchi na tutakwenda kufanya tathmini ili tuone namna gani tunachangia kukamilisha Kituo cha Afya cha Upendo. Ahsante. (Makofi)

Name

Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMISI S. TALETALE aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Ngerengere?

Supplementary Question 7

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante; nimekuwa nikiuliza kila siku kuhusu Zahanati ya Town Clinic ambayo ina msongamano mkubwa wa watu kufikia kuzalisha wanawake 200 kwa mwezi, na Mheshimiwa Naibu Waziri amekuwa akinijibu Mkurugenzi alete michoro; je, Mheshimiwa Naibu Waziri ana mkakati gani wa kumwandikia sasa Mkurugenzi kwa maandishi ili aweze kuleta huo mchoro na Zahanati ya Town Clinic iwe Kituo cha Afya? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Munde, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza sana Mheshimiwa Munde, alikuja, tulimwita Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora, tulikaa naye mimi, Mheshimiwa Mbunge na Mkurugenzi, tukampa mkakati wa kwenda kuandaa michoro hiyo aweze kuiwasilisha. Si kwa barua, bali tulimwita na tukakutana. Kwa hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari tuna taarifa zote za hatua ambazo zinaendelea kwa ajili ya kupandisha hadhi Zahanati ile ya Town kuwa Kituo cha Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasisitiza kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora kuleta michoro ile haraka iwezekanavyo Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tuweze kuona namna gani tunaanza ujenzi wa Kituo cha Afya cha Town. Ahsante. (Makofi)

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. HAMISI S. TALETALE aliuliza: - Je, lini Serikali itakamilisha Ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Ngerengere?

Supplementary Question 8

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, namuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, Zahanati ya Kijiji cha Nkome nimekizungumza humu mara tatu; inazalisha shule kila mwezi, maana yake watoto zaidi ya 550; na kwa sasa tumeenda zaidi tunafika karibia 600 kwa mwezi; mliniahidi kuongeza uwezo wa ile zahanati ili iwe Kituo cha Afya, tathmini zote zimefanyika na mwezi huu wametoka kukagua tena, na fedha ipo shilingi milioni 500; lini hiyo fedha itakuja? Lini Mheshimiwa Naibu Waziri atakuja ili akaangalie huo uzalishaji wa hiyo zahanati?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Musukuma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu kwamba Zahanati hii ya Nkome aliyoitaja Mheshimiwa Mbunge, kwa kweli imezidiwa kwa idadi kubwa ya wananchi katika eneo lile na Serikali ishaweka mpango wa kupandisha hadhi kuwa Kituo cha Afya. Mwenyewe amesema wiki moja, mbili zilizopita wataalamu kutoka Ofisi ya Rais, TAMISEMI, walifika kufanya tathmini kwa ajili ya kutumia fedha za Benki ya Dunia kujenga Kituo cha Afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hili liko on track na tutahakikisha tunajenga Kituo cha Afya hiki mapema iwezekanavyo. Ahsante. (Makofi)