Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE K.n.y MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha stakabadhi za mashine za EFD ili zisifutike baada ya muda mfupi?

Supplementary Question 1

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Wananchi na wafanyabiashara wamekuwa na mwamko mdogo wa kudai risiti.

Je, Serikali ina mpango gani wa kutoa elimu ili wananchi na wafanyabiashara wawe wanadai risiti?

Swali la pili; Wafanyabiashara wengi hawana mashine hizi za EFD pia zilizopo nyingi ni mbovu, unapokwenda madukani unakuta hawana mashine.

Je, Serikali sasa ina mpango gani wa kununua mashine kusambaza kwa wafanyabiashara wote ili kuongeza mapato? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Innocent Bilakwate kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba wananchi wengi wana mwamko mdogo wa kudai risiti na baadhi ya wafanyabiashara wanakuwa wazito kutoa risiti. Mikakati ya Serikali ni kutoa elimu, kuendelea kuhamasisha na nitoe wito kwa TRA kuendelea kutoa elimu kupitia vyombo vya habari vyote ndani ya nchi ikiwezekana hata nje ya nchi, vile vyombo ambavyo huwa vinasikilizwa sana. Pia ninawaomba Wabunge wenzangu kutoa taaluma hiyo kwa wananchi wetu kudai risiti baada ya kununua bidhaa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, tunaliangalia kwa kweli kutoa mashine za EFD tunaweza tukatoa hivyo hapo baadaye, kwa mwaka huu wa fedha hatutaweza kutoa lakini tutalingalia baadaye ikionekana ipo haja na fedha ipo ya kutosha basi tutatoa mashine hizo kwa wananchi wetu.

Name

Bernadeta Kasabago Mushashu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE K.n.y MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha stakabadhi za mashine za EFD ili zisifutike baada ya muda mfupi?

Supplementary Question 2

MHE. BENARDETA K. MUSHASHU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana naomba kuuliza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mashine za EFD ni za gharama sana lakini mtu akibadilisha biashara kwa maana ya TIN analazimika kununua mashine mpya. Kwa nini Serikali isiweke utaratibu wa badala ya kununua mashine mpya wakaondoa ile program akaendelea kutumia mashine ile ile kwa kubadilisha tu program? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mbunge huo ni shauri tunauchukua na tunaufanyia kazi. (Makofi)