Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha kukamilisha ujenzi wa majengo ya zahanati Kijiji cha Masagalu Mission, Kilindi?

Supplementary Question 1

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi kwa mwaka wa fedha 2024/2025 inatarajia kutenga au itatenga shilingi milioni 100 kwa ajili ya kumalizia Kitua cha Afya cha Kilindi asilia na shilingi milioni 40 kwa ajili ya hospitali ya wilaya.

Mheshimiwa Spika, sasa, nataka tu nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri, hizi taarifa za kwamba tumetenga shilingi milioni 100 kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa Zahanati ya Masagalu amezipata wapi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Serikali imekuwa na utaratibu wa kuhamasisha wananchi kujenga majengo na wao kutenga milioni 50. Je, Serikali haioni iko sababu ya kutenga milioni 50 na kuwapelekea wananchi wa Masagalu na kumalizia majengo haya? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwa namna ambavyo ameendelea kuweka kipaumbele katika Baraza la Madiwani ili kuhakikisha kwamba wanatenga fedha za mapato ya ndani kwa ajili ya ukamilishaji wa majengo ya Zahanati na Vituo vya Afya.

Mheshimiwa Spika, Serikali ni moja. Mkurugenzi wa halmashauri, Katibu tawala wa mkoa wana wajibu wa kupokea maelekezo kutoka katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI, hasa tunapoona vigezo vya ukamilishaji wa majengo hayo vinakidhi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwa mujibu wa jengo hili ambalo lina zaidi ya miaka mitano halijakamilika, tumemwelekeza Mkurugenzi na amechukua hiyo commitment kwamba, atenge milioni 100 kama kipaumbele katika Mwaka wa Fedha 2024/2025 kukamilisha boma hili ambalo lina muda mrefu na baadaye tutaendelea na maboma mengine.

Mheshimiwa Spika, ni kweli Serikali ina utaratibu wa kutenga milioni 50 kwa ajili ya kukamilisha maboma na Halmashauri hii ya Kilindi imekuwa ikipata fedha hizo. Pia, nimhakikishie tu kwamba tutaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kuhakikisha tunachangia ukamilishaji wa zahanati hiyo. Ahsante.

Name

Mwantumu Mzamili Zodo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha kukamilisha ujenzi wa majengo ya zahanati Kijiji cha Masagalu Mission, Kilindi?

Supplementary Question 2

MHE. MWANTUMU M. ZODO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, toka Desemba, 2022 Mheshimiwa Rais amepeleka milioni hamsini hamsini kwenye maboma ya zahanati. Mpaka leo hayajakamilika ikiwepo Zahanati ya Mpasilasi kwenye Jimbo la Korogwe vijijini. Je, ni upi mkakati wa Serikali sasa kuhakikisha wanakwenda kusimamia ili maboma yale yakamilike?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, Serikali inapeleka milioni 50 kwa ajili ya kukamilisha maboma kwenye maeneo ya halmashauri zetu ambako kuna viongozi. Kuna wakuu wa idara, Wakurugenzi, wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa. Sasa, ni wajibu wao kuhakikisha kwamba, fedha hizi ambazo Mheshimiwa Rais anazipeleka zinafanya kazi kwa wakati na kukamilisha ujenzi kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, nittumie fursa hii kuwakumbusha Wahesjhimiwa wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, Makatibu tawala wa mikoa pamoja na wakurugenzi kwamba, ni wajibu wao na sisi tutafuatilia kuona maboma haya yanakamilika kwa wakati na kuanza kutoa huduma kwa wananchi. Ahsante.

Name

Vedastus Mathayo Manyinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Mjini

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha kukamilisha ujenzi wa majengo ya zahanati Kijiji cha Masagalu Mission, Kilindi?

Supplementary Question 3

MHE. VEDASTUS M. MATHAYO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya swali dogo la nyongeza. Kila mwaka Serikali imekuwa ikiahidi kutoa fedha kwa ajili ya kumalizia kituo cha afya cha Bweri. Sasa ni lini tutapata hizo fedha ili kile kituo kiweze kukamilika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Bweri tayari kimeingizwa kwenye orodha ya vituo vya kimkakati ambavyo vinatafutiwa fedha kwa ajili ya ukamilishaji. Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mbunge awe mvumilivu, aamini kwamba Serikali ipo kazini na mara fedha itakapopatikana tutahakikisha kwamba tunaipeleka kwa ajili ya kukamilisha Kituo cha Afya cha Bweri. Ahsante.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha kukamilisha ujenzi wa majengo ya zahanati Kijiji cha Masagalu Mission, Kilindi?

Supplementary Question 4

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Je, ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi wa nyumba ya Mganga katika Zahanati ya Kijiji cha Mchalambuko Wilayani Kilwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, tutafanya tathmini ya mahitaji ya gharama zinazohitajika kwa ajili ya ukamilishaji wa nyumba ya mtumishi. Lakini tutatafuta fedha kwa kupitia mapato ya ndani, lakini pia na Serikali Kuu ili nyumba hiyo ikamilike na watumishi wetu waweze kuishi pale. Ahsante.

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha kukamilisha ujenzi wa majengo ya zahanati Kijiji cha Masagalu Mission, Kilindi?

Supplementary Question 5

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Wakati wa Bunge la Bajeti niliahidiwa shilingi milioni 500 kwa ajili ya uboreshaji wa vituo vya Kalenge na Nyubusozi wilayani Biharamulo. Ni lini pesa hiyo itatumwa ili huduma hiyo iweze kufanyika kwa ajili ya wananchi wa Biharamulo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Vituo hivi vya afya ambavyo viliahidiwa katika Bunge la Bajeti, ni sehemu ya kipaumble cha Serikali katika kuhakikisha kwamba tunatafuta fedha na kuzipeleka ili ujenzi uweze kufanyika. Kwa hiyo, nikuombe Mheshimiwa Mbunge uwe na Subira kidogo wakati Serikali inatafuta fedha na mara fedha zikipatikana kwa awamu tutahakikisha kwamba tunaanza ujenzi wa vituo vya afya katika maeneo hayo. Ahsante.

Name

Dr. Christina Christopher Mnzava

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha kukamilisha ujenzi wa majengo ya zahanati Kijiji cha Masagalu Mission, Kilindi?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. CHRISTINA C. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Ni lini Serikali itapeleka fedha za kumalizia Zahanati ya Kidanda katika Kata ya Itwangi – Shinyanga?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nielekeze halmashauri husika iweze kuleta taarifa ya hatua ya ujenzi wa boma hilo la zahanati ulipofikia, ili liweze kuingizwa kwenye mpango wa kutafutiwa fedha kwa ajili ukamilishaji wa jengo hilo. ahsante.

Name

Kasalali Emmanuel Mageni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha kukamilisha ujenzi wa majengo ya zahanati Kijiji cha Masagalu Mission, Kilindi?

Supplementary Question 7

MHE. KASALALI E. MAGENI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Je, ni lini Serikali itapeleka fedha za kutosha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Zahanati katika Kijiji cha Chamva ili hali fedha iliyokuwa imetumwa awali haikutosha?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, maeneo yote ambayo Serikali ilipeleka milioni 50 kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma, kwanza maelekezo ilikuwa ni kwamba boma liwe limefikia hatua ya linter. Pia, kwa tathimini zetu kwa kiasi kikubwa milioni 50 ilikuwa inatakiwa kukamilisha boma. Sasa kama eneo hili la Chamva fedha ilipelekwa lakini boma halikukamilika, kwanza tunataka Mkurugenzi wa Halmashauri atupatie taarifa rasmi kwa nini milioni 50 hazikutosha kukamilisha boma, tujiridhishe na matumizi sahihi ya fedha hizo.

Mheshimiwa Spika, pili, wanatakiwa kutenga fedha kwenye mapato ya ndani ili kuhakikisha kwamba wanakamilisha jengo la Zahanati ya Chamva. Ahsante.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha kukamilisha ujenzi wa majengo ya zahanati Kijiji cha Masagalu Mission, Kilindi?

Supplementary Question 8

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Mimi katika Jimbo langu la Sikonge, wananchi pamoja na Mfuko wa Jimbo tumeshirikiana. Tuna maboma 14 ambayo yanahitaji milioni hamsini hamsini, jumla milioni 700 na halmashauri haina uwezo. Je, Serikali kuu haiwezi kutusaidia tuweze kumaliza maboma hayo 14.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Safari ni hatua, Serikali imeendelea kupeleka fedha katika Jimbo la Sikonge kwa ajili ya umalizaji wa maboma. Nimhakikishie kwamba tutaendelea kwa awamu kutafuta fedha ili kuendelea kukamilisha maboma haya. Ahsante.

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha kukamilisha ujenzi wa majengo ya zahanati Kijiji cha Masagalu Mission, Kilindi?

Supplementary Question 9

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kuniona. Kwa muda mrefu Jimbo la Kibamba halijapata fedha hizi za mambo na ninayo maboma ya zahanati ya Saranga King’azi na Msakuzi. Je, ni lini Serikali inaweza kuweka commitment hasa kwa mwaka huu 2023/2024 ili waweze kuleta fedha tumalizie maboma haya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Maboma ya zahanati katika Jimbo la Kibamba Halmashauri ya Ubungo yatatafutiwa fedha kwa ajili ya ukamilishaji. Hata hivyo, nitumie fursa hii kuwakumbusha wakurugenzi wa Manispaa zenye mapato makubwa kama Ubungo na Manispaa nyingine, kuweka kipaumbele cha fedha za miradi ile asilimia 40,60 kwa ajili ya ukamilishaji wa maboma hayo wakati Serikali ikiendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kukamilisha maboma hayo. Ahsante.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza: - Je, lini Serikali itatoa fedha kukamilisha ujenzi wa majengo ya zahanati Kijiji cha Masagalu Mission, Kilindi?

Supplementary Question 10

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Je, ni lini sasa Serikali itatuletea fedha za kujenga chumba cha maiti na jengo la emergence katika Kituo cha Malawi katika Kata ya Vituka ukizingia sasa Temeke hospitali ni ya kimkoa na si kituo tena.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, mpango wa Serikali ni kuhakikisha kwamba huduma zote za msingi zinapatikana katika maeneo ya vituo vya huduma ikiwemo majengo haya ya mortuary na majengo ya dharura. Ndiyo maana mwaka 2022 majengo ya dharura zaidi ya 80 yamejengwa, majengo ya ICU yamejengwa.

Mheshimiwa Spika, Kwa hiyo, naomba nitumie fursa hii kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, tutafanya tathimini ya majengo hayo tujue gharama zake lakini pia tuone mapato ya ndani yatachangia kiasi gani na Serikali kuu itachangia kiasi gani. Ahsante.