Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:- Je, nini mkakati wa Serikali kuboresha miundombinu ya barabara na kuinua maendeleo mikoa ya Lindi na Mtwara?

Supplementary Question 1

MHE. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Spika, ahsante, Lindi na Mtwara tunashukuru kwa jitihada za Dkt. Samia Suluhu Hassan kutuletea maendeleo na ndiyo maana akaridhia kusaini kwa Mkataba huo wa EPC + F hapo Juni mwaka huu.

Mheshimiwa Spika, kusaini mkataba ni jambo moja na kuanza ujenzi ni jambo lingine; je, ni lini sasa Mkandarasi ataanza kazi ya Ujenzi Masasi – Nachingwea – Liwale? (Makofi)

Swali la pili; je, ni lini sasa barabara ya Nachingwea kwenda Kilimarondo itajengwa kwa kiwango cha lami? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Tecla Ungele, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara ya Masasi – Nachingwea hadi Liwale kilometa 175 kama nilivyosema katika jibu la msingi inatekelezwa kwa utaratibu wa EPC + F na iko kwenye hatua kama ambavyo barabara zote zipo.
Mheshimiwa Spika, sasa hivi Waziri alitolea maelezo wako wanapitia usanifu wale Wakandarasi ambao wamepewa hizo barabara na tunategemea Januari wakandarasi watakuwa wako site baada ya kukamilisha zile taratibu zao za kupitia ule usanifu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba zoezi hilo linaendelea na barabara hizo zitaanza kujengwa. Kinachoendelea tu hapa ni kwamba ni utaratibu ambao ni mpya kwetu sisi lakini wanatakiwa wale ambao wamepewa hizo kazi nao lazima wapitie usanifu na wajiridhishe.

Mheshimiwa Spika, swali la pili kuhusu barabara aliyoitaja hiyo kwenda Kilimarondo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, barabara hiyo baada ya kufanyiwa usanifu bajeti ikiruhusu basi tutaanza kuijenga kwa kiwango cha lami, kwa sababu lengo la Serikali ni kuzijenga barabara hizi kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:- Je, nini mkakati wa Serikali kuboresha miundombinu ya barabara na kuinua maendeleo mikoa ya Lindi na Mtwara?

Supplementary Question 2

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, nami niulize swali moja la nyongeza.

Barabara ya kutoka Mtama – Kitangali hadi Amkeni – Newala, yenye urefu wa kilometa 74 ipo kwenye zoezi la Upembuzi Yakinifu, ni lini zoezi hili litakamilika ili barabara hii ijengwe kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, suala la upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ni suala ambalo linategemeana na aina ya barabara yenyewe. Kwa hiyo, mandhari tumeanza tunategemea kwamba, usanifu kwa urefu wa kilometa hizi 74 haziwezi kuzidi mwaka lakini namshawishi Mheshimiwa Mbunge kwamba, tunategemea ndani ya mwaka mmoja baada ya kuanza usanifu utakuwa umekamilika wa hii barabara, ahsante. (Makofi)

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:- Je, nini mkakati wa Serikali kuboresha miundombinu ya barabara na kuinua maendeleo mikoa ya Lindi na Mtwara?

Supplementary Question 3

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana.

Kwa kuwa ujenzi wa barabara ya Ifakara – Kidatu unakaribia kukamilika na kwa kuwa kumekuwa na ajali nyingi sana katika eneo la Mang’ula Kona kutokana na eneo la hifadhi kuingia barabarani, na kwa kuwa, kupitia Waziri wa Maliasili, Mheshimiwa Rais aliliridhia akatupatia eneo la hifadhi ili tuweze kupasafisha kusaidia magari kuonana, na kwa kuwa Waziri wa Ujenzialifika katika eneo husika akaahisi kwamba eneo hilo litasafishwa.

Mheshimiwa Spika, swali langu ni lini ahadi hiyo ya kusafisha Mang’ula Kona itaanza kutekelezwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, barabara anayoitaja hii ya Kidatu kwenda Ifakara ni barabara kuu na bahati nzuri kwenye hiyo kona ya Mang’ula Kona mimi nimefika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, tayari Wizara ilishaelekeza baada ya maombi ya Mheshimiwa Mbunge lakini pia na Waziri kutoa maelekezo kwa Meneja wa Mkoa wa Morogoro aende akaangalie namna ambavyo watafanya kupunguza ile kona. Kwa sababu kupunguzwa kwa hiyo kona haikuwa sehemu ya usanifu wa hiyo Barabara, kwa hiyo lazima waende wakafanye usanifu mpya wa eneo na kuona gharama ya kufanya hiyo kazi. Ahsante. (Makofi)

Name

Amandus Julius Chinguile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:- Je, nini mkakati wa Serikali kuboresha miundombinu ya barabara na kuinua maendeleo mikoa ya Lindi na Mtwara?

Supplementary Question 4

MHE. AMANDUS J. CHINGUILE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara ya Nanganga – Nachingwea kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, katika jibu la msingi nilisema kwamba barabara ya Nachingwea – Nanganga ipo katika hatua za mwisho na tunategemea katika zile barabara ambazo tunategemea kuzisainia kwa pamoja hiyo barabara ni mojawapo ya Nanganga – Nachingwea. Ahsante.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:- Je, nini mkakati wa Serikali kuboresha miundombinu ya barabara na kuinua maendeleo mikoa ya Lindi na Mtwara?

Supplementary Question 5

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; nini mkakati wa Serikali sasa kujenga kwa kiwango cha lami Barabara ya Mtwara – Pachani na Nalasi – Tunduru ambayo upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ulishafanyika na ipo kwenye Ilani, na ndiyo tunayoisubiri barabara hii inayotegemewa na vijiji vingi zaidi ya 50 katika eneo hilo la Namtumbo na Tunduru? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tunatambua umuhimu wa hii barabara ya Mtwara – Pachani hadi Nalasi – Tunduru ambayo ina urefu wa kilometa 300. Wakati Serikali inaendelea kutafuta fedha kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami, tulichoshauri na tunachokifanya sasa hivi katika barabara hiyo ni kwanza kuhimarisha madaraja ambayo ina madaraja mengi ya mito.

Pili, ni kujenga kwa kiwango cha zege ama lami maeneo yote ambayo huwa yanakwamisha usafiri katika hiyo barabara ili wananchi waendelee kupita kipindi chote wakati Serikali inatafuta fedha ya kuijenga barabara yote kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:- Je, nini mkakati wa Serikali kuboresha miundombinu ya barabara na kuinua maendeleo mikoa ya Lindi na Mtwara?

Supplementary Question 6

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Ni takribani miezi mitano imepita sasa hivi tangu mikataba ya ujenzi wa barabara ya Mnivata – Nanyamba – Newala hadi Masasi imesainiwa.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, kwanza mimi niseme kama kuna barabara ambayo wenzetu hawatakiwi kuwa na wasiwasi ni hiyo barabara ya Mnivata – Newala kwenda Masasi.

Mheshimiwa Spika, taratibu ambazo zinaendelea sasa hivi ni taratibu za maandalizi kwa maana ya mobilization na wenzetu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika ndiyo ambao tunasaidiana nao kuijenga hiyo hiyo barabara.

Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni taratibu tu zinaendelea za kimkataba lakini muda siyo mrefu watawaona sasa wakiwa wako site katika hivyo vipande viwili, ambavyo barabara hiyo imegawanywa katika vipande viwili, ahsante. (Makofi)

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:- Je, nini mkakati wa Serikali kuboresha miundombinu ya barabara na kuinua maendeleo mikoa ya Lindi na Mtwara?

Supplementary Question 7

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Je, Serikali ina mpango gani wa kupanua au kurekebisha barabara ya Kilwa kipande cha Mbagala Zakheim kutoka Zakheim mpaka Mzinga, kwa sababu kipande hicho kimekuwa na changamoto, unatoka huko lakini unafika pale magari hayaendi, kunakuwa na msongamano mkubwa sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, nimshukuru Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Spika, barabara zote za Dar es Salaam kulingana na ukuaji wa mji zinafanyiwa study kuona barabara zote ambazo zina changamoto zinafanyiwa marekebisho, ikiwa ni pamoja na kuongeza upana wa barabara hizo, na siyo za Dar es Salaam tu hata barabara za Mikoani ambazo zilijengwa zamani nyingi zilikuwa na upana mdogo.

Kwa hiyo, sasa hivi hizo barabara zinapitiwa upya ikiwa ni pamoja na barabara aliyoitaja ili kuhakikisha kwamba sasa tunakwenda kwa kipindi cha sasa kuzipanua hizo barabara, ahsante.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:- Je, nini mkakati wa Serikali kuboresha miundombinu ya barabara na kuinua maendeleo mikoa ya Lindi na Mtwara?

Supplementary Question 8

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa kuwa wananchi wa Haydom wameshawapa eneo la kujenga majengo ya mkandarasi ili aanze kazi na wewe ulikuja kusaini ule mkataba.

Je, ni lini anakuja kujenga yale majengo ili barabara ianze kujengwa ya Haydom – Labay?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, bahati nzuri hiyo barabara mkandarasi ambaye anajenga kipande cha kwanza ndiyo atakaejenga kipande cha pili. Kazi anayofanya sasa hivi ni kufanya usanifu, kwa sababu barabara hiyo inayojengwa ni sanifu inajengwa na atakapokuwa amekamilisha nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge ndipo atakapoanza sasa kujenga hiyo kambi yake eneo ambalo, tunamshukuru sana Mheshimiwa Mbunge na Wananchi wa Mbulu kwa kulitoa hilo eneo la ujenzi bure kabisa, ahsante. (Makofi)

Name

Bahati Keneth Ndingo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:- Je, nini mkakati wa Serikali kuboresha miundombinu ya barabara na kuinua maendeleo mikoa ya Lindi na Mtwara?

Supplementary Question 9

MHE. BAHATI K. NDINGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Je, ni lini Serikali sasa mtaanza ujenzi wa barabara muhimu ya kutoka Lujewa – Madibila mpaka Mafinga? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Bahati Ndingo, Mbunge wa Mbarali, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli hiyo barabara ni muhimu na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, Mheshimiwa Rais akiwa ziara katika Mkoa wa Iringa alitoa maelekezo hiyo barabara ianze kujengwa kwa kiwango cha lami kilomita 25. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, sasa hivi tuko kwenye hatua za manunuzi kutekeleza hiyo ahadi na maelekezo ya Mheshimiwa Rais, ahsante. (Makofi)

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. TECLA M. UNGELE aliuliza:- Je, nini mkakati wa Serikali kuboresha miundombinu ya barabara na kuinua maendeleo mikoa ya Lindi na Mtwara?

Supplementary Question 10

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, napenda kujua tunao ujenzi wa kilomita moja ya lami Mji wa Karumwa, takribani miezi 24 na tuta lile limenyanyuliwa zaidi ya mita moja, mvua zinaendelea kunyesha na maji yanaingia kwenye nyumba za watu imekuwa ni kero kubwa. Miezi 24 kilomita moja haijakamilika, nataka kauli ya Serikali ni lini kilomita moja hiyo itakamilika? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ninakiri kwamba, Mheshimiwa Mbunge amekuja ofisini kufuatilia hili suala, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Mji wa Karumwa, nimeongea na Meneja wa Mkoa wa Geita kwamba hiyo barabara itakamilishwa. Sasa hivi kilichokwamisha tu ni kwamba mvua inanyesha na baada ya hapo kwa sababu ipo chini ya Meneja wa Mkoa wa Geita, wataikamilisha hiyo barabara ikiwa ni pamoja na kutengeneza hiyo mifereji ambayo inaleta adha kwa wananchi wa Karumwa, ahsante. (Makofi)