Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. SALMA R. KIKWETE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Jimbo la Mchinga kutoka kwenye chanzo cha maji cha Ng’apa?

Supplementary Question 1

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza ninaishukuru Serikali kwa majibu yake mazuri na yenye matumaini makubwa kwa jengo la Mchinga na kwa Manispaa yetu ya Lindi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nina swali la nyongeza, sambamba na hili tuna suala zima la ukarabati kwenye Kata yangu ya Milola na chanzo kiko kule Chipwapwa, fedha tulizozipata ni shilingi milioni 50 na jana wamesaini mkataba, lakini mahitaji ni shilingi milioni 490.

Je, fedha zilizobaki zitapatikana lini na hii ikiwa na maana kwamba huu ndiyo mwisho wa bajeti wa 2021/2022?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Salma Rashid Kikwete, Mbunge wa Jimbo la Mchinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kata aliyoitaja ni kweli fedha zimekwenda kwa utangulizi, lakini kama ilivyo kawaida kila mgao unapokuwepo tunaendelea kuleta fedha. Kwa wiki hizi mbili zilizobaki za kumaliza mwaka huu wa fedha tutajitahidi kuona uwezekano wa kuongeza fedha kadri ya mahitaji. Ahsante. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SALMA R. KIKWETE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Jimbo la Mchinga kutoka kwenye chanzo cha maji cha Ng’apa?

Supplementary Question 2

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Mradi wa Maji wa Bunda kutoka Nyabeu tayari Serikali imeshafikisha Bunda Mjini, lakini changamoto kubwa iliyokuwepo ni miundombinu ya usambazaji maji, ni ya zamani, ndiyo maana mpaka leo wananchi wameshindwa kupata maji safi na salama. Je, ni lini sasa Serikali watahakikisha wanaweka miundombinu mipya ili kata zote 14 za Bunda Mjini ziweze kupata maji safi na salama? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ester Bulaya, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama alivyokiri maji yameshafika mjini; lengo la Wizara ni kuhakikisha maji yakishafika katika maeneo ya mwanzoni, basi sasa usambaji utafuata na miundombinu ya zamani yote tunakwenda kuendelea na ukarabati kuhakikisha tunaleta mabomba na miundombinu ambayo itaendana na idadi ya watu waliopo kwa sasa. Hivyo, nipende kukwambia tu Mheshimiwa Mbunge kwamba mwaka ujao wa fedha tutaendelea na ukarabati wa mradi huu. (Makofi)

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. SALMA R. KIKWETE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji katika Jimbo la Mchinga kutoka kwenye chanzo cha maji cha Ng’apa?

Supplementary Question 3

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwenye Kata ya Nyakatuntu kuna chanzo cha maji Kitoboka, na kwenye Kata ya Songambele kuna chanzo cha maji Kitega ambacho wananchi wanapata adha kuhusu maji safi na salama. Je, ni lini Serikali itaboresha chanzo hiki lakini pia kukamilisha visima ambavyo tumetengewa kwenye bajeti? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bilakwate, kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, visima hivi ambavyo amevitaja Mheshimiwa Mbunge tunaendelea kuvifanyia kazi kuona kwamba pamoja na hivi vyanzo vya maji alivyovitaja vyote tuweze kuvitumia, lengo ni kuona tunapata maji mengi yatakayoweza kuwafikia wananchi wengi. Nimwombe Mheshimiwa Mbunge avute Subira, kazi ambayo tumeianza kwa pamoja tutakwenda kuikamilisha. (Makofi)