Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza:- Je, lini barabara ya Makofia - Mlandizi itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. MUHARAMI S. MKENGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; barabara hii iliyofanyiwa tathmini, je, ni lini wananchi wake watalipwa fidia zao?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; miezi miwili iliyopita, nilihudhuria utiaji saini Mkataba wa BRT, awamu ya tatu ambao umejumuisha ujenzi wa kipande kilichobakia cha Barabara kutoka Tamko kuja Mapinga Bagamoyo. Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa kipande hiki cha barabara?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli Barabara hii ya Makofia - Mlandizi tulishakamisha usanifu na tulifanya tathmini kwa maana kupata gharama ya fidia mwaka 2018, lakini hatukufika mpaka mwisho. Kwa hiyo zoezi hilo limerudiwa na Mheshimiwa Mbunge atakuwa shahidi kwamba tayari watu wameshapita na hatua ambayo tunayo sasa hivi, ni kupata uhakiki ili jedwali la malipo liende Hazina kwa ajili ya kuandaa malipo. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, zoezi hilo linaendelea na watalipwa baada ya kuhakikiwa na kuridhika kwamba hiki ndio kiasi ambacho wanatakiwa walipwe hao ambao wataipisha hiyo barabara.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala lake la pili ni kweli Barabara ya Tamko – Mapinga tulishatia saini na nakiri kushiriki. Mheshimiwa Mbunge, atakubaliana nami kwamba, barabara hii haikuwa na hifadhi ya kama barabara. Sasa Mkandarasi kuna mambo ya kimkataba ambayo anakamilisha na sisi kama Serikali tuko tunamfuatilia kuona anakamilisha zile taratibu ili aanze kuijenga na tuko kwenye hatua za mwisho, barabara hiyo sasa itaanza kujengwa kwa sababu tayari tulishawekeana saini, ahsante.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza:- Je, lini barabara ya Makofia - Mlandizi itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Barabara ya kutoka Tarime Mjini mpaka Mugumu ni barabara muhimu sana kwa uchumi wa Tanzania na Mkoa wa Mara kwa ujumla kwa sababu inaunganisha kwenda kwenye utalii na ilitengewa fedha kuanzia mwaka 2021/2022, takribani bilioni 35, lakini Serikali imekuwa ikipeleka fedha kwa kusuasua mpaka sasa hivi imepeleka bilioni tano tu.

Je, ni lini, Serikali itahakikisha kwamba inampelekea mkandarasi fedha kwa wakati ili aweze kukamilisha ile barabara kwa wakati?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge Matiko, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli barabara hii ni muhimu na hii barabara imegawanywa katika lot mbili, hatupeleki hela yote, tunalipa kulingana na mahitaji ya mkandarasi. Kwa hiyo akishaleta hati ya malipo ndipo tunapomlipa. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Serikali itaendelea kulipa kadri hati zinavyokuja kuhakikisha kwamba barabara yote ya Tarime - Mugumu inakamilika, ahsante.

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza:- Je, lini barabara ya Makofia - Mlandizi itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Spika, ahsante, je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa kilometa 54 za lami kwa wananchi wa Ushetu ambapo Serikali iliahidi yenyewe, lakini hakuna dalili yoyote inayoendelea?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ni kweli kwamba Serikali iliahidi kuijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami. Barabara zote zinazofanana na hiyo ya Ushetu, mpango wa Serikali ni kuzijenga kwa kiwango cha lami, lakini utakubaliana nami kwamba hapa ndio tunapopitisha bajeti, kwa hiyo bajeti ndio inayoamua. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba sisi tutaendelea kuweka kwenye mipango ile ahadi ya Serikali ambayo tuliahidi iweze kutimia kuijenga hiyo barabara kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza:- Je, lini barabara ya Makofia - Mlandizi itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Je, ni lini Barabara ya Mgololo - Mafinga itajengwa kwa kiwango cha lami kwa sababu hii barabara ni kitega uchumi katika Jimbo la Mufindi Kusini?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, barabara ya Mgololo – Mafinga ni kati ya barabara sita ama saba ambazo tunazijenga kwa utaratibu wa EPC + F na nimelijibu mara kadhaa kwamba tayari kazi zinaendelea za awali kwa wakandarasi ambao wamepatikana kuijenga hii barabara. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii ni kati ya barabara ambazo zinatekelezwa kwa Mpango wa EPC + F na tutahakikisha kwamba hiyo barabara inajengwa kama Serikali ilivyoahidi, ahsante. (Makofi)

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza:- Je, lini barabara ya Makofia - Mlandizi itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi.

Kwa kuwa, barabara ya Utegi – Shirati mpaka Kihongwe Upembuzi yakinifu na usanifu wa kina umekwishakamilika na barabara hii tayari imetengewa fedha. Ninataka kujua kwa Mheshimiwa Waziri, ni lini sasa barabara hii itatangazwa na kuanza ujenzi wa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Chege, swali la nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli bahati nzuri barabara hii nimetembelea tukiwa na Mheshimiwa Mbunge na aliahidiwa kwamba barabara hii itaanza kujengwa. Barabara hii ipo kwenye mpango wa kuanza kuijenga kwa kipindi cha bajeti hii ya 2023/2024. Kwa hiyo, taratibu za kuandaa tender document zinaendelea, basi zikikamilika barabara hii itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami. (Makofi)

Name

Dr. Florence George Samizi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza:- Je, lini barabara ya Makofia - Mlandizi itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. FLORENCE G. SAMIZI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipatia nafasi. Ujenzi wa barabara ya kutoka Kabingo hadi Kibaoni kilometa 25 kwa kiwango cha lami unasuasua sana.

Je, ni lini Serikali itakwamua ujenzi wa barabara hii?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Muhambwe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, barabara hii inayoisema ni Kibondo link, barabara ambayo inajengwa kwa kiwango cha lami. Nimeitembelea hiyo barabara kuangalia changamoto zilizopo, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali imeshaona changamoto zilizokuwepo za kiutendaji kwa Mkandarasi na tuna hakika baada ya kukaa nae barabara hii sasa itaanza kwenda kasi ili tukamilishe zile kilometa 25. Ahsante.

Name

Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza:- Je, lini barabara ya Makofia - Mlandizi itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Spika, ahsante.

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara ya MR – Pawaga kwa kiwango cha lami kuanzia MR – Iringa Mjini?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge atakuwa shahidi kwamba katika bajeti ya mwaka huu kuna kiasi kimetengwa kwa ajili ya kuanza kilomita kama sikosei ni kilometa kama 20 kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, kadri tutakavyokwenda taratibu zikishakamilika barabara hizo zitatangazwa kwa ajili ya kuanza kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. MUHARAMI S. MKENGE aliuliza:- Je, lini barabara ya Makofia - Mlandizi itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Ningependa kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri; barabara ya Nkome – Nzela – Geita yenye urefu wa kilometa 20 mwaka wa tatu Mkandarasi amepatikana tunasubiri kusaini.

Je, huna mafuta nikuwekee ili tuende tukasaini kesho? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan haiwezi kukosa mafuta ya kwenda kusaini, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tunatambua umuhimu wa hiyo barabara ni suala la muda tu na ipo kwenye mipango, muda ukifika nina hakika barabara hii tutaisaini kwa sababu tayari imeishatengewa fedha na kila kitu kimekamilika. Kwa hiyo, tunachosubiri tu ni suala la taratibu zikamilike ili Mkandarasi aweze kuanza kazi hiyo ya kujenga kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)