Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaharakisha na kumaliza upembuzi yakinifu kwa ajili ya mradi wa maji katika vijiji 46 Wilaya ya Rungwe?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nina maswali mawili ya nyongeza:-
Swali la kwanza, tunashukuru kwa Shilingi Bilioni 1.1 ambayo Wilaya ya Rungwe ilipata kati ya Shilingi Bilioni Nne ambayo ilikuwa ni bajeti. Sasa Serikali haioni umuhimu wa kuhakikisha angalau tunapata nusu ya bajeti ambayo ilikuwa iliombwa ili kuwasaidia watendaji kufanyakazi yao vizuri?

Swali la pili, kumekuwa na ahadi za viongozi mbalimbali wanaokuja kwenye Wilaya zetu na kuahidi wananchi kupata maji kwa wakati. Sasa Serikali haioni umuhimu wa miradi ile inayoahidiwa na viongozi iweze kufanyika haraka na watu waweze kupata maji kama ambavyo watu walipata ahadi hasa katika hivyo vijiji 155 vya Rungwe?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kupokea kwanza shukrani na anayeshukuru anaomba tena ndiyo swali lako la pili linapoelekea. Ni kweli tumefika Wilaya ya Rungwe na tumeahidi na tunakwenda kutekeleza ni suala la muda tu Mheshimiwa Mbunge naomba utupe nafasi tufanye kazi.

Name

Juliana Daniel Shonza

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaharakisha na kumaliza upembuzi yakinifu kwa ajili ya mradi wa maji katika vijiji 46 Wilaya ya Rungwe?

Supplementary Question 2

MHE. JULIANA D. SHONZA: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Naomba kufahamu ni lini Serikali itaanza Upembuzi yakinifu katika mradi wa maji katika Kijiji cha Lukululu uliopo katika Jimbo la Vwawa? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Juliana Shonza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, upembezi yakinifu tunatarajia kuanza mwaka ujao wa fedha na kadri fedha itakapopatikana kasi itakuwa ni kubwa, lengo ni kuwafikia wananchi wote ili waweze kupata maji safi na salama bombani.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaharakisha na kumaliza upembuzi yakinifu kwa ajili ya mradi wa maji katika vijiji 46 Wilaya ya Rungwe?

Supplementary Question 3

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kuna vijiji vya Machiga na Chandama kuna mradi wa maji ambao tayari Kandarasi yake ilitangazwa na Mzabuni akapewa lakini mpaka leo hayupo site. Nini kauli ya Serikali kuhusu Mzabuni huyu kuwepo site? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Monni, Mbunge wa Chemba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wakandarasi wote ambao tumesaini nao mikataba wanafahamu sheria na taratibu na tayari Mheshimiwa Waziri ameshaongea mara nyingi, hatutakawa na mzaha na wale Wakandarasi ambao wanachelewa kufika site hivyo Mheshimiwa Mbunge hili nimelipokea na tutalifanyia kazi kwa karibu.