Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka lami walau kilometa 10 za barabara za ndani za Mji wa Katesh ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 1

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Swali kwanza, tarehe 29 Septemba, 2022, Mheshimiwa Waziri wa TAMISEMI alitutembelea na kati ya miradi aliyokagua, alikagua ujenzi wa barabara za lami Mji wa Katesh aliahidi kwa mwaka ule wa fedha 2022/2023 ameshaongea na Mheshimiwa Rais angeongeza fedha kwa ajili ya kilometa moja na hizo fedha hazikuja kwa mwaka huo wa fedha.

Je, Serikali sasa iko tayari kwa mwaka huu wa fedha 2023/2024 kutupa fedha za kilometa moja?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; mradi huu kidogo hauendi kwa kasi ili kufikia kilometa 10; je, Serikali ina mkakati gani mahususi ili kujenga barabara za lami katika Mji wa Katesh? Ahsante sana.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Samwel Hhayuma. Swali la kwanza na la pili yote nitayajibu kwa pamoja. Ahadi hizi za viongozi ni lengo la Serikali kuzikamilisha zote kwa wakati na kama ambavyo Mheshimiwa Mbunge anafahamu tayari asilimia 30 ya ahadi hii ya barabara ya kilometa 10 imeshafikiwa mpaka hivi tunavyozungumza.

Mheshimiwa Spika, tutaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kukamilisha ahadi hiyo ya kilometa 10 iliyotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ahadi pia iliyotolewa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, tutahakikisha fedha inapopatikana ahadi hizi zinaenda kutekelezwa kwa ujenzi wa barabara hizi za lami.

Name

Ghati Zephania Chomete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka lami walau kilometa 10 za barabara za ndani za Mji wa Katesh ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 2

MHE. GHATI Z. CHOMETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Serikali iliahidi ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami, kilometa tano katika Halmashauri ya Mji wa Tarime. Je, ni lini Serikali itapeleka pesa ili mradi huo uanze?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, ili barabara hiyo ya kilometa tano ambayo imeahidiwa na Serikali Tarime iweze kuanza kujengwa, tutakaa na Mheshimiwa Mbunge kuweza kuona ni nini kinaweza kikafanyika na fedha ikipatikana basi ahadi hii iweze kutekelezwa mara moja.

Name

Asia Abdulkarim Halamga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka lami walau kilometa 10 za barabara za ndani za Mji wa Katesh ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 3


MHE. ASIA A. HALAMGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itakamilisha ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa kilometa tano za lami Babati Mjini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, ni lengo la Serikali kuhakikisha ahadi zote za Viongozi wetu Wakuu, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Naibu Waziri Mkuu zinatekelezwa kwa wakati na tutaendelea kuratibu kupitia Ofisi ya TARURA, Mkoa wa Manyara, Ofisi ya TARURA, Wilaya ya Babati, kuona ni kiasi gani kinahitajika ili tuweze kutafuta fedha kuweza kutekeleza ahadi hiyo.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka lami walau kilometa 10 za barabara za ndani za Mji wa Katesh ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 4

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi. Pamoja na kwamba Mheshimiwa Rais alipokuja Liwale ametuahidi kutujengea barabara ya Nangurukuru - Liwale, vilevile alituahidi kutujengea barabara kilometa mbili kwa ajili ya Liwale Mjini. Je, ahadi hiyo itatekelezwa lini?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kwa kuwa ziara ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mkoani Lindi, ilifanyika muda si mrefu sana kutoka sasa. Tunaendelea kuratibu ahadi zote ambazo zimetolewa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kutafuta fedha kwa ajili ya kupeleka mara moja katika maeneo mbalimbali ambapo ahadi hizi zimetoka ikiwemo kule Liwale kwa Mheshimiwa Kuchauka.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka lami walau kilometa 10 za barabara za ndani za Mji wa Katesh ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Pamoja na jitihada za Serikali kujenga barabara za lami kwenye miji yetu, kumekuwa na shida kubwa ya ubora wa wakandarasi wanaotekeleza miradi hii hasa maeneo ya pembezoni kama ilivyo Ukerewe. Je, ni nini mkakati wa Serikali kushughulikia changamoto hii? Nashukuru.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mkundi. Ni mkakati wa Serikali sasa kupitia Taasisi yetu ya TARURA kuhakikisha tunanunua mitambo na kupeleka maeneo ya pembezoni ikiwemo kule Ukerewe kwa ajili ya kuweza kutengeneza barabara hizi mara kwa mara. Changamoto ambayo inapatikana kwenye maeneo kama Ukerewe, maeneo kama Mafia ni wakandarasi kuweza kupeleka mitambo katika maeneo yale na tayari Serikali imeliona hili na itanunua mitambo yake yenyewe kwa ajili ya kupeleka kwenye maeneo hayo.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka lami walau kilometa 10 za barabara za ndani za Mji wa Katesh ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 6

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kuboresha barabara kwa kiwango cha lami katika Kata za Mikumi na Ruaha ambazo ni Kata za kimkakati?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, Serikali itatekeleza ahadi hii ya kuboresha Barabara za Mikumi na Ruaha kwa kiwango cha lami kadri ya upatikanaji wa fedha. Nitakaa na Mheshimiwa Londo kuona ni namna gani ambavyo tunaweza tutaratibu hili kupitia Ofisi ya Meneja wa TARURA Wilaya ya Kilosa na Meneja wa TARURA Mkoa wa Morogoro ili tuweze kutekeleza ahadi hiyo.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka lami walau kilometa 10 za barabara za ndani za Mji wa Katesh ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 7

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Spika, ahsante, je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami Barabara ya kutoka Vwawa – London - Msiya hadi Isarawe, ambayo ni ahadi ya Serikali kwa muda mrefu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, tutaanza kutekeleza ahadi hii kadri ya upatikanaji wa fedha, lakini tutakaa tena na Mheshimiwa Mbunge, kuweza kuona ni namna gani tutaratibu hili kupitia Mameneja wetu wa mikoa na hasa Meneja wa Mkoa wa Songwe kuona tunaanzaje kutekeleza ahadi hii ya Serikali.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka lami walau kilometa 10 za barabara za ndani za Mji wa Katesh ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais?

Supplementary Question 8

MHE. DKT. ANGELINE S. L. MABULA: Mheshimiwa Spika, ningependa kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, wamejenga barabara ya kilometa 2.5 ya breweries kwa kiwango cha lami kwa kilometa 1.7 na kimebaki kipande kidogo cha mita 750. Je, ni lini watakamilisha ujenzi huo kwa maana sasa ujenzi umesimama?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nitakaa na Mheshimiwa Mabula kuona ni namna gani ambavyo Serikali inaweza ikaliratibu hili na kukamilisha kipande hiki cha barabara ambacho kimesalia kwa kuwasiliana na Meneja wa TARURA, Mkoa wa Mwanza na Meneja wa TARURA, Wilaya ya Ilemela kuona ni kiasi gani kinahitajika ili kuweza kukamilisha ahadi hiyo.